Mkutano wa CHADEMA viwanja vya NMC Arusha

Mkutano wa CHADEMA viwanja vya NMC Arusha

Wadau,

Katika hali ya kushangaza, ama kuchanganyikiwa mwanachama maarufu wa CDM a.k.a "Dogo janja"

Ametamka hadharani katika viwanja vya nmc kuwa kama CCM ikiboa wataigawanya nchi kama Sudan.

Wakuu sijajua sababu ya kutoa maneno haya na nina wasiwasi sana na agenda hizi za siri, ukiunganisha na post ya

pasco ya ukaskazini ambayo sikuweza kuijibu kwa kuwa nilikuwa kifungoni naona kuna siri nzito imefichika.

Nawakilisha

Sema "nawasilisha" hivi hujui tofauti ya "kuwakilisha" na "kuwasilisha" au unafanya kusudi?
 
CDM si mmo humu ndani?
Thibitisheni au mkanushe hili.
Siku zote nimesema CDM hawana sera inayoeeleweka sasa kama kuna hizi tetesi za msimamo kama huo wa siri basi twafa!

Mkuu tatizo hawa vijana bado wadogo kiumri hawawezi kuweka siri zao, lazima wazitoe LIVE kama ilivyokuwa leo.

Maana na agenda ya mkutano ikabadilika ghafla mbowe ikabidi ajikanganye!!!
 
Atamaniaye faida(kishika dola) huifadhaisha nyumba yake(Chama chake), bali achukiaye zawadi ataishi.
Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye.

Hayo ni mambo ya akupigaye shavu la kulia mgeuzie na kushoto. Ila waswahili husema adui mpende kwa kumwombea njaa.
 
Akihutubia utitiri wa wana CDM wa Arushwa Mh. Mbowe alieleza maeneo yafuatayo ambayo KIKWETE amevunja katiba Ya Tanzania.
1. Huwezi kumteua mtu awe mbunge halafu kabla hajakabidhiwa na kuapa kwa kanuni za bunge unamteua kuwa waziri kama alivyofanya jana. Wabunge aliowateua hata kabla hawajaidhinishwa na bunge yeye akawapa madaraka ya kuwa mawaziri na mbaya zaidi kumteua mtu asubuhi mbunge na jioni anakuwa waziri. Mfano mzuri wa mgongano huo ni wakati mbunge wa viti maalum wa chadema alipopeleka maswali bungeni (Akiwa ni mteule baada ya kuchukua nafasi ya Regia Mtema R.I.P) swali lake liliondolewa kwa sababu tu wabunge wa CCM walikataa kwa sababu hajaapishwa. Je? kanuni hiyo inafanya kazi kwa sababu ni mbunge wa chadema tu? CCM na Kikwete wako juu ya sheria?
2. Kuna wizara za Muungano ambazo ni Mambo ya ndani, jeshi na kujenga taifa, fedha, mambo ya nje lakini nyingine ni za Tanzania bara tu! mfano elimu ni bara tu maana zanzibar wana ya kwao au afya ni ya bara tu! Lakini leo Huseein Mwinyi ambaye ni mzanzibar anapewa wizara ya afya ya Tanzania bara! JE? Zanzibar wamewahi kufanya makosa kama hayo? au ni sisi tunajikomba kwao? kwani katiba si inasema wazi?

Naomba kuwasilisha
 
Hakika ni raha hapa mjin!waliotoka nmc wamepokelewa na mabango kwa wapiga debe stand!zingine zikisomeka 'jk kabadili tu wachezaji,no 2 kampeleka 3,hakuna jipya' nk!raha zaidi ni pale gari la polisi lilipokatiza maeneo ya soko,akina mama wakazizima kwa 'peoplesssss' wengine wakiitikia 'powerrrr'!its very fany!
 
Mkuu mtu mzima wa akili aliyeaminiwa na watu,tena wa jimbo la uchaguzi,mdomo wake inabidi achunge sana maana kauli kama tunzozisikia zaweza kuleta vita.
Huyo Nasari tayari amekuwa gugu linalofaa kung'olewa katika nchi ya Tanzania yenye amani.
mbona hatukusikia mkimsema mtoto wa m.kwe.re kama gugu linalofaa kung'olewa pale aliposema rais wa 2015 hatatoka kaskazini? mkutano umewachanganya mpaka mnaanza kuweweseka na kauli ya mtu mmoja...!
 
Huu mpango wa kuimega Kaskazini ni ajenda ya cdm tangu kimeanzishwa,na sasa ndio wameshika kasi.

Ni suala la kujiuliza,ivi kwa nini mikutano yao mikubwa inayoudhuriwa na viongozi wa kitaifa inafanyikia Arusha na Moshi pekee!!??

Mwanza, Mbeya, Sumbawanga ni wilaya Arusha na Kilimanjaro? Uwe na akili wewe.
 
JK anacheza rafu nyingi either kwa makusudi au kwa ufahamu wake mdogo na washauri wake...inasemekena alitaka kumpa uwaziri Mbatia...kajisau kuwa katiba hairuhusu serikali mseto
 
Mkutana umemalizika salama hakuna hata sisimizi alie umizwa na hakukuwepo na Polisi...
 
Wamasai wamechoka kutumika kama condomu, wameamua kuvaa magwanda
 
unajua hapa ni Ar na hapa ndiyo starting point ya ukombozi wa nchi, leo ilikuwa tunaanzisha operation mpya 'vua gamba vaa gwanda' halafu tunatembea nchi nzima
 
Thanks all kwa taarifa. Naona magamba wanajidai kuwa wamepata story ya kusimuliana vibarazani. Ujumbe umefika kwa wenye akili wameelewa. Hamna kurudi nyuma
 
Back
Top Bottom