CHADEMA
Political Party
- Apr 13, 2013
- 495
- 2,540
- Thread starter
- #61
Dkt. Slaa "Watanzania tulieni, tulieni, tulieni. Wingi wenu hapa na kunisubiri kwa muda mrefu namna hii tangu mchana kwenye jua kali ni ishara kubwa ya upendo wa dhati kwa chama chenu na viongozi wenu, asanteni sana sana sana Kahama.
"Chama hiki ni chenu, kipo kwa ajili ya kuwatumikia na kusimamia maslahi na matakwa yenu. Hakiwezi kuwa chama legelege. Ni lazima ili kiweze kuwasemea watu, kwanza muhimu kiweze kusimamia misingi yake, ikiwemo katiba, kanuni, maadili na itifaki, mambo ambao hata CCM hawana pamoja na ukongwe wao.'
"Wakati wa kampeni 2010 tuliwaambia tutasimama kidete kwa ajili yenu kuwavusha kutoka hapa kwenda nchi ya matumaini. Ni lazima mtuone hivyo bila chembe ya shaka kuwa chama chenu ni imara, kinaweza kusimamia misingi yake ambayo ni pamoja na katiba yake, kisha tutakuwa na ubavu wa kupigania maslahi yenu."
"Haya mambo tunayopitia sasa wapo wanofikiri yatatukwamisha, tunawaambia ndiyo kwanza yanatukomaza na kutuimarisha kuwa chama imara kwenda kushika dola," Dkt. Slaa leo mjini Kahama.
"Chama hiki ni chenu, kipo kwa ajili ya kuwatumikia na kusimamia maslahi na matakwa yenu. Hakiwezi kuwa chama legelege. Ni lazima ili kiweze kuwasemea watu, kwanza muhimu kiweze kusimamia misingi yake, ikiwemo katiba, kanuni, maadili na itifaki, mambo ambao hata CCM hawana pamoja na ukongwe wao.'
"Wakati wa kampeni 2010 tuliwaambia tutasimama kidete kwa ajili yenu kuwavusha kutoka hapa kwenda nchi ya matumaini. Ni lazima mtuone hivyo bila chembe ya shaka kuwa chama chenu ni imara, kinaweza kusimamia misingi yake ambayo ni pamoja na katiba yake, kisha tutakuwa na ubavu wa kupigania maslahi yenu."
"Haya mambo tunayopitia sasa wapo wanofikiri yatatukwamisha, tunawaambia ndiyo kwanza yanatukomaza na kutuimarisha kuwa chama imara kwenda kushika dola," Dkt. Slaa leo mjini Kahama.