Mkoa unaotoka hiki chakula kinapatikana? Mnakiitaje?

Mkoa unaotoka hiki chakula kinapatikana? Mnakiitaje?

Mwanamwana

Platinum Member
Joined
Aug 1, 2011
Posts
9,604
Reaction score
22,714
Juzi kati nilikuwa nyumbani Missenyi, Kagera nikaenda shambani na kuibuka na hiki kiazi. Kwa Dar sijawahi bahatika kuviona, ila kwetu vipo sana na vilikuwa chakula changu pendwa. Ilibidi nikisafirishe sasa hivi najimegemea kipande kidogo kidogo nakula kwa samaki kibambala.

Kwa nyumbani tunaika e'kira.

IMG-20250926-WA0002.jpg

20251001_204658.jpg
 
Kiazi kitamu, kuna wengine wanaita makaba
 
Kwa nje waweza dhani ni mzizi
Kumbe ni kiazi?
Mi nafahamu viazi vitamu
 
Juzi kati nilikuwa nyumbani Missenyi, Kagera nikaenda shambani na kuibuka na hiki kiazi. Kwa Dar sijawahi bahatika kuviona, ila kwetu vipo sana na vilikuwa chakula changu pendwa. Ilibidi nikisafirishe sasa hivi najimegemea kipande kidogo kidogo nakula kwa samaki kibambala.

Kwa nyumbani tunaika e'kira.

View attachment 3482032
View attachment 3482031
Lushoto.. Missed it😋
 
Juzi kati nilikuwa nyumbani Missenyi, Kagera nikaenda shambani na kuibuka na hiki kiazi. Kwa Dar sijawahi bahatika kuviona, ila kwetu vipo sana na vilikuwa chakula changu pendwa. Ilibidi nikisafirishe sasa hivi najimegemea kipande kidogo kidogo nakula kwa samaki kibambala.

Kwa nyumbani tunaika e'kira.

View attachment 3482032
View attachment 3482031
Homeboy msimu mzuri wa kula hiki kiazi ni kuanzia mwezi July kwenye kiangazi hadi kabla ya kupanda mazao shambani. Vinastawi kwenye udongo wa kichanga kiasi, na mbolea ya mboji.

Kwa Joanah anayehisi ni chakula cha kubahatisha, nakuhakikishia sio chakula cha kivivu kinahitaji ukifanyie kazi na kusubiri msimu mmoja kwa mwaka. Sio magimbi haya.

Harufu yake kwa mbali ni kama maziwa fresh na maji ya mchele mzuri, ladha ni kama neutral. Inategemea na ukomavu na msimu wa kuvuna kama ni jua Kali au mvua au wakati kina majani yamekauka au yananza kuchipua mapya.
 
Homeboy msimu mzuri wa kula hiki kiazi ni kuanzia mwezi July kwenye kiangazi hadi kabla ya kupanda mazao shambani. Vinastawi kwenye udongo wa kichanga kiasi, na mbolea ya mboji.

Kwa Joanah anayehisi ni chakula cha kibahatisha, nakuhakikishia sio chakula cha kivivu kinahitaji ukifanyie kazi na kusubiri msimu mmoja kwa mwaka. Sio magimbi haya.

Harufu yake kwa mbali ni kama maziwa fresh na maji ya mchele mzuri, ladha ni kama neutral. Inategemea na ukomavu na msimu wa kuvuna kama ni jua Kali au mvua au wakati kina majani yamekauka au yananza kuchipua mapya.

Nilisema sijawahi kukijua hiko chakula,sio cha kubahatisha

Lakini asante kwa maelezo mazuri
 
Vikwa.....

Ni vizuri kwa kuchomwa..... unaweza kula na parachichi au chai whatever.....

Ama unavimenya ukataka vipande vya wastan, chemsha vikiiva.. unaweza kula na roast ya nyama au samaki na vimboga vikiwepo inakuwa mukidee.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom