Mkulo, Maige, Ngeleja kikaangoni TAKUKURU

Mkulo, Maige, Ngeleja kikaangoni TAKUKURU

Tutakaa tunadanganyana tu.

Mnakumbuka kipindi fulani Hosea alitangaza kwenye vyombo vya habari kuwa kulikuwa na kesi 9 nzito zilikuwa zinashughulikiwa na 7 kati ya hizo zilikuwa zinasubiriwa kupelekwa mahakamani kuhusu EPA?? It's more than 2 years ni pelepele tu, walishatufanya wadanganyika kuwa wadanganyika kweli.

Tatizo ni kwamba Mkuu wa nchi si msafi ndiyo maana hawa jamaa wanadunda kwa sababu kuna deals ambazo zinamgusa hata yeye mwenyewe. Hosea, and Manumba Lake Zone route.....so do Maige, and Mzee wa Megawatt. Kuna kulindana kupita maelezo. Kwa msemo wa Mkuu Mwanakijiji "tunazugwa tu"
 
Hivi hawa mawaziri na huwa wana kinga wawapo madarakani?

Inakuwaje nyendo zao hazichunguzwi kipindi wapo madarakani? Sababu hii taarifa zinaonyesha haya mambo hawakuyafanya baada ya kuondoka wizarani bali ni sehemu ya maisha yao walipokuwa pale.

Nashindwa kuelewa hii nchi ipo salama kwa kiwango gani... Hawa PCCB wanapswa wajiulize wanamsaidiaje rais na nchi.

Utata mwingine ni kitendo cha rais kutoa speech inayotafsirika kama vile anawalilia mawaziri wake kwa kusema wanaponzwa na watendaji wao na kuahidi safari hii ku deal na hao watendaji.

Nazidi kujiuliza kama hawa ndiyo rais alikuwa anawalilia au tumpe nafasi atuonyeshe wengine!
 
Wakuu yumkini JK kaamua kumaliza ungwe yake ya mwisho kwa kuwapa zawadi waTZ ya angalau kuwashughulikia "mchwa" wa pesa za umma, wakiwemo hawa mawaziri. Ngoja tusubiri tuone. Tunawategemea wabunge waendelee kuchochea moto kuhakikisha kuwa hatua stahiki zinachuliwa dhidi ya wezi wote wa mali zetu.

Lakini Mkulo na uzee wote huo Vogue 2 na VX ni ulafi uliokithiri.
 
Hazina imekauka kumbe kuna watu tukiwakamua hazina inajaa upya
 
TAKUKURU ipi ya Edward Hosea au mwingine? hakuna kitu hapa serikali imeshakuwa corrupt, kama takukuru imeshindwa kwenye suala la rada, kagoda na mengineyo inataka kuchunguza nini?
 
Takukuru kazi yao kukamata watendaji wa vijiji na mahakimu au polisi
mapapa wakubwa takukuru wanakula nao
hata hawa mawaziri watahonga wanaowachunguza
hakuna kitu hapa ni usanii mtindo mmoja.
 
Sijui ni kwanini kodi za watanzania zinatumiwa kuwalipa TAKUKURU? Mawaziri wote watatu wameanikwa na CAG, TAKUKURU walikuwa wapi kama kweli kazi yao ni kuzuia rushwa? Na hapa TAKUKURU inahusika kwa lipi maana tayari report ya CAG imeshaweka wazi tuhuma?

DPP ndiyo alitakiwa apitie hiyo report na kuona kama kuna kesi au la. Kitendo cha kuwapa TAKUKURU nafasi wakati makosa yalishafanyika na kuwa documented na CAG ni kuendelea kutafuna kodi za walalahoi bila huruma.
 
Watanzania hasa vijana, kwa ufahamu wangu na udadisi juu ya Politics, Power Strugle and Economy naomba nisimame kuhesabiwa miongoni mwa watakao dumu daima upande wa utetezi kwa Ezekiel Maige.

Mzimu mkubwa unaomwandama huyu Mtanzania si nyumba aliyonunua $0.7M cash au njia aliyotumia kupata hiyo pesa bali ujasiri wake kuvuluga syndicate ya waporaji wa maliasili zetu waliodumu kwenye sekta tangu miaka ya mwanzo wa 1960.

Na kubwa la pili ni malengo makubwa na dhamira ya dhati iliyokuwa ikijidhihirisha katika mafanikio yaliyokuwa yameanza kupatikana katika sekta ya Maliasili na Utalii. Maige asingeweza kuyafanya haya bila kuyagusa na kuyabatilisha maslahi makubwa na ya toka enzi ya wakubwa wa nchi hii. Wakubwa hao wengi wako nje ya serikali na hata nje ya nchi. Wananguvu za kubadilisha uongo kuwa ukweli na kinyume chake vilevile. Mwiko aliouvunja Maize ndo Ngeleja alidhani kwa kuuenzi nao watamuenzi kumbe haikuwa hivyo. Ngeleja hajavuluga maslahi ya mkubwa yeyote ila pale wao walipokula yeye kakomba mboga hadi kulamba mwiko.

Rai yangu kwa vijana wasimeze habari kama zinavyowekwa kwenye vyombo vya habari. Na katika yanayoitwa kashfa kuu kupitia kamati za Bunge msichukulie wajumbe kama Malaika na kudhani kila wanalotaarifu ndo ukweli. Hata marefa wana timu zao! Ukitaka kunielewa rejea mswada wa kuondoa kodi kwenye mafuta ya taa uone jinsi Bunge na Kamati zinavyotumika ki-udalali hata katika masuala nyeti.

Nikipata muda nitajitahidi nifumbue mafumbo zaidi labda vijana wenzangu mtanielewa. Hapa mimi si mjumbe wa Maige bali ni muathirika wa ukweli uliopindishwa. Kwa jinsi hii taifa litaendelea kuwakosa watu wenye maamuzi yenye manufaa kwa wananchi. Mbaya zaidi sijazisikia sauti za Wazawa ambao kwa hakika kabisa walipewa vitalu kwa mara ya kwanza toka Tanganyika huru. Simameni jamani, jitokezeni muuweke ukweli huu wazi na Watanzania wasiojua waelewe pumba na mchele.

Ni dhambi kubwa kumuacha Maige kujitetea mwenyewe kwa jambo alilolifanya kwa nia safi kuwanufaisha ninyi Wazawa.
 
Eti, haiwezekani wakatolewa hadharani kwa wananchi wenye hasira kali wakamaliza game? mbona vibaka wa simu na kuku huwa wanakutana na wananchi wenye hasira kali? hawa vipi hawaingii kwene category hii? laiti wezi wa kuku nao na wale wa simu wangekuwa wanachunguzwa na Takokuru haki ingepatikana bila ya ncha ya upanga

Ndo maana Roma alikuambia hii ni Tanzania!
 
Takukuru ni cleaning agent...

kwa kuwa hawa jamaa wote watatu ni vipenzi wa JK kitakachofanyika ni kuwasafisha tu ionakane wamewajibika kwa makosa ya watu wa chini yao. Mbona EPA kahukumiwa Maranda na nduguye Farijala huku Wahindi kesi zao zinapigwa danadana!!?
 
mkuu Invisible siwaamini sawa hawa TAKUKURU CCM! acha tusubiri!

Kwani ni mangapi yashawai kuchunguzwa na yakaishia kuliwa kwa kodi zetu na ukimya uka tawala kwa hii serikali iliyo jaa wezi na walafi wa mali zetu!
 
Last edited by a moderator:
Mimi nilitarajia kusikia wapo lupango na kesi inasubiri kupangiwa jaji kumbe ni kwa hao wachumia tumbo takukuru?
 
na huyu Maige alivyokuwa analalamika kwa Michuzi na hadi kuweka mistari ya biblia kumbe hana lolote anatafuta fadhila

Waovu ndo wanajitahidi kupindisha maneno ya biblia ili waonekane wema
 
Kuwa kiongozi wa watu inabidi uwe muadilifu sana... Wanatumia kodi zenu na rasilimali za watanzania kujinuisha wao na familia zao huku wengine tukifa kwa matatizo chungu nzima...

MUNGU hakumpa uwaziri Mkulo, Megawatt eta'l na akamfanya baba yangu kuwa mkulima kule kijijini kwetu halafu maisha yaishie hapo...lazima na ipo siku Mungu ataweka usawa miongoni mwetu...na siku hiyo yaja....

wapo wengine wanaotuibia japo indirect kwa kusafiri kila kukicha eti wanaenda kupiga picha na 50 cent na sasa beckam usawa utapatikana lini sasa?
 
Eti, haiwezekani wakatolewa hadharani kwa wananchi wenye hasira kali wakamaliza game? mbona vibaka wa simu na kuku huwa wanakutana na wananchi wenye hasira kali? hawa vipi hawaingii kwene category hii? laiti wezi wa kuku nao na wale wa simu wangekuwa wanachunguzwa na Takokuru haki ingepatikana bila ya ncha ya upanga
Hawa jamaa wanaotuibia, kwa kuwa hatimaye itaishia kuwa hakuna ushahidi, hawana kesi ya kujibu; katika pita zao zao mitaani wajihadhari na wananchi wenye hasira kama mbogo.
 
Back
Top Bottom