Mkemia Mkuu, Ernest Mashimba is NO MORE

It was a privilage to work with you and knowing you in person. Tutayaendeleza mazuri yote uliyoyasimamia. R.I.P
 
Mkuu, kwani alikuwa anaifanyia kazi ishu yoyote tata au inayowahusu vigogo?..kwanini upate shaka?

Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi!

Mkuu kuna matukio tata mengi yametokea hivi karibuni, na ukichukulia afya ya mkulu ipo majaribuni. naamini mkemia anaweza akawa mtu muhimu ktk kipindi cha lala salama.

Hivi ile ripoti ya wananchi walidhurika na zile kemikali kutoka machimbo ya dhahabu ya barik yalipaswa kuwa na second testing au?

Doubtful, lakini ametutoka. nadhani postmortem ya kifo chake ifanyike kwa undani zaidi
 
Habari zilizopatikana hivi punde ni kuwa Mkemia Ernest Mashimba, PhD amefariki ghafla huko Tanga alikokuwa amealikwa kama mgeni rasmi kwenye mahafari ya darasa la saba.

Mauti yamemkuta hotelini alikokuwa amefikia baada ya kuanguka ghafla, habari ni kuwa kifo chake kimegundulika baada ya dereva wake kumpitia leo asubuhi kwa ajili ya kuanza safari ya kurejea DAR.

Bwana ametoa, Bwana ametwaa . . . . . . .

RIP MASHIMBA,kafia Lushoto Executive Hotel alikokuwa ameenda Kifungiro kwenye mahafali ya binti yake.Mungu alitoa na Mungu ametwaa Jina lake Lihimidiwe.
 
aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kusishi si nyingi, ni miaka 70 ikizidi sana 80.
Bwana alitoa naye ametwaa, jina la Bwana libarikiwe.
 
RIP Ernest Mashimba.

Wafuatiliaji wa mambo, mimi nakumbuka kama Chief Chemist kabla yake au yule wa nyuma zaidi naye alikufa ghafla, na alikuwa anafuatilia issue ya mchele mbovu uliokuwa bandarini? Nina shaka sana na hivi vifo!
 
Mkemia Mkuu wa Serikali akutwa amekufa hotelini Send to a friend Monday, 20 September 2010 08:43 0diggsdigg

Burhani Yakub, Lushoto

MKEMIA Mkuu wa Serikali, Ernest Mashimba amekutwa amekufa katika chumba
cha Hoteli ya Executive Lodge iliyo nje kidogo ya mji wa Lushoto mkoani hapa.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana mjini hapa ambazo pia zimethibitishwa na mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Sophia Mjema, kifo hicho kilitokea usiku wa kuamkia Jumamosi kwenye hoteli hiyo ya kitalii ambayo alifikia katika safari yake mjini hapa ya kuhudhuria mahafali ya Shule ya Sekondari ya Kifungilo.

Kwenye mahafali hayo, Mashimba alikuwa akitarajiwa kuwa msoma risala mkuu kwa niaba ya wazazi.

“Hatujajua ni muda gani hasa alikufa lakini inahofiwa ni usiku baada ya
kuingia chumbani kwake kulala. Hivi ninavyozungumza uchunguzi unafanywa
na madaktari pamoja na polisi ili kujua chanzo,” alisema Mjema.

Mkuu huyo wa wilaya alisema taarifa rasmi juu ya tukio hilo itatolewa
baada ya kufanyika kwa uchunguzi, hasa ikizingatiwa kuwa kuna utata katika tukio zima.
Alisema kifo cha mkemia huyo kilibainika Jumamosi asubuhi baada

ya wahudumu wa hoteli hiyo kuingiwa na shaka kutokana na mkemia huyo kutumia muda mrefu chumbani . Wahudumu waliwasiliana na uongozi ambao uliamua
kufungua mlango wa chumba alicholala na kumkuta kitandani akiwa tayari
ameshakufa.

“Polisi walipokwenda walikuta amekufa muda mrefu sasa hatujajua ni saa
ngapi yalimkuta mauti na ni sababu gani,” alisema Mjema.

Uongozi wa shule hiyo ya Kifungilo uliifahamisha Mwananchi kuwa mgeni
rasmi katika mahafali hayo alikuwa ni mkuu wa Mkoa wa Tanga, Meja
Jenerali Said Kalembo wakayti Mashimba alipangwa kusoma risala maalumu kwa
niaba ya wazazi wenye watoto shuleni hapo.

Kwa mujibu wa maelezo ya uongozi huo ni kwamba sherehe za mahafali
zilianza kama kawaida na ilipofika zamu ya kusomwa risala ya wazazi,
iliwalazimu kumteua mzazi mwingine kuchukua nafasi yake.

Watu waliokuwepo kwenye mahafali hayo wameeleza kuwa wakati wa kuimba
nyimbo walitangaziwa juu ya kifo, tangazo ambalo lilisababisha wahitimu
kuishiwa nguvu kwa kuwa Mashimba ni baba wa mwanafunzi mwenzao.
 
Mkuu kuna matukio tata mengi yametokea hivi karibuni, na ukichukulia afya ya mkulu ipo majaribuni. naamini mkemia anaweza akawa mtu muhimu ktk kipindi cha lala salama.

Hivi ile ripoti ya wananchi walidhurika na zile kemikali kutoka machimbo ya dhahabu ya barik yalipaswa kuwa na second testing au?

Doubtful, lakini ametutoka. nadhani postmortem ya kifo chake ifanyike kwa undani zaidi

Ndugu yangu wewe ni hatari kwa kuunganisha nukta. Kwani ripoti yenyewe ilishatoka? Kuna jamaa alishanambia kwamba kuna kazi nyingine ni hatari kama landmine,...ikiwemo hii ya Mkemia Mkuu na AG. Unakuwa na profession yako lakini unafanya kile unachoagizwa kama kitoto kidogo!

RIP Ernest Mashimba.

Wafuatiliaji wa mambo, mimi nakumbuka kama Chief Chemist kabla yake au yule wa nyuma zaidi naye alikufa ghafla, na alikuwa anafuatilia issue ya mchele mbovu uliokuwa bandarini? Nina shaka sana na hivi vifo!

Huyo waliamua kumpoteza na ushahidi wake kipindi kile cha Ruksa!
 
Taarifa za watz siku zote tata.....mara kaanguka bafuni!!!????
mara kakutwa amelala kitandani
Mara alihudhuria mahafali na akachanga fedha na kufanya harambee...mara hakufika hata kwenye mahafali hayo ha hah ha ha a
kweli wanaoripoti wanajichanga kiasi hiki??/ kwanini????
anyway nami nawapa pole wafiwa
Jamani marehemu hakwenda na mkewe kwenye hayo mahafali? nimesikitika kuona kuwa amekufa peke yake.....anyway hayanihusu
mix with yours
 
Hakuna ajabu mtu kufariki dunia maana hii ni tabia mojawapo ya viumbe hai wote. Issue ni chanzo au kisababishi cha kifo chenyewe au mazingira ya tukio la kifo. Wanahabari jitahidini ku - reconcile hizi habari maana huku kutofautiana kwa mazingira ya hiki kifo cha Dr. Mashimba kunatufanya tuwe na wasiwasi.
 
Habari zozote ambazo zinazotolewa kuhusu jambo moja kisha zikaonekana kutofautiana ni dhahiri kuna ukweli unaofichwa.

Mauaji yanaweza kuitwa ujambazi na poisoning ikaitwa shinikizo la damu. Kwani tuliwitness huo uchunguzi ukifanyika? Mwenyezi mungu tunusuru viumbe wako waadilifu (endangered species)
 
rip MASHIMBA, tULIKUPENDA ILA bWANA mUUMBA WAKO KAKUPENDA ZAIDI.
wENGINE TU NJIA KUJA KWA MUUMBA RABANA
 
Back
Top Bottom