Mkutano wa CHADEMA Arusha - Nov 29, 2013

Mkutano wa CHADEMA Arusha - Nov 29, 2013

atapelekaje huko kwenu msoga wakati mmezoea kula mihogo na kashata kwa gahawa?!!!

mswahili na maendeleo wapi na wapi?!!
majungu na umbeya pembeni mpe gahawa atakupa mpaka ya chumbani mwake, hiyo ndo jadi yenu.

muache apeleke njiro kwa wanaojua nini maana ya maendeleo.

njiro vs msoga............

ha ha ha ha ha ha!!!!
Waswahili ndiyo wapiga kura kamanda.
 
Makosa ya usaliti anayofanya Zitto ni makubwa sana sio tu anasitahili kuvuliwa nyadhifa bali kufukuzwa uanachama
Wewe subiri muda wako uishe urudi kwenye kazi yako ya zamani.
 
Watu kila siku wanachangia harusi halafu anakuja mwanasiasa anawakataza kuchagia elimu!

Hivi elimu na harusi kipi muhimu?

Chadema sifuri kabisa...

Wanachi wamechangia elimu toka nchi ipate uhuru, mbona elimu hiyo haijawahi kuwa bora hadi leo? Wananchi wanatoa michango lakini maabara hazijengwi, madarasa hayajengwi, madawati hayatoshelezi si shule za msingi si shule za sekondari. Zile shule chache zenye maabara hazina vifaa vya maabara, wanafunzi wameendelea kufanya mitihani ya practical kwa jina la alternative to practicals. Waalimu hawana taaluma nzuri kutokana na kuandaliwa kwa kutumia mtaala mbovu na hawanaga in-service training kiasi cha kuwa na akili mgando kisichoendana na mabadiliko ya teknologia na muda.

Sasa serikali kwa makusudi imeamua kutoa elimu kwa matabaka. Masikini wamelazimishwa kujenga shule zao za kata kwa ajili ya watoto wao. Shule zenyewe hazina madarasa ya kutosha, wanafunzi wanasomea wakiwa wamekaa sakafuni. Hakuna waalimu wenye taaluma wa ualimu ktk shule hizi badala yake watoto wa maskini wanafundishwa na ex-form six ambao pia either wamepata div. iv au zero, hawaqualify kwenda chuo chochote lakini wameruhisiwa kufundisha shule za kata. Shule hizi zimeongoza kwa kufelisha hapa nchini kwa kiwango cha kutisha. Lakini nani anajali ilhali watoto wa viongozi hawasomi humo? Acha watu wachangie harusi, ukichangia harusi ndoa inaonekana, wananchi wameendelea kuchangia elimu lakini hawaoni maendeleo ya michango yao. Mazingira ya shule zetu yameendelea kuwa mabovu, elimu imeendelea kuwa duni. Ya nini kuendelea kuchangia?
 
Mkuu sio mbunge mjinga tu na ambae ana tabia chafu mbunge gani anakubali kirahisi kushikishwa ukuta?!,kwa nn tusiamini kwamba ndio biashara yake siku zote?!

Katika akili ya kawaida tu mtu una bastola halafu unashikishwa ukuta kirahisi tu,hivi kwa namna anavyofahamika huyu jamaa si angeua mtu?!

kama alivyo shikishwa kikwete...
 
Mbunge wa Arusha Mjini ambaye pia Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema, Mh Godbless Lema ameeleza kushangazwa sana na kinacholazimishwa na watu na viongozi wa CCM akiwemo Mwigulu Nchemba, January Makamba, Ridhiwani Kikwete na wengineo, kuwataka Chadema wapatane na kumrudishia vyeo Bw Zitto Kabwe.

Akiwahutubia wananchi wa Arusha jana viwanja vya Kilombero, Lema aliwaachia kama swali wananchi hao watafakari wenyewe kwamba "Migogoro ndani ya Chadema ni faida kwa CCM, sasa inakuwaje wanatamani Chadema wapatane!? Wanamaslahi gani na Upatanishao huo!?"

Katika mambo mengine Lema alisema pia kwamba tofauti na maigizo mengi ya waliovuliwa vyeo kuwa kuna watu wanachoma kadi na kutoa matamko wakisaidiwa na wanapropaganda wa CCM, ukweli ni kwamba wananchi wengi wanaipongeza Chadema kwa maamuzi ambayo hakuna chama kingine nchini kimeweza kufanya.

Sentensi nyingine alizonukuliwa Mh Lema ziko hivi..
" Wanasema Chadema itaparaganyika. Chadema haitaparaganyika kwa sababu ya migogoro. Chadema itaimarika kwasababu ya changamoto na migogoro"

"Hakuna mtu maarufu zaidi kuliko Chadema. Chadema ni maarufu kuliko kiongozi yeyote. Kama mtu ni maarufu, umaarufu wake utusaidie kuimarisha chama na sio kuua chama"

Lema alihitimisha hotuba yake kwa kuzungumzia mzaha wa Serikali katika swala la gharama za umeme nchini na kuwatupia lawama wananchi kuwa ndio wanaruhusu kuonewa siku zote. Alisema tabia ya watanzania kuonekana wameshazoea umasikini na matatizo ndio mambo yanayowapa jeuri watawala kuendelea kuwanyonya. Alitolea mfano wa mashine za risiti za TRA kuwa ni mradi wa kinyonyaji kwasabu bei wanayouzia ni mara kumi ya bei halisi, kitu alichodai ni makakati wa kuwaibia wananchi kutafuta hela za kampeni 2015.

Lema pia alizungumzia utapeli unaotaka kufanywa na Lowassa jijini hapa kuteka kiwanja cha umma akidaiwa anataka kukodi kufungua Car Wash lakini mpaka sasa ameshajenga uzio wa thamani ya milioni 500. Uzio wa tofali 500mil kwa Car Wash ya kukusanya elfu 80 kwa siku??

NENO LA AMANI GOLUGWA (KATIBU WA KANDA YA KASKAZINI)
Akizungumza katika mkutano huo wa hadhara jana Nov 29, 2013 Ndg Amani Golugwa aliwataka wananchi na wapenzi wa Chadema kuwa wavulimivu, wawaamini viongozi na wawape ushirikiano kukijenga chama. Alisema mtaji mkubwa wa Kiongozi ndani ya Chadema ni UADILIFu na hivyo chama hakitasita kumuwajibisha yeyote yule bila kujali cheo chake endapo anakwenda kinyume na misingi ya chama.

Golugwa alisema kwa Chadema kipaumbele cha sasa ni ujenzi wa chama kuanzia ngazi yamsingi na hivyo kuomba ushirikiano na wala wananchi wasihuzunishe na maamuzi ya chama chao maana inalazimu kufanya hivyo ili chama kiimarike.

Aliwashangaa wale waliovuliwa vyeo kuhaha kutoa matamko na kushangazwa na utetezi wao aliouita wa kijinga kuwa eti waliandaa mkakati ili waje wamshirikishe Zitto. Golugwa akahoji ni kiherehere gani kimewakumba kumuhangaikia mwanaume mwenzao kama kweli hawajui anahitaji ama la!?

Chama cha Demokrasia na Maendeleo Mkoa wa Arusha kilifanya mkutano wa hadhara eneo la Kilombero uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi ambao muda wote walikuwa wakikatisha hotuba za viongozi kwa kushangilia na kupandishia maneno yao. Mkutano huo ulihudhuriwa na madiwani karibu wote wa Chadema Arusha pamoja na Naibu Meya Msofe, huku viongozi mbalimbali wa Wilaya na Mkoa wakiwa miongoni mwao bila kuwasahau makamanda wengine kama Ally Bananga n.k!

View attachment 124023
Amani Golugwa Jukwaani

View attachment 124024
Ally Bananga jukwaa kuu
View attachment 124026
Naibu Meya, Diwani wa Daraja Mbili Mh Msofe akiteta na wadau
View attachment 124030
 
Ndugu zangu wapenda mabadiliko, wana CHADEMA na wapinga ukoloni huu wa weusi wenzetu, nawaombeni kuwa watulivu katika kipindi hiki ambacho zitto amesababisha sokomoko ndani ya chama chetu, naamini ndicho alichotumwa kufunya. Amini usiamini wote wanaomtetea zitto na wenzake ni wana ccm.

Embu jaribu kutafakari tuhuma za zitto kuuza majimbo; angelikuwa mwanaccm na kubainika angesalimika? ccm acheni unafiki, hizi ni tuhuma nzito mno kwa mtu aliyekuwa na nafasi aliyokuwa nayo zitto.

Huu ni usaliti mkubwa sana, na alipaswa kupewa adhabu kali zaidi, wanaofuata chama kama taasisi tutabaki kuwa imara, wanaoabudu watu waende na zitto wao.


Hitimisho langu ni kuwa wote wanaomtetea zitto ni wanaccm ambao hawapendi kuona CHADEMA inafanya maazimu makini na sahii kwa wakati ili kuweka hai matumaini ya mabadiliko na ukombozi.


Taka msitake ukombozi toka makucha ya ufisadi na dhuluma ni LAZIMA.
 
Hata mimi nashangaaa ccm wanavyo ushupalia na kushauri amani cdm wakati ni hatari kwa siasa zao
 
Viongozi wengi wa ccm wameumizwa sana na maamuzi ya kamati kuu ya cdm. Hii inadhihirisha kuwa zitto ndie aliyekuwa atumike kuhakikisha cdm inasambaratika. Hata ukiangalia kwenye mitandao watu wanao coment kwa wingi na kushauri zitto asifukuzwe ni wana ccm. Inaonyesha mipango yao imefeli baada ya pandikizi lao kushtukiwa. Mimi naamini bila Zitto chadema itasonga mbele hivyo chama kimuadabishe bila wasi wasi. Kama zitto alikuwa anaihitaji uenyekiti ni kwa nini aanzishe mikakati kwa siri?. Je ni kwa nini asisubiri mda wa uchaguzi ufike agombee nafasi hiyo?. Zitto anatuhumiwa kuwa hujumu wagombea wa cdm 2010 na hakutaka kushiriki na wenzake kwenye kampeni sasa hii si inaonyesha usaliti?. Inashangaza viongozi wa ccm wanatuhumiwa kwa ufisadi, mauaji ya Tembo, madawa ya kulevya na wengine wanabaka watoto kama kapuya lkn hawawajibishwi sasa kuna uongozi kweli?. Badala yake wanaangaika na cdm inayoondoa magugu yanayotaka kuharibu chama. Chadema ni mpango wa Mungu kuwakomboa Watanzania hivyo itaendelea kupambana na mafisadi mpaka kieleweke. Ccm ni mpango wa shetani na hakika itakufa tu.
 
Ninyi watu kama wakati mwingine mnakosa majibu ni bora mkanyamaza,hivi mnataka na sisi tuige visivyo faa?mboe ajiandae kwakura,kamwe hatosalimika lazma atang'oka

Alikutangazia kuwa anagombea? au wewe ni mke wake? maana unaonekana kujua mengi yamuhuyo Mh.Mbowe.
 
...sera mojawapo ya CHAMA TAWALA ni kuhakikisha kuwa vyama vya upinzani vinakufa...,

...unakumbuka hii, "ZITTO TUNAKUHESHIMU..."

...kule! Mjengoni...!
 
Project ime-fail sasa hapo wanahangaika kurudisha mtu wao wakati kashatupwa nje.
Kina Wassira, Lukuvi, Msangi, Zoka na team zao wanalaumiwa kwa kuahindwa kupanga mkakati sahihi sasa ndiyo unaona wanajitutimua na kale kajamaa chso cha magetisita na zitto Team lkn hakuna kitu. Issue CLOSED.
 
kuna mtu mmmoja alisema humu ukiwa mfuasi wa Mungu kwa dhati kabisa shetani hawezi kukupenda kamwe.tunashangaa kuona zitto mfuasi wa chadema kwa dhati kabisa anapendwa na magamba.
 
Si ccm tu hata vyama vingine vimeumia sn,sielewi ni kwanini? Au kuna kilicho nyuma ya pazia? TAFAKARI
 
Mmelikoroga wenyewe na mlinywe mlimalize, sio muanze kutafuta mchawi na kusingizia wengine ujinga wenu
 
Ok, nadhani una jibu hebu tueleze wewe Sabodo alitoa kiasi gani na kilitumika kiasi gani kikabaki kiasi gani na kiko wapi??
Then tupe michanganuo ya misaada inayoletwa na wazungu kwa Serikali yako inayoongozwa na Chama SIKIVU.
Akijibu kuanzia leo sio mwanaChadema
 
Back
Top Bottom