Mkuu wa Wilaya Vs Kamanda wa Polisi

Mkuu wa Wilaya Vs Kamanda wa Polisi

Hapo Polisi wana kosa la nidhamu na wanapaswa kuwajibishwa, Mkuu wa Wilaya ni sawa na raisi katika Wilaya, maamuzi yake OCD hapaswi kuyapinga hata kama kakosea. Huyo ni boss wake na anapaswa kutii pasipo kuhoji. OCD ni Mwakilishi wa IGP na DC ni Rais.
Umeshaambiwa ni kielelezo, unafikiri siku watu wakikomaa si itaoneka polisi wamepoteza kielelezo?

Hakuna doa baya kama kupoteza kielelezo
 
Amri za Polisi zipo kama ifuatavyo;-
1. Amiri Jeshi Mkuu
2. IGP
3. Commisioner of Police
4. Deputy Commisioner of Police
5. Senior Assistant Commisioner of Police
6. Assistant Commisioner of Police
7. Senior Superitendent of Police
8. Superitendent of Police
9. Assistant Superitendent of Police
10. Inspector of Police
11. Assistant Inspector of Police
12. Sergeant Major
13. Staff sergeant
14. Sergeant
15. Corporal
16. Police Constable

Umeona wengine hapo? PGO 101 imetaja watu wanaotakiwa kupewa heshima (Complement) katika mihimili mitatu ya dola . Complement hizo haziwapi Amri za moja kwa moja (Orders) kwa Police bali maelekezo (directives). Waziri/Mkuu wa Mkoa/Mkuu wa Wilaya (executives), Spika wa bunge/ wabunge (Regislatures) na Majaji na Mahakimu (Judiciary) wanapokea Complement zao na wanaweza kutoa directives ambazo baada ya kupitiwa kitaalamu na watoa amri wanaandaa amri ya utekelezaji. Wakiona kuna ukakasi wanaachana nazo. Hawalazimiki kufanya kitu wanachoelekezwa kama mizani ya kisheria haijakaa vizuri
Inapotokea Polisi anapokea mtu ambae kaamuriwa kumweka ndani na watoa maelekezo, yule mtu akafia ndani ya selo za Polisi bila kuwa na sound accusation atakayechukuliwa hatua sio mtoa maelekezo bali mkamataji, ndio maana Polisi wanapoomba muda wa kutafakari ukamataji wana maana nzuri tu kuwa wanapima kwenye mizani ya kisheria wakichukulia tahadhari zote
 
Nanikakudanganya polisi ni jenshi??? Rufi shule wewe ungekuwa unawaonawakati wakumuapisha Rais
Kumuapisha Rais na ni jeshi au sio jeshi vinahusiana nini?
 
Kama DC alitoa maagizo yanayopingana na utekelezaji au mchakato wa uchukuaji wa sheria OCD alipashwa amshauri DC siyo kupingana naye hadharani
Polisi anashauri wakati kielelezo kipo salama, angeshaurije huku kielelezo kinaondoka?
Akishauri halafu DC akaelewa ndio wangeingia mtaani kukuchukua kwenye mahindi ya watu?
 
sasa wewe zezeta square mbona hujasema police ni jeshi gani la ardhini,angani,majini au jeshi la namna gani?yaelekea wewe ni wale police mlioingia huko idarani kwa vyeti vya kufoji.kobe jike wewe
Acha matusi, kubali hufahamu
 
Polisi anashauri wakati kielelezo kipo salama, angeshaurije huku kielelezo kinaondoka?
Akishauri halafu DC akaelewa ndio wangeingia mtaani kukuchukua kwenye mahindi ya watu?
Nakutumia video hapa, walikuwa kwenye store ya kutunzia vielelezo. Sio shambani.
 
Nakutumia video hapa, walikuwa kwenye store ya kutunzia vielelezo. Sio shambani.
Habari inavyoeleza DC alitoa ruksa kielelezo kigawiwe kwa wananchi, ilikuwa ni lazima kizuiwe ndio wakashauriane bila hivyo OCD asingezuia wangekuwa wanashauriana huku amri ya DC ikiendelea kutekelezwa, ingekula kwa OCD
 
Wakuu wa mikoa /wilaya ni mizigo na hasara kwa Taifa. wengi wao!
 
Amri za Polisi zipo kama ifuatavyo;-
1. Amiri Jeshi Mkuu
2. IGP
3. Commisioner of Police
4. Deputy Commisioner of Police
5. Senior Assistant Commisioner of Police
6. Assistant Commisioner of Police
7. Senior Superitendent of Police
8. Superitendent of Police
9. Assistant Superitendent of Police
10. Inspector of Police
11. Assistant Inspector of Police
12. Sergeant Major
13. Staff sergeant
14. Sergeant
15. Corporal
16. Police Constable

Umeona wengine hapo? PGO 101 imetaja watu wanaotakiwa kupewa heshima (Complement) katika mihimili mitatu ya dola . Complement hizo haziwapi Amri za moja kwa moja (Orders) kwa Police bali maelekezo (directives). Waziri/Mkuu wa Mkoa/Mkuu wa Wilaya (executives), Spika wa bunge/ wabunge (Regislatures) na Majaji na Mahakimu (Judiciary) wanapokea Complement zao na wanaweza kutoa directives ambazo baada ya kupitiwa kitaalamu na watoa amri wanaandaa amri ya utekelezaji. Wakiona kuna ukakasi wanaachana nazo. Hawalazimiki kufanya kitu wanachoelekezwa kama mizani ya kisheria haijakaa vizuri
Asante saana mkuu, uko smart sana kiongozi , sasa nimeelewa ndio maana mkuu wa polisi wa uganda alimdindia waziri wa ulinzi na usalama wa uganda
 
Kama DC alitoa maagizo yanayopingana na utekelezaji au mchakato wa uchukuaji wa sheria OCD alipashwa amshauri DC siyo kupingana naye hadharani
Ok sasa tuone kama DC ana uwezo wa kumfukuza kazi OCD au kumwajibisha
 
Back
Top Bottom