Kosa limeshatokea,mkae myamalize ila wakati mwingine ni vizuri kumshirikisha mkeo atajiona ana nafasi katika maamuzi yenuNingependa zaidi kupata michango toka kwa wazoefu wa ndoa kuliko wale wenye ndoa za "kufikirika" vichwani.
Kosa limeshatokea,mkae myamalize ila wakati mwingine ni vizuri kumshirikisha mkeo atajiona ana nafasi katika maamuzi yenuNingependa zaidi kupata michango toka kwa wazoefu wa ndoa kuliko wale wenye ndoa za "kufikirika" vichwani.
Wewe unadhani ikizama inakula kwangu au kwa huyo mwenzio?
Mwili mmoja ni huko Ughaibuni sio Bongo! Hapa tu mnaonekana jinsi mitazamo yenu ilivyo selfish!
Sorry isomeke utalaamKama kweli hana utalaanika huo wa mawasiliano basi jua ana reliable Na credible source kutoka kwa provider wa mtandao wa simu unayotumia! Sasa anzia hapo kuitafuta hiyo source! Jifunze umafia na wewe usiregee!
Mimi ndio ninayemtuhumu kwa kuingilia mawasiliano yangu bila idhini yangu, yeye yupo kwenye upande wa kuomba msamaha kuwa nisilifikishe hili suala kwenye vyombo vya sheria, kati yangu na yeye ni nani anatakiwa amueleze mwenzie sababu ya kufanya kilichofanyika?!!Sina hakika saana kama huyo ni mke wako wa ndoa na si rahisi kumshitaki mahakaman na kesi ikawa simple chakufanya mweleze mkeo kwanin ulifanya hvo na jitahidi kumshirikisha mkeo kwa kila kitu
Kwa hiyo maana ya ndoa ni kufanyiana ujasusi? Nijuavyo mimi ndoa ni UPENDO.Aisee we jamaa unajua maana ya ndoa, wewe umeshakamatika kuwa mpole tu, ana haki ya kujua mambo yote. Kwanini unapokuwa na wasiwasi wa mawasiliano unapoenda kuchukua kibali polisi kwa ajili ya kufuatilia mawasiliano si huwa wanaomba cheti cha ndoa??, kuwa mpole weka mambo sawa
CHAPA MAKOFI, MWENYEWE ATAKUELEZA NJIA ALIYOTUMIA KUPATA HIZO TAARIFA ZAKO NA PIA MTU ALIYEMFANYIA HIYO KAZI. kUWA MWANAUME ACHA UBWEGE.Habari wanajamvi,
Katika hali isiyo ya kawaida nimegundua kuwa mke wangu wa ndoa ame-hack simu yangu na kuweza ku-access mawasiliano yangu yote hasa ya sms tokea mwezi wa 10 mwaka jana 2015 na kuzihifadhi kwenye simu yake.
Sina uhakika kama aliweza kupata mawasiliano mengine tofauti na sms.
Ninasema ku-hack kwa sababu tunaishi mikoa tofauti na hivyo hakuwa na namna yoyote ya ku-access simu yangu physically toka wakati huo, pia simu yangu ambayo ni smart phone ina security (password) in case angetumia mtu aliye karibu yangu.
Nimegundua hii hacking baada ya kuwa na hali ya kutoelewana kati yetu kwa muda sasa ambapo pamoja na mambo mengine niligundua kuna taarifa zangu za siri anazozifahamu ndipo nilipoanza uchunguzi na kugundua kuwa ana hizo sms.
Miongoni mwa sms anazoshikia bango ni zile zinazohusiana na miamala ya Mpesa ambapo nimewatumia pesa ndg, jamaa na marafiki ambao sikuona umuhimu wa kumtaaifu hivyo akazijengea hoja mbali mbali ikiwemo ya uhusiano wa kimapenzi wakati si kweli!
Nimejaribu kumbana aseme amewezaje ku-access "private communications" zangu ila amegoma kabisa kuweka wazi.
Cha kushangaza zaidi ni kuwa hana utaalam wowote wa masuala ya mawasiliano!
Kwa kuzingatia usumbufu uliojitokeza kwa kuingilia mawasiliano yangu ya siri hasa kupitia mis-perception ya taarifa alizokutana nazo, nimepata wazo la kumshtaki kwa mujibu wa ile SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO, 2015 ila nikaona kabla sijafanya hivyo nililete suala hili hapa ili nipate michango yenu ya mawazo hasa juu ya nini cha kufanya.
Suala hili limenichanganya sana hasa ukizingatia kuwa tumekuwa kwenye ndoa takribani miaka 8 sasa na tuna watoto 2.
Naombeni michango yenu ya mawazo.
Ahsante!
Mimi ndio ninayemtuhumu kwa kuingilia mawasiliano yangu bila idhini yangu, yeye yupo kwenye upande wa kuomba msamaha kuwa nisilifikishe hili suala kwenye vyombo vya sheria, kati yangu na yeye ni nani anatakiwa amueleze mwenzie sababu ya kufanya kilichofanyika?!!
Hujatulia!Hahahaaa. ... mkisikia wake kuchepuka vinawauma kwelikweli,
Ila wanaume kuchepuka ni urijali.
Hahahaaa. .... ukigawa game nje lazima na yeye agawe game nje tuuu sabab hakuna namna nyingine
Kwa hiyo maana ya ndoa ni kufanyiana ujasusi? Nijuavyo mimi ndoa ni UPENDO.
Hii comment imekomaa!Ndoa sio rahisi kama unavyotafsiri wewe, Upendo? Yaani kila siku upendo tu!! Ingekuwa hivyo watu wasingetalikiana,ndoa ni pamoja na hayo unayoyapitia sasa,ndio maana kila anayeshauri kuhusu ndoa haachi kutaja uvumilivu, Ninahisi suala la wewe kuishi mikoa tofauti na mkeo ndilo linaloigharimu ndoa yako. Ukame hapa lazima unahusika.
Uaminifu kwenye ndoa Afrika ni kitendawili usifikri wote tunabeba boksi.Hakuna povu bali ukweli tu.
Watu wasio waaminifu kwa wenza wao hupenda sana kulialia wakibambwa.
Kama jamaa hana baya afanyalo basi hana sababu ya kupatwa na kiwewe.
Na yy huko nje kapata sheikh anayeruhusiwa kuoa wake wa 4. Hebu kaa na mkeo muyamalize. Jishushe uache michepuko. Ndoa sio mashindano. Fikiria na hao watotoMwanamke haruhusiwi kuchepuka, ulisikia wapi kwenye historia ya Dunia hii mwanamke mmoja akaolewa na zaidi ya mwanaume mmoja? Ila sisi Masheikh mpaka sasa tunaoa hadi 4 teh teh teh!
Hili nalo neno!! Atueleze vizuriWatu mnaingiaga kwenye ndoa huku mkiwa hata hamjielewi.
Inavyoonekana mnaingiaga tu ili kukidhi matakwa potofu ya jamii.
Sasa wewe unalalamika eti mkeo anazifahamu taarifa zako za siri.
Siri gani hizo ilhali mko kwenye ndoa?
Au mliwekeana makubaliano ya mipaka kwenye ndoa yenu kabla hamjaifunga?