Mkuu wa Wilaya Vs Kamanda wa Polisi

Mkuu wa Wilaya Vs Kamanda wa Polisi

Hawa wakuu wa wilaya wa bwana mkubwa hawa sijui wanaongozwa na nini?

Wewe mtu mzima kabisa unashindwa kujua kwamba kitu anachokamatwa nacho mtuhumiwa huwa kinatumika kama kielelezo katika kesi yake?

Basi hapo kajiona yeye anajua kuliko kamanda wa polisi.
 
Mkuu wa Wilaya ni sawa na raisi katika Wilaya, maamuzi yake OCD hapaswi kuyapinga hata kama kakosea..
Ndo maana wanasema Tanganyika ni kisiwa cha amani. Yaani DC afanye madudu na aachwe tu kisa yeye ni "sawa na Rais wilayani"!?
 
Kama DC alitoa maagizo yanayopingana na utekelezaji au mchakato wa uchukuaji wa sheria OCD alipashwa amshauri DC siyo kupingana naye hadharani
DC kama anafikiri vizuri inabidi ajikalie kimya tu kwani agizo lake lilikuwa linaenda kuvuruga kama sio kuharibu kabisa kesi.

Tulimkamata na mbolea, vielelezo viko wapi??
 
Mkuu wa wilaya anafanya maamuzi kwa mzuka...nimewaonea huruma wananchi maana walishajitwika viroba vya mbolea kichwani kabla ya kushushwa kwa mabomu ya machozi.
Walijua free lunch [emoji38][emoji38][emoji38]
 
Polisi siyo jeshi kama unavyoota ndoto,polisi ni raia kabisa kama raia wengne tofauti ni kwamba yeye anajua guu pande guu sawa ,

Polisi ni nanga tena wa demo ,mbona huyo mkuu wa wilaya hakumuita kamanda wa kikosi cha kambi ya jeshi hapo kwake atoe maelezo fooolish sana huyo mkuu wa wilaya na polisi wake
Mbona povu mjomba, kasome katiba ya nchi utajua majeshi ya nchi.. Yani kusikia polisi ushapata wivu wamekuzidi nini hao polisi.
 
hapo ndo patamu DCs kiufupi hawanaga kazi kabisa ni are ghosts in government payrolls... hata ukimuuliza kama ni mwanasiasa au mtumishi wa umma haelewi....hapo naona DC yupo sawa na hayuko sawa inategemeana na sababu ya kukamata mbolea...kama wahusika walenda mahakamani...ila DC anamwajibisha OCD coz ndiye mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya...anawasimamia makamanda wote wa wilaya wanaohusika na ulinzi.....mimi huwa napenda nikisikia DC akimkurupusha mkurugenzi unaona wanaangaliana tu mwisho wa siku Dc anavyata mkia anaendelea kupiga tumba........kazi zao ni issues za utoro wa wanafunzi, uzururaji na nyingine kama hizo ...hawaderve bendera kwenye gari zao kabisa
Tofautisha Jeshi la Polisi na Kamati za Tamisemi. Hivi mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama anaweza kutangaza vita eneo lake akapeleka Jeshi la Wananchi kupambana? Polisi hawafanyi kazi zao under Tamisemi. Wizi wowote unatakiwa kufanyiwa upelelezi na vielelezo vipelekwe mahakamani, DC anawezaje kugawa vielelezo? Itakuwa nchi ya kwanza makosa ya jinai kusimamiwa na wanasiasa.
 
Hapo Polisi wana kosa la nidhamu na wanapaswa kuwajibishwa, Mkuu wa Wilaya ni sawa na raisi katika Wilaya, maamuzi yake OCD hapaswi kuyapinga hata kama kakosea. Huyo ni boss wake na anapaswa kutii pasipo kuhoji. OCD ni Mwakilishi wa IGP na DC ni Rais.
Nitashangaa kama wapo watanzania wanaodhani Mkuu wa Wilaya ni sawa na Rais kwa Jeshi la Polisi, kumbuka Jeshi la Polisi halipo chini ya Serikali ya Wilaya bali Amiri Jeshi Mkuu mmoja tu. Vitabu vya Polisi vinasema zipo Rank ambazo zinawajibika kuwapigia saluti ma-DC na sio zote. Kwa hiyo ukikuta OCD anapiga saluti hiyo is just ofa tu
 
Hapo Polisi wana kosa la nidhamu na wanapaswa kuwajibishwa, Mkuu wa Wilaya ni sawa na raisi katika Wilaya, maamuzi yake OCD hapaswi kuyapinga hata kama kakosea. Huyo ni boss wake na anapaswa kutii pasipo kuhoji. OCD ni Mwakilishi wa IGP na DC ni Rais.

Nyie ndio mnasababisha Waafrika tunatukanwa.
 
Tofautisha Jeshi la Polisi na Kamati za Tamisemi. Hivi mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama anaweza kutangaza vita eneo lake akapeleka Jeshi la Wananchi kupambana? Polisi hawafanyi kazi zao under Tamisemi. Wizi wowote unatakiwa kufanyiwa upelelezi na vielelezo vipelekwe mahakamani, DC anawezaje kugawa vielelezo? Itakuwa nchi ya kwanza makosa ya jinai kusimamiwa na wanasiasa.
Labda uniambie ULINZI maana yake nini kwa tafsiri yako....tofautisha kusimamia na kutekeleza DC anamuamuru OCD na OCD anatii amri bila swali...issue ya kukusanya ushahidi na mwndelzo wa kesi watafanya wanaohusika...DC anaweza kutangaza hali ya hatari katika mamlaka yake...issue ya vita hata Kwa mujibu wa katiba ya nchi hii hata Rais peke yake hawezi kutangaza...vitu vingine siwezi kukujibu ni kama nakusaidia kufikiri its not fair..wilaya nyingi zina captain wa Jeshi la wananchi ambaye nae yupo chini ya Dc pia ....majanga yoyote yanayotokea ndani ya wilaya au matatizo ya kiulinzi DC anahusika moja kwa moja na maana yake ni kwamba anaviamuru vikosi husika kutatua tatizo
 
Back
Top Bottom