Mkuu wa Programu JamiiForums: Taasisi za serikali zinapaswa kutambua JamiiForums ni mtandao wa ndani, tuuthamini

Aug 29, 2022
24
39
1708677785505.png

Mkuu wa Programu JamiiForums, Ziada Seukindo amesema taasisi za serikali zinaruhusiwa kutumia mtandao wa JamiiForums kwa sababu ni Jukwaa la mtandao kama majukwaa ya mitandao ya kijamii mengine duniani.

“Taasisi za serikali zinapaswa kutambua JamiiForums ni mtandao wa ndani tuuthamini, baadhi hatutambui vitu vinavyoanzishwa na wataalamu wetu wa ndani sijajua kwa nini hatuna imani navyo na wakati huo huo tunakimbilia kutumia mtandao kama ‘TikTok’ wakati ‘TikTok’ yetu ya Tanzania ni Jamii Forum,” amesema Ziada.

Ziada amesema hayo wakati akiwasilisha mada ya mitandao ya Kijamii wakati wa mkutano wa Mafunzo wa 108 wa watayarishaji wa vipindi vya Elimu kwa Umma ulioandaliwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) unaofanyika mkoani Mwanza.
 
Mkurugenzi wa TBC amesema....
Jamiiforums sio chombi cha mtandao wa ndani, bali ni chombo cha habari na akawashauri jamiiforums watafute wahariri wazuri.
Dahhhhh....
Ila kumbe humu ndani kuna piskali eehhhh😜
 
M
Mkurugenzi wa TBC amesema....
Jamiiforums sio chombi cha mtandao wa ndani, bali ni chombo cha habari na akawashauri jamiiforums watafute wahariri wazuri.
Dahhhhh....
Ila kumbe humu ndani kuna piskali eehhhh😜
mmmh kijana punguza tamaa!
 
Shida ya JF imekaa zaidi kama blog,
Inakuwa haina tofauti na Millard ayo 😂

Serious, m nashauri jf waongeze page ambayo itaruhusu interaction kama ile ya twiter humu,

Kucopy inaruhusiwa, mbna Zuck alicopy
 
Weeh!

Tunataka private yetu ..naona zinatumika mbinu za digital kubana watu ..waogope kutoboa tobo!
 
Back
Top Bottom