Mke wangu wa ndoa ame-hack simu yangu

Mke wangu wa ndoa ame-hack simu yangu

Sina hakika saana kama huyo ni mke wako wa ndoa na si rahisi kumshitaki mahakaman na kesi ikawa simple chakufanya mweleze mkeo kwanin ulifanya hvo na jitahidi kumshirikisha mkeo kwa kila kitu
 
Mwili mmoja ni huko Ughaibuni sio Bongo! Hapa tu mnaonekana jinsi mitazamo yenu ilivyo selfish!

Uselfish mnauanza nyie wanaume,wewe tayari uko kwenye ndoa,unafanyaje baadhi ya miamala bila kumshirikisha mkeo? Na hiyo ndio sababu iliyomfanya akabe mawasiliano yako baada ya kuhisi hali sio shwari. Mkeo naye ana nafasi katika maamuzi yako,vinginevyo umetawaliwa na mfumo dume.
 
mi cdhan kama mpes no taarif ya cr kwa wanandoa.Mke umeish naye miaka 8 bado unaish kwa kijiiba kwamba humwamin au?
 
Kama kweli hana utalaanika huo wa mawasiliano basi jua ana reliable Na credible source kutoka kwa provider wa mtandao wa simu unayotumia! Sasa anzia hapo kuitafuta hiyo source! Jifunze umafia na wewe usiregee!
 
Kama kweli hana utalaanika huo wa mawasiliano basi jua ana reliable Na credible source kutoka kwa provider wa mtandao wa simu unayotumia! Sasa anzia hapo kuitafuta hiyo source! Jifunze umafia na wewe usiregee!
Sorry isomeke utalaam
 
Sina hakika saana kama huyo ni mke wako wa ndoa na si rahisi kumshitaki mahakaman na kesi ikawa simple chakufanya mweleze mkeo kwanin ulifanya hvo na jitahidi kumshirikisha mkeo kwa kila kitu
Mimi ndio ninayemtuhumu kwa kuingilia mawasiliano yangu bila idhini yangu, yeye yupo kwenye upande wa kuomba msamaha kuwa nisilifikishe hili suala kwenye vyombo vya sheria, kati yangu na yeye ni nani anatakiwa amueleze mwenzie sababu ya kufanya kilichofanyika?!!
 
Aisee we jamaa unajua maana ya ndoa, wewe umeshakamatika kuwa mpole tu, ana haki ya kujua mambo yote. Kwanini unapokuwa na wasiwasi wa mawasiliano unapoenda kuchukua kibali polisi kwa ajili ya kufuatilia mawasiliano si huwa wanaomba cheti cha ndoa??, kuwa mpole weka mambo sawa
Kwa hiyo maana ya ndoa ni kufanyiana ujasusi? Nijuavyo mimi ndoa ni UPENDO.
 
Habari wanajamvi,

Katika hali isiyo ya kawaida nimegundua kuwa mke wangu wa ndoa ame-hack simu yangu na kuweza ku-access mawasiliano yangu yote hasa ya sms tokea mwezi wa 10 mwaka jana 2015 na kuzihifadhi kwenye simu yake.

Sina uhakika kama aliweza kupata mawasiliano mengine tofauti na sms.

Ninasema ku-hack kwa sababu tunaishi mikoa tofauti na hivyo hakuwa na namna yoyote ya ku-access simu yangu physically toka wakati huo, pia simu yangu ambayo ni smart phone ina security (password) in case angetumia mtu aliye karibu yangu.

Nimegundua hii hacking baada ya kuwa na hali ya kutoelewana kati yetu kwa muda sasa ambapo pamoja na mambo mengine niligundua kuna taarifa zangu za siri anazozifahamu ndipo nilipoanza uchunguzi na kugundua kuwa ana hizo sms.

Miongoni mwa sms anazoshikia bango ni zile zinazohusiana na miamala ya Mpesa ambapo nimewatumia pesa ndg, jamaa na marafiki ambao sikuona umuhimu wa kumtaaifu hivyo akazijengea hoja mbali mbali ikiwemo ya uhusiano wa kimapenzi wakati si kweli!

Nimejaribu kumbana aseme amewezaje ku-access "private communications" zangu ila amegoma kabisa kuweka wazi.

Cha kushangaza zaidi ni kuwa hana utaalam wowote wa masuala ya mawasiliano!

Kwa kuzingatia usumbufu uliojitokeza kwa kuingilia mawasiliano yangu ya siri hasa kupitia mis-perception ya taarifa alizokutana nazo, nimepata wazo la kumshtaki kwa mujibu wa ile SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO, 2015 ila nikaona kabla sijafanya hivyo nililete suala hili hapa ili nipate michango yenu ya mawazo hasa juu ya nini cha kufanya.

Suala hili limenichanganya sana hasa ukizingatia kuwa tumekuwa kwenye ndoa takribani miaka 8 sasa na tuna watoto 2.

Naombeni michango yenu ya mawazo.

Ahsante!
CHAPA MAKOFI, MWENYEWE ATAKUELEZA NJIA ALIYOTUMIA KUPATA HIZO TAARIFA ZAKO NA PIA MTU ALIYEMFANYIA HIYO KAZI. kUWA MWANAUME ACHA UBWEGE.
 
Je,una wazazi? Na mkeo ana wazazi? Kama kwako hilo limekiwa tatizo ni kwa nini usiwafikishie wazazi wenu ili m-malize tofauti zenu? Unachokitafuta wewe ni kusuluhisha au ni kuachana? Vinginevyo tuambie kuwa umemchoka huyo dada. Kama kweli unatafuta ushauri kwa ajili ya kutatua hilo suala basi washirikisheni wazazi wenu,au wajomba na mashangazi,si mahakamani. Watu mmeoana kwa ndoa,mnalala watupu kitandani,halafu mwisho wa siku mna simamishana mahakamani kama maadui? Haileti picha nzuri bhanaa.


Mimi ndio ninayemtuhumu kwa kuingilia mawasiliano yangu bila idhini yangu, yeye yupo kwenye upande wa kuomba msamaha kuwa nisilifikishe hili suala kwenye vyombo vya sheria, kati yangu na yeye ni nani anatakiwa amueleze mwenzie sababu ya kufanya kilichofanyika?!!
 
Hahahaaa. ... mkisikia wake kuchepuka vinawauma kwelikweli,
Ila wanaume kuchepuka ni urijali.
Hahahaaa. .... ukigawa game nje lazima na yeye agawe game nje tuuu sabab hakuna namna nyingine
Hujatulia!
 
Kwa hiyo maana ya ndoa ni kufanyiana ujasusi? Nijuavyo mimi ndoa ni UPENDO.

Ndoa sio rahisi kama unavyotafsiri wewe, Upendo? Yaani kila siku upendo tu!! Ingekuwa hivyo watu wasingetalikiana,ndoa ni pamoja na hayo unayoyapitia sasa,ndio maana kila anayeshauri kuhusu ndoa haachi kutaja uvumilivu, Ninahisi suala la wewe kuishi mikoa tofauti na mkeo ndilo linaloigharimu ndoa yako. Ukame hapa lazima unahusika.
 
Ndoa sio rahisi kama unavyotafsiri wewe, Upendo? Yaani kila siku upendo tu!! Ingekuwa hivyo watu wasingetalikiana,ndoa ni pamoja na hayo unayoyapitia sasa,ndio maana kila anayeshauri kuhusu ndoa haachi kutaja uvumilivu, Ninahisi suala la wewe kuishi mikoa tofauti na mkeo ndilo linaloigharimu ndoa yako. Ukame hapa lazima unahusika.
Hii comment imekomaa!
 
Hakuna povu bali ukweli tu.

Watu wasio waaminifu kwa wenza wao hupenda sana kulialia wakibambwa.

Kama jamaa hana baya afanyalo basi hana sababu ya kupatwa na kiwewe.
Uaminifu kwenye ndoa Afrika ni kitendawili usifikri wote tunabeba boksi.
 
Mwanamke haruhusiwi kuchepuka, ulisikia wapi kwenye historia ya Dunia hii mwanamke mmoja akaolewa na zaidi ya mwanaume mmoja? Ila sisi Masheikh mpaka sasa tunaoa hadi 4 teh teh teh!
Na yy huko nje kapata sheikh anayeruhusiwa kuoa wake wa 4. Hebu kaa na mkeo muyamalize. Jishushe uache michepuko. Ndoa sio mashindano. Fikiria na hao watoto
 
Hata kama umeoa naamini kuna mambo ambayo ni private na mojawapo ya mambo hayo ni simu za mikononi.Jaribu kubadili simu na chip pia
 
Watu mnaingiaga kwenye ndoa huku mkiwa hata hamjielewi.

Inavyoonekana mnaingiaga tu ili kukidhi matakwa potofu ya jamii.

Sasa wewe unalalamika eti mkeo anazifahamu taarifa zako za siri.

Siri gani hizo ilhali mko kwenye ndoa?

Au mliwekeana makubaliano ya mipaka kwenye ndoa yenu kabla hamjaifunga?
Hili nalo neno!! Atueleze vizuri
 
Naona makosa kadhaa kwa wanandoa hawa;
1. Ukimsaliti mwenzako kwa kutoka nje ya ndoa (nae akafahamu kuwa umemsaliti), usitegemee quick fix coz you've torn your partner's heart. Hilo linasababisha yeye kukosa imani na wewe, hivyo kupelekea kuangalia mapito yako (ikiwa ni pamoja na mawasiliano ya simu).
Huenda mke hakuwa na nia ya kufuatilia miamala yako, lakini you gave her a reason not to trust you. You need to fix that, na inachukua mda. Ukimsaliti mtu leo nae akasema amekusamehe, usifikiri kila kitu kitaishia hapo, atakumbuka...atakulaani...atafanya moyo mgumu..nk.
2. Kitendo cha wanandoa kuishi mbali either coz of education or work, kinaathiri na kudhoofisha sana ndoa coz hata mwenyezi Mungu alipowaumba Adam & Eve aliwaambia waambatane, kuwa pamoja au kuishi pamoja kunapunuza mengi sana,.. nadhani unaelewa hilo, hivyo yeye kufuatilia mawasiliano yako, kunaweza kuletwa na umbali mlio nao...she's protecting what belongs to her, usimlaumu sana.
3. Mke nae ana makosa yake, hakupaswa kufanya alichofanya hata kama ni wivu au kukubana ili usitume pesa ovyo kwa watu baki. Lakini unaposema (privacy yako), ukiwa na ndoa neno ''privacy'' halina nafasi kabisa. Unatakiwa kumshirikisha mke kwa kila unalotaka kufanya.

Mwisho, huna sababu za kumshtaki mwandani wako, kaa nae chini myaweke vizuri...ukimshitaki ujuwe unajishitaki...unless uniambie umeichoka ndoa yako.
 
Back
Top Bottom