Mkurugenzi wa JATU PLC aomba kukiri Makosa kwa DPP

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,119
Peter-Isare-Gasaya.jpg
Peter Gasaya (33) anayekabiliwa na mashtaka mawili likiwemo la kujipatia Tsh. Bilioni 5.1 kwa njia ya udanganyifu, amemwandika Mkurugenzi wa Mashitaka Tanzania (DPP) barua ya kukiri na kuomba apunguziwe adhabu.

Gasaya alishtakiwa kwa makosa ya kujipatia fedha hizo kutoka katika Saccos ya JATU kwa madai kuwa fedha hizo ataziweka (Kuzipanda) kwenye Kilimo cha Mazao ili kuzalisha faida zaidi, wakati akijua kuwa ni uongo.

Kupitia wakili wake, Nafikile Mwamboma amedai Gasaya amedai kuwa ameandika barua kwa DPP, tangu Aprili 20, 2023 akiomba kukiri mashtaka yake ili aweze kuimaliza kesi hiyo.

============

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya JATU PLC, Peter Gasaya (33) anayekabiliwa na mashtaka mawili likiwemo la kujipatia Sh5.1 bilioni kwa njia ya udanganyifu, amemwandika barua ya kukiri na kuomba apunguziwe adhabu, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP).

Gasaya anadaiwa kujipatia fedha hizo kutoka katika Saccos ya JATU kwa madai kuwa fedha hizo atazipanda kwenye kilimo cha mazao ili kuzalisha faida zaidi, wakati akijua kuwa ni uongo.

Mshtakiwa huyo ameileza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo, Aprili 24, 2023 mbele ya hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo Richard Kabate, wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya kutajwa.

Gasaya, kupitia wakili wake, Nafikile Mwamboma amedai kuwa ameandika barua kwa DPP, tangu Aprili 20, 2023 akiomba kukiri mashtaka yake ili aweze kuimaliza kesi hiyo.

MWANANCHI
 
This is how they always get await, na wataendelea, maana wanachopoteza sio chao, ni cha wahanga.

Wataendelea wakijua ndiyo namna ya kumaliza hii tatizo baada ya kuficha some amount.

No one will protect you but yourself in this world, hata wale waliopo kwenye nafasi na wajibu wa kufanya hivyo.
 
Wamfilisi Kama mafisad wengine walioandika barua za kukiri kosa
 
Jamaa ana miaka 33 lakini ana akili ya kutengeneza zaidi ya 5b huyu ndio mwanaume, haijalishi kazipataje maana wajinga ndio waliwao.

Kwenye hii Dunia ukiwa mnyonge na mpumbavu utakufa maskini na kuishia kulalamika, vyovyote vile atatoka na maisha yanaendelea, majinga yashapigwa...
 
Back
Top Bottom