Mkutano wa CCM live Singida kupitia Star tv

Mkutano wa CCM live Singida kupitia Star tv

Hao jamaa wamepewa mkate wa siku 5 tu ngoja nape na kinana warudi dar uone mchaka mchaka wao watakavyo pigika kimaisha
 
Watu wanatoka uwanjani baada ya nape kuanza kutukana viongozi akiwemo dr.slaa

alaf kaanza kusema eti hao wanaenda kunywa maji watarudi, watu wanaondoka utadhani ni maandano au wameitwa, nimecheka sana! jamaa hawajui kula na vipofu, hao wanaahibika kwa maneno yao watu wanasepaaaa!!
 
Mbona watu wameondoka hapo kwenye mkutano watu kibao???
 
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza. Naona watu ni wawastani wamehudhuria wakiwa wamevaishwa kijani na njano hapa.

Namshangaa Nape na Ngonjera za ajabu eti ana nyomi wakati tunaona kwa macho,anatapika tu mda unaisha hakuna hata la maana,Ni aibu kubwa kuwa na kiongozi kama huyo
 
Akihutubia Singida , muda huu na kusema kuwa UKAWA itakufa kwa sababu zifuatazo;
1. Kuwa Dr Slaa anaruka na Helkopta kwenye mikutano ya UKAWA wakati Lipumba hana , huu ni uongo wa wazi kwani Ndesamburo binafsi ndio aliamua kuhudhuria mikutano ya UKAWA Arusha, Babati, Mwanza na Musoma na huko a kaamua kutumia usafiri wake binafsi , leo kilio MAGAMBANI.

2. Eti posho ziko tofauti baina ya viongozi hao, sasa alitaka katibu mkuu na dereva walipwe kiwango sawa? Huyu anasema kuwa hapo itavuruga UKAWA,


3. Eti UKAWA iliundwa kwa migogoro , na hapo anasema kuwa CUF haidhubutu kuiga baraza kuu kwani watawafukuza kina Lipumba , nakumbuka hata juzi kuwa CUF iliitwa baraza kuu Lao .......eti kuna wabunge wa mahakama, anatia sana aibu, ila hoja moja ni kuwa Mbatia aulizwe alipata wapi fedha za kuitisha mkutano mkuu wa uchaguzi , inawezekana CCM wanataka kutumia kete hiyo kugawa UKAWA ....

Kweli CCM imefulia kisawasawa maana naona hawana meseji mahususi kwa ajili ya mikutano yao ....ni kubwabwaja tu....
 
Ningekuwa mimi ni Kinana nisingehangaika na mtu anaetoka chama kingine kujiunga (iwe ni upya au kurudi) maana mtu alietoka ccm hii na akairudia ikiwa haina ilichobadirika mtu huyo hatakuwa na msaada zaidi ya kuwa msaka tonge!
 
Nijuzeni kwa watu mnaofuatilia mkutano huo, nasikia kuna baadhi ya watu wameondoka kabla ya mkutano haujaisha?? Ni baada ya nnape kuongea utumbo
 
LIVE from STAR TV, nape na kinana wanaendeleza uongo kwenye jimbo la Tundu Lisu singida, nape anatumia muda mwingi kuwaponda viongozi wa UKAWA badala ya kuonyesha njia za kutatua matatizo yanayowakabili wananchi. Kama uko home fungua star tv.
 
Hatuna muda wa kusikiliza porojo,bora nitazame chanel 5 kuliko kuwasikiliza hao waimba taarabu
 
Makapi yanarudi muda mfupi yatakwisha chadema itabakia na creem;ila magamba kufikia mwakani watakua wamemaliza mbuga kwa kuhonga wana cdm wajiunge kwao
 
LIVE from STAR TV, nape na kinana wanaendeleza uongo kwenye jimbo la Tundu Lisu singida, nape anatumia muda mwingi kuwaponda viongozi wa UKAWA badala ya kuonyesha njia za kutatua matatizo yanayowakabili wananchi. Kama uko home fungua star tv.

hahaha! jamaa wameamua kula matapishi ya 'mchakato majimboni'.

mi niko mbali na TV. warekodini.
 
makala badala ya kuwaambia watu wa singida watapataje maji yeye anakazana kuwaeleza maji ya Ngudu
 
Back
Top Bottom