Mkuu wa Mkoa wa Iringa hajui Sheria

Mkuu wa Mkoa wa Iringa hajui Sheria

DC hapi kafanya kitu sicho yan.ni mnyama.daaah
Magufuli amshauri kijan wake.mamb ya kuamua mambo km mpo bar,sio kabisa.
 
Hivi huyu Hapi ni mtoto wa Warioba, kama ni wake basi hapa Warioba aliteleza au alipakaziwa. Hizi co akili ya warioba, mara nyingi mtoto hurithi matendo au akili.
Mkuu, hi imeingiaje!? I mean Warioba na Hapi, wapi na wapi!?
 
Dogo kajitoa ufahamu. Sijue ana taaluma gani maana duu.
 
Nachelea kukubaliana na maelezo ya mshitaka (mzee aliebomolewa), kwamba kila alipo kwenda kupanga huyo diwani alimfuata! Je, Iringa mjini hakuna vyombo vya sheria? How can someone be harassed to that extent and not take action to open a case!? Kitu kingine kilicho nishangaza nihao watendaji wa manispaa walokiri kwamba mzee alionewa harafu wakumsaidia hata kumpa ushauri tu!? Yaani hata kuripoti hii kwa Dc hapana jamani! There's more ambiguity in this case! At the of the day the truth will known!
 
Nimesikiliza nakuona video ya Mkutano wa Hapi na wanaringa. Magufuli anaipeleka nchi pabaya. Hawezi kuwapa vitoto ukuu wa mkoa au wilaya, watoto ambao hawajielewi wala hawajui sheria inasemaje. Hapi kamweka Diwani wa CHADEMA ndani eti kwasababu ya kuvunja nyumba ya mwanaccm.

Nimuulize Hapi je huyu mwanaccm nyumba yake iliyovunjwa ilijengwa ndani ya hifadhi. Huyo aliyevunjiwa wala siyo nyumba kwani ilikuwa bado inajengwa. Mwenyewe akasema ilikuwa hata aijawekwa paa.

Manispaa wanao uwezo wa kubomoa nyumba yoyote hata likiwa imeisha kama atakuwa ajafuata sheria. Halafu huyu Diwani hana mgambo, mgambo ni wa manispaa kwahiyo nyumba ilivunjwa na MANISPAA YA IRINGA SIYO DIWANI WA CHADEMA.

Halafu kwanini alikuwa hataki kumpa nafasi diwani nae aeleze jinsi ilivyokuwa. Yaani yote haya kwasababu manispaa inaongozwa na Opposition. Magufuli anaiangamiza nchi.

Hivi huyu Hapi ni mtoto wa Warioba, kama ni wake basi hapa Warioba aliteleza au alipakaziwa. Hizi co akili ya warioba, mara nyingi mtoto hurithi matendo au akili.
 
Maswali yaliyopaswa kuulizwa ni :
1. Je hiyo sehemu alipokuwa anajenga huyu Mheshimiwa imetengwa kwa ajili ya makazi?
2. Kama sehemu haikutengwa kwa ajili ya makazi, alipataje kibali cha ujenzi?
3. Na je hicho kibali alichokuwa nacho ni kwa eneo ambalo alikuwa anajenga?
4. Je alipata kibali cha kuendelea kujenga baada ya msingi wa nyumba kukaguliwa?
5. Je Halmashauri husika iliwahi kumtaka anayejenga hiyo nyumba kusita kujenga kwa maandishi? na kwa kuweka alama kwenye nyumba kumtaka asiendelee na ujenzi?
6.Je kuna maelekezo yeyote ya maandishi ya kuwaagiza wale mgambo kwenda kubomoa ile nyumba?

Kwa kumtia ndani huyu mama kwa kosa la kubomoa nyumba iliyokuwa inajengwa kwenye eneo lilizouiwa kujengwa kuna maana kuwa zuio hilo limeondolewa na watu waote ruksa kuendelea jenga katika eneo hilo. Hivi Mkuu wa Mkoa ana mamlaka ya kuondoa zuio hilo?

Kama nilisikia vizuri, mlalamikaji alikuwa anamtumhumu huyu mama kwa kumzuia kulala kwenye eneo ambalo anafanyia biashara. Ninavyojua mimi, hairuhusiwi kubadilisha eneo la biashara kuwa la makazi au makazi/biashara bila kupeleka maombi kwenye mamlaka husika. Kutumia sehemu ya biashara kunaweza kusababisha majanga kama moto ( kutokana na vibatali, sigara, au jiko la kupikia chakula) n.k.

Mwisho ni je hili shauri lisingeweza kushughulikiwa bila kumtia ndani yule mama? Yule mama angevuruga vipi hili shauri kwa kuwa nje?

Mimi nahisi mlalamikaji ndie aliyekuwa anawaambia watendaji kuwa hawawezi kumfanya kitu kutokana na nafasi yake ya kisiasa. Mheshimiwa alitakiwa atumie busara katika kutatua hili shauri ili kuepuka kuonekana amefanya maamuzi ya kisiasa kwenye masuala ya kiutawala. Kwa kufanya hivyo hajakitendea haki chama chake.

Amandla.............
hivii mkuu.. umejiuliza huyu dogo Hapi alikotoka Kino ameharibu kiasi kutia aibu halafu Jiwe kam'bandua na kum'bandika ukuu wa mkoa?

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom