Entareyehirungu
JF-Expert Member
- Oct 27, 2006
- 488
- 471
BABU CHONDO,...unadhani kampuni zilizo nyimwa vitalu ndani kuna watanzania wangapi wanao tegemewa na familia zao? unatoa kwa mtu ambaye hata hajui wageni anapata lini je ni kuijenga nchi..............,si tuanalilia maslahi ya watanzania wenzetu ambao wanapunguzwa kazi.
Ni sisi wenyewe tuliolalamika kwamba sheria inawapendelea wageni kwenye biashara za vitalu na utalii. Ni sisi tuliotaka Professional Hunters na Guide wawe Watanzania. Maige alichofanya ni kuitikia kilio cha Wazawa.
Kama ajira walikuwa wanapata kwa kuajiliwa ktk makampuni za kigeni basi vilevile wangeendelea kuzipata kwenye Kampuni za Wazawa. Na kubwa zaidi mapato yanabaki nchini kukuza uchumi. Kwa nini Watanzania hatubebeki na hatutaki kuaminana?
Yaani kwa imani yako BABU CHONDO hatuwezi kuajiliana mpaka hao wageni kutoka nje? Suala la makampuni kutojua wageni wanakuja lini: wageni hawaji kutembelea Kampuni bali kuangalia vivutio vya nchi. Na hivi vivutio vinatangazwa na TTB kwa manufaa ya sekta nzima na si kampuni fulani.
Last edited by a moderator: