Bemendazole
JF-Expert Member
- Nov 14, 2020
- 2,363
- 5,883
Leo, makada wengi wa chama pendwa walitarajia Shaka angetoa orodha ya walioteuliwa kugombea nafasi za Ubunge wa Afrika Mashariki, Lakini hakufanya hivyo.
Dalili zinaonesha kuna mkwamo mahali fulani na nani apite, nani atemwe! Tathmini yangu inaonesha vigogo wengi wameleta vimemo wakipendekeza watu wao. Wengine ni watoto wa vigogo na wengine ni washirika wa karibu kiasi kwamba chama kimepata kigugumizi kisijue nani apitishwe nani aachwe.
Lakini ngoja ni wapeni mbinu, kanuni ya mchezo huu inasema, ukitaka kumuua nyani, usimuangalie usoni. Ili kupitisha majina, angalieni sifa kama kujitoa kwa mwanachama, uwezo wa mwanachama kitaaluma na kujenga hoja nk.
Msiangalie huyu ni mtoto wa mjomba, huyu tulisoma naye, mkiangalia vigezo hivyo ni sawa na kumuangalia nyani usoni na mchakato utaisha kwa maning'uniko.
Dalili zinaonesha kuna mkwamo mahali fulani na nani apite, nani atemwe! Tathmini yangu inaonesha vigogo wengi wameleta vimemo wakipendekeza watu wao. Wengine ni watoto wa vigogo na wengine ni washirika wa karibu kiasi kwamba chama kimepata kigugumizi kisijue nani apitishwe nani aachwe.
Lakini ngoja ni wapeni mbinu, kanuni ya mchezo huu inasema, ukitaka kumuua nyani, usimuangalie usoni. Ili kupitisha majina, angalieni sifa kama kujitoa kwa mwanachama, uwezo wa mwanachama kitaaluma na kujenga hoja nk.
Msiangalie huyu ni mtoto wa mjomba, huyu tulisoma naye, mkiangalia vigezo hivyo ni sawa na kumuangalia nyani usoni na mchakato utaisha kwa maning'uniko.