Mkutano wa Dkt. Slaa mjini Kahama - Dec 4, 2013

Mkutano wa Dkt. Slaa mjini Kahama - Dec 4, 2013

Mzee slaa kweli kazeeka hiyo picha mnaiona wakuu halafu mkutanomgani unaanza saa kumi na mbili huu ni uongo.
 
Nashangaa sana wana ccm uchwara na mafisadi kama .......... kung'ang'ania kuipa promo chadema wakati katibu mkuu wetu kinana amedoda vya kutosha mbeya leo na kuishia kufanya mkutano wa ndani na kukagua tazara ambayp imefilisiwa na ccm mafisadi
 
wekeni picha zakutosha hapa JF kuzime ngebe za wana zito.
sisi wanachadema roho kwatu
 

Dkt. Slaa baada ya kuhutubia kwa takriban dakika 30, akiwaaga wananchi waliokuwa na shauku ya kumsikiliza wakiwa wamemsubiri zaidi ya masaa 4.

Pamoja na kuwa na kiu ya kuendelea kumsikiliza, wakipaza sauti 'endelea endeleea, endelea' wananchi walisikiliza kauli ya Dkt. Slaa pale alipowaambia kuwa anapaswa kuwahi kikao cha ndani hivyo akawaahidi kuwa atapanga mkutano mwingine ili kufidia masaa 'yaliyopotea' leo, ikiwa ni ishara ya heshima yake kwa wananchi hao kumsbiri uwanjani kwa muda mrefu kiasi hicho.




Hakuna mkutano wa saa kumi na mbili huu ni upotoshaji wa hali ya juu.
 
1452339_558673044208406_2063836110_n.jpg
TATIZO NI HICHO KITI USILIE
 
Mkutano saa kumi n mbili?hahhaa au mlisubr bus toka moshi nn lifike kujaza raia?
 
Chadema mnatumia nguvu nyingi sana kupambana na Zitto lakini mmeishachelewa.
 
Dr.slaa amefika hapa Kahama saa 11na nusu,na amepokelewa na bodaboda 5 ambazo walichangiwa sh.5000 kutoka kwa viongozi kadhaa walioambatana na Dr.slaa,hapo awali Vijana wa chadema walionekana wakizunguka maeneo ya kahama stendi kuomba madreva Bodaboda wahudhurie mapokezi ya Dr.slaa lakini hali haikuwa nzuri kwani asilimia 90 ya madreva waligoma kuifanya hivyo.Wakati akielekea eneo la Mkutano Dr.slaa alipokelewa na mabango yanayosema"CHADEMA BILA ZITTO HAIWEZEKANI,TUACHIENI CHAMA CHETU,ENDELEENI NA UBAGUZI WENU",Baada ya kupanda jukwaani Slaa alipokelewa na Mawe,na matusi ya kejeli sana kutoka kwa Wananchi wachache waliokuwepo eneo la Mkutano.
Dr.slaa aliomba Vijana wake wa usalama watulize ghasia za wananchi,kisha akazungumza maneno machache tu kwa kusema Naomba maswala ya Zitto mtuachie sisi tutayamaliza,Mkutano nauahirisha hadi Jumapili jioni hapahapa Kahama.Kwahiyo Mkutano Kahama hadi Jumapili.
 
saa 12:15? kwani kwa kawaida mkutano unatakiwa uishe saa ngapi? yaani toka saa 8-12 watu wamesubiri tuu bila sababu ya msingi
 
mpunguzieni Babu mlolongo wa safari na vituo vya kuhutubia ili kuleta ufanisi wa ziara yake. Chadema note wananchi hawana shida ya kuona sura ya Dr Slaa kwa dk 20 bali wamesubiri kwa masaa 4 kusikiliza sera na dira ya chama. kama ingekuwa mkutano wa dk20 wangekusanyika uwanjani saa 12 kamili jioni
 

Huu ndiyo mkutano wa Dkt. Slaa leo Kahama mjini ambao umeanza majira ya saa 12.15 jioni ambapo watu wamekuwepo uwanjani tangu saa 8 mchana kama walivyotangaziwa.

View attachment 124850
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilibrod Slaa akiwahutubia wanachi wa mji wa Kamaha na vitongoji vyake, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kukagua na kuimarisja uhai wa chama katika mikoa ya Shinyanga, Kigoma, Tabora na Singida, uliofanyika kwenye Uwanja wa CDT mjini Kahama jana. (Picha na Joseph Senga)


View attachment 124852
Katibu Kuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (chadema), Dk. Willibrod Slaa akiagana na wananchi wa mji wa Kahama baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara kwenye Uwanja wa CDT mjini huo jana, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuimarisha uhai wa chama katika mikoa ya Shinyanga, Tabora, Kigoma na Singida. (Picha na Joseph Senga)
Kurungezi ya Habari au kurugenzi ya uongo mmeamua kutengeneza picha Slaa anahutubia, teh teh teh.
 
Chadema mnatumia nguvu nyingi sana kupambana na Zitto lakini mmeishachelewa.

I beg you pardon Mr Magambaz!! Unaionaje hiyo poll inayoendelea humu JF? Naona umepiga KOSA lakini ni bure tu! -- nawe umeshachelewa!! Ha ha ha.
 

Huu ndiyo mkutano wa Dkt. Slaa leo Kahama mjini ambao umeanza majira ya saa 12.15 jioni ambapo watu wamekuwepo uwanjani tangu saa 8 mchana kama walivyotangaziwa.

View attachment 124850
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilibrod Slaa akiwahutubia wanachi wa mji wa Kamaha na vitongoji vyake, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kukagua na kuimarisja uhai wa chama katika mikoa ya Shinyanga, Kigoma, Tabora na Singida, uliofanyika kwenye Uwanja wa CDT mjini Kahama jana. (Picha na Joseph Senga)


View attachment 124852
Katibu Kuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (chadema), Dk. Willibrod Slaa akiagana na wananchi wa mji wa Kahama baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara kwenye Uwanja wa CDT mjini huo jana, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuimarisha uhai wa chama katika mikoa ya Shinyanga, Tabora, Kigoma na Singida. (Picha na Joseph Senga)

Naona kuna mnazi nyuma ya picha!!!! Hii kitu ya kuchaka chua aise!!!
 
Dr Slaa azuhiliki yani ni kama Ronaldo hata ukazeje lazima apite tu, kweli we ndio raisi wa mioyo ya watanzania, kila sehemu lazima umati ambao ujabebwa na costa wala maroli ujae kukusikiliza. Go on Dr!
 
Back
Top Bottom