Dullybrown13
New Member
- Jun 25, 2013
- 3
- 1
I prefer Mwanza
Ahsante sana, nnapajuwa vizuri sana, mume wangu yuko kwenye mradi fulani huko na mimi huwa nakuja mara kwa mara. Kwenu kuzuri na nnadhani ntahamia huko panapo uhai na majaaliwa, nimependa sana nipate nyumba karibu ya Kindai.
Aahahahahahhh, ule upepo wa ziwa kindai utauvumilia mamii? Na hii baridi ya kiangazi utaiweza, mie nilienda mwezi wa sita baridi ilinishinda kama sio kwetu lol!
We afadhali umejitahidi, kule Mwanza kuna bahari ya victoria na Morogoro kuna bahari ya mindu. Mambo bahari bwana, mito mafuriko tuFor me naipenda Mwanza then Morogoro aisee
We afadhali umejitahidi, kule Mwanza kuna bahari ya victoria na Morogoro kuna bahari ya mindu. Mambo bahari bwana, mito mafuriko tu
Wilaya za Handeni na Lushoto ziko mkoa gani? Au unajua Tanga mjinj tu?
Jamani mimi natafuta mkoa mzuri wa kuishi ambako maisha ni ahueni! Nijuzeni waungwani!
Kwani mikoa ipo Bara tuu?wadau Znz nako hakuna mikoa ?
duh!!!! unataka mwenzio yamkute ya wale walimu waliomba kazi iishe kwa kulazwa nje kila sikuKigoma
Shekhe zipo mkoa huo huo, nimezaliwa Tanga (M) nyumba ya pili kutoka klabu ya Coastal Union, wilaya zote hizo ndizo zilikuwa sehemu ya maisha yetu ya kila siku katika kutafuta maisha kabla ya kuhamishia makazi Jiji la Makamba.Wilaya za Handeni na Lushoto ziko mkoa gani? Au unajua Tanga mjinj tu?
Pale ni pazuri sana tena sena, sijaona mji katika Tanzania ambao watu wema zaidi ya Singida, wanapenda wageni, wacheshi, mji mzuri, pasafi na siku hizi lami barabara zote za muhimu mpaka za sokoni.
Unajuwa Singida kwa sasa kunatoa Strawberries nyingi kuliko sehemu yoyote Tanzania? nilishangaa sana nilizikuta sokoni mwaka jana zimejaa, nikauliza zinatoka wapi hizi, nikaambiwa zinalimwa pale-pale kuna sehemu inaitwa Mkiwa, karibu ya Manyoni.
Halaf nikalishwa matunda aina mbili tatu ambayo sijawahi kuyaona kwingine duniani, yanaitwa siunga na mingine sasati na mingine yanaitwa lade.
Aaah umenikumbusha a home away from home. Singida sikujihisi kama ni mgeni kwenda kwangu kote.