MKOA WA PWANI UGAWANYWE

MKOA WA PWANI UGAWANYWE

Nicolas J Clinton Gabone

JF-Expert Member
Joined
Mar 13, 2014
Posts
892
Reaction score
536
Mkoa wa Pwani ugawanywe

Kibaha, Bagamoyo, Kisarawe na Mkuranga ziunde jiji la Dar Es Salaam.

Rufiji, Kilwa, Mafia na Kibiti ziunde Mkoa wa Pwani/Rufiji/Kilwa.

Mikoa miwili ya Tanzania bara yaani Morogoro na Tabora iwe mikoa ya Viwanda vikubwa/vizito zaidi na technologia ya majeshi yetu na taasisi nyingine kama za matibabu.

Hapa naamanisha Viwanda vizito vyote visiendelee kujengwa Mkoa wa Pwani tena bali vielikezwe Morogoro na Tabora na Viwanda vyepesi viendelee kujengwa Mkuranga kama eneo la rasmi la Viwanda, huku Bagamoyo, Kibaha na Kisarawe yawe makaazi tu lakini serikali ipime maeneo hayo yote ili kuepuka ujenzi holela wa makaazi, hii inalenga upanuzi wa Jiji la Dar Es Salaam.

Serikali ichore ramani mpya ya Dar Es Salaam ikiunganisha Halmashauri hizo katika miundombinu ya Barabara za kisasa, Reli, umeme, Maji, pia serikali itenge eneo kubwa zaidi kule Kisarawe kwa ajili ya ujenzi wa uwanja mwingine wa ndege, yawezekana miaka 50 mpaka 70 ijayo kutoka leo uwanja wa ndege wa Mwalimu Julias Nyerere utazidiwa kutokana na maendeleo makubwa na upanuzi wa miundombinu ya usafiri wa Anga.

Viwanda vyote ambavyo vimejengwa tayari Mkoa wa Pwani vibakie hivyo hivyo na/au vinaweza kuhamishwa hasa vile vizito na kuelekezwa Morogoro na Tabora.

Morogoro iwe sehemu ya kilimo cha kimkakati na Viwanda vikubwa/vizito ikiwemo na taasisi za utafiti wa kisayansi za majeshi yetu na technologi nyingine zielekezwe Morogoro na Tabora.
 
Nilifika sehemu kilwa inapakana na Morogoro ... Kibata huko nadhani .. ile wilaya kubwa saaana
 
Malengo mazuri.

Lakini kwa Tanzania ya sasa hakuna wa kuyatekeleza
 
Actually ingependezA mkoa wa Kilwa uwe na Rufiji , mafia, Kibiti
 
Tabora kuna nini cha kuvutia viwanda vikubwa? Why isiwe mikoa yenye madini muhimu kama chuma, nickel na makaa ya mawe, maana Heavy Industries zinatumia zaidi chuma
 
Makao makuu yawe kilwa kivinje ikishindikana kabisa basi yawe kipatimo huko
Kivinje ni mji kihistoria,,, naonga mkono hoja kuliko eti mkoa wa rufiji.. kilwa imebeba historia kubwa sana ... Mimi si mwenyeji wa kusini.. maneno ya mchengrwa Rufiji iwe mkoa hayana maana Rufiji iwe wilaya ndani ya mkoa wa kilwa kutokana na historia iliyobebwa na kilwa
 
Tabora kuna nini cha kuvutia viwanda vikubwa? Why isiwe mikoa yenye madini muhimu kama chuma, nickel na makaa ya mawe, maana Heavy Industries zinatumia zaidi chuma
Unajua mjerumani chupuchupu makao makuu ya nchi ayapeleke Tabora
 
Mkoa wa Pwani ugawanywe

Kibaha, Bagamoyo, Kisarawe na Mkuranga ziunde jiji la Dar Es Salaam.

Rufiji, Kilwa, Mafia na Kibiti ziunde Mkoa wa Pwani/Rufiji/Kilwa.

Mikoa miwili ya Tanzania bara yaani Morogoro na Tabora iwe mikoa ya Viwanda vikubwa/vizito zaidi na technologia ya majeshi yetu na taasisi nyingine kama za matibabu.

Hapa naamanisha Viwanda vizito vyote visiendelee kujengwa Mkoa wa Pwani tena bali vielikezwe Morogoro na Tabora na Viwanda vyepesi viendelee kujengwa Mkuranga kama eneo la rasmi la Viwanda, huku Bagamoyo, Kibaha na Kisarawe yawe makaazi tu lakini serikali ipime maeneo hayo yote ili kuepuka ujenzi holela wa makaazi, hii inalenga upanuzi wa Jiji la Dar Es Salaam.

Serikali ichore ramani mpya ya Dar Es Salaam ikiunganisha Halmashauri hizo katika miundombinu ya Barabara za kisasa, Reli, umeme, Maji, pia serikali itenge eneo kubwa zaidi kule Kisarawe kwa ajili ya ujenzi wa uwanja mwingine wa ndege, yawezekana miaka 50 mpaka 70 ijayo kutoka leo uwanja wa ndege wa Mwalimu Julias Nyerere utazidiwa kutokana na maendeleo makubwa na upanuzi wa miundombinu ya usafiri wa Anga.

Viwanda vyote ambavyo vimejengwa tayari Mkoa wa Pwani vibakie hivyo hivyo na/au vinaweza kuhamishwa hasa vile vizito na kuelekezwa Morogoro na Tabora.

Morogoro iwe sehemu ya kilimo cha kimkakati na Viwanda vikubwa/vizito ikiwemo na taasisi za utafiti wa kisayansi za majeshi yetu na technologi nyingine zielekezwe Morogoro na Tabora.
Una hoja lakn unaoosema viwanda visijengwe pwani unakosea.
Pwani inamiliki bahari na Bandari na ni karibu na Bandari kuu ya daslam.
Hakuna mchina anaweza kujenga kiwansa Tabora halafu asafirishe malighafi kutoka dar km800+
 
Kwa Sasa pwan nadhan ndo mkoa unaoongoza kwa viwanda hasa vya wachina.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom