Mkuu wa Mkoa Arusha aropoka mei mosi

Mkuu wa Mkoa Arusha aropoka mei mosi

Umenikumbusha mbali sana mkuu,kipindi nasoma kukawa na mwanafunzi anaswaki na kiroba mkononi nahisi ndio huyu saivi kabadilisha lishe
Jamaa breakfast yake itakuwa ni kuberi
 
Waandishi wa habari waungane pamoja kupinga vitisho hivyi hasa ukiunganisha na kuteswa kwa Kibanda na mfanano wa kauli ile ya Membe.
Chonde chonde wanahabari watanzania, juzi spika makinda amewakejeli wanahabari bungeni kama vile tasnia ya habari ni tasnia isiyotakiwa kwenye jamii.
Leo muwakilishi wa Kikwete hapa Arusha anawatolea wanahabari maneno ya kuwatisha, nawashauri wanahabari mchukue tahadhari na serikali hii ya ccm inayotumia mafia tactics kuwatesa na kuwaua watu wote wanaotangaza habari zinazowakwaza wapiga kura dhidi ya mwenendo huu mbovu wa ccm.

Taasisi ya haki za binadamu pamoja na umoja wa wanahabari wanapaswa kushirikiana na kutoa matamko na kuiburuza serikali mahakamani kwa kutoa vitisho na kudhamiria kubaka haki ya wanahabari na watanzania kwa ujumla kupitia kwa mtendaji huyu wa serikali ambaye ni mkuu wa mkoa asiye na sifa ya uongozi hata tone moja.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Kweli sasa nimeanza kuamini huyu bwana ni mjinga kwani leo katika siku ya mei mosi Mkuu wa mkoa Arusha amesema waandishi wahabari wawe makini kuandika habari za serikali vingenevyo wawe tiyari kuweka roho zao rehani kwani serikali ina nguvuu nyingi

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums


Kauli kama hizi hutumiwa na watawala na sio viongozi,Serikali ya Tanzania ina watawala kwa sasa sababu nikiyakumbuka na maneno ya Wasira kuhusu Kibanda nnachoka kabisa.Wenye nchi yao(Wananchi-Watanzania)wametulia tu na kuwapa nchi watawala wafanye vile wanataka,WAANDISHI WA HABARI FANYENI JAMBO KATIKA HILI KWA KUILAANI KAULI HII YA MKUU WA MKOA..
 
Polisi, mmeshamsikia mtesaji wa wanahabari? Kazi kwenu.
 

Alionywa
:

....huyu atakuwa na tatizo la kisaikolojia ....ukipambana na G Lema lazima uwena ubongo wa chuma....ubongo wa maji maji utayeyuka kama barafu....

cc DR Pauline
 
Polisi, mmeshamsikia mtesaji wa wanahabari? Kazi kwenu.
Namsindikiza wife ni muandishi wa habari wa gazeti la Arusha Times tunaenda kukutana na mwanasheria wa familia tufungue kesi dhidi ya jamuhuri imemtishia wife uhai wake kama mwanahabari kupitia kauli hii ya kikatili kutoka kwa muwakilishi wa jamuhuri ya tz hapa arusha.
Kauli ya Mkuu wa mkoa ni kauli ya Jamuhuri.

CC to Bashe, Tundu Lissu, James Millya, Riziwani Kikwete, Rostam Aziz, Mary Chatanda na Mzee Mwanakijiji

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli hiyo kauli imetolewa?
Alikuwa ktk mkutano wa hadhara au na waandishi peke yao?
Majibu ili tumpe adhabu hata ya kumlaumu tu.
 
Kweli sasa nimeanza kuamini huyu bwana ni mjinga kwani leo katika siku ya mei mosi Mkuu wa mkoa Arusha amesema waandishi wahabari wawe makini kuandika habari za serikali vingenevyo wawe tiyari kuweka roho zao rehani kwani serikali ina nguvuu nyingi

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums

Na waandishi wa habari Tanzania nzima wanakenua menu wanapoambiwa hivi? Nisipoona wamemchukulia hatua kali sana nitashangaa kweli kweli!!!!
 
Hawa ni aina ya viongozi ambao ni wachochole kifikra na hudhani kuwa mabavu ndio kila kitu lakini sasa amekanyaga pabaya.Hajui kuwa hapo ni Arusha?
Namsihi ajivua ukuu wa mkoa arejee kwenye kazi yake ya Utarishi Posta.

HAYA NDIO MATATIZO YA KUBEBANA-KWANI ALIKUWA TARISHI POSTA MBEYA HADI MKUU WA MKOA NI BORA ANGEPEWA MPIGA DEBE
 
Utawala bana si kila mtu anaweza kutawala. Haya ni matokeo ya wrong recruitment zinazofanyika katika nafasi nyeti.
 
Ile Kesi ya SMS ya Vitisho inamsumbua sana akili Mulongo .
 
Kah!,sasa tumekwisha kama ndio utawala bora huu
 
..meno yangu yameoza hata akining'oa sio ishu sana..
 
Pamoja na kwamba structure hii ya ukuu wa mkoa sijui wa wilaya siikubali, ningependa katika kipindi hiki mfumo huu una exist wachaguliwe watu makini kwani si kila mtu anaweza kushika ukuu wa mkoa au wilaya kwa kigezo kwamba ni mwanachama wetu au kasoma, inatakiwa waende mbele zaidi kama zamani kwa kuangalia uzoefu wake katika mambo mbalimbali tena ikiwezekana awe ameshapitia katika utumishi wa Umma maana unampa mtu UDC kwa kumuokota mtu tu akienda huko wilayani anashindwa kufanya kazi na wakurugenzi na idara mbalimbali za serikali kwa kuwa hata jinsi zinavyofanya kazi hajui na JD yake pia hajui na kwa kuwa amekariri kwamba yeye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama anabaki kuwa mbabe tu. Mbona zamani pamoja na kwamba mfumo una mapungufu jamaa walikuwa wanafanya kazi vizuri tena walikuwa hawajionyeshi waziwazi kama ni chama tawala (kuna shida sehemu kiukweli inabidi irekebishwe)
 
Sasa mbona mnabisha? nani hajui serikali ina nguvu nyng? Ina akina Ighondu, zoka, michuzi, KOVA, Mulongo n.k anayebisha amulize kibanda na ulimboka
 
Namsindikiza wife ni muandishi wa habari wa gazeti la Arusha Times tunaenda kukutana na mwanasheria wa familia tufungue kesi dhidi ya jamuhuri imemtishia wife uhai wake kama mwanahabari kupitia kauli hii ya kikatili kutoka kwa muwakilishi wa jamuhuri ya tz hapa arusha.
Kauli ya Mkuu wa mkoa ni kauli ya Jamuhuri.

CC to Bashe, Tundu Lissu, James Millya, Riziwani Kikwete, Rostam Aziz, Mary Chatanda na Mzee Mwanakijiji

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums


Vipi unakwenda na maandamano au utatoa tamko?
 
Mi naona Lema ndio awe mkuu wa mkoa....Sipati picha babake....maandamano na mikutano ya hadhara kila kukicha ,kudadeki...
Tutaandamana kweli mpaka mafisadi wote mkimbie nchi.
 
Back
Top Bottom