Mke wangu kachachamaa anataka tuachane!

Mke wangu kachachamaa anataka tuachane!

Nimetaka watu wa JF wanaishauri namna ya kumsihi mke wangu arudishe moyo nyuma tulee watoto..
haya ni mambo ya mila huwa hayakwepeki

hebu Nenda zako huko kwenye kikao cha familia/ukoo wako walokushauri um-rithi mke wa kaka yako... huko watakushauri ufanye nini kuhusu mkeo maana humu naona hutapata atakayekushauri kwenye hizi so called MILA ZENU....
Eti oooh Mila, kweli kabisa mkuu MILA?




Bora:tape2: mdomo wangu maana nahisi kuchanganyikiwa kabisa na nashindwa kukuelewa kabisaaa, unavokazana kutetea MILA potofu na zisizo na maana!!!gud Luck, kawaambie wazee wa ukoo wako wakushauri kuhusu huyo mkeo humu hamna atakayekuunga mkono i guess!



 
Eti ni kwa sababu kikao cha ukoo kilichokaa juzi kimeamua nimrithi mke wa marehemu kaka yangu aliyefariki mwezi uliopita kwa ajali ya gari.

Kwa mila na desturi zetu inaruhusu mdogo mtu au kaka mtu kumrithi mke wa ndugu yake pale anapofariki. Sasa namshangaa mke wangu kanuna wiki sasa anataka talaka yake aondoke.

Hivi hapa nimechanganyikiwa sijui nifanye nini maana mke wangu nampenda lakini pia nisingependa damu ya kaka yangu ipotee. Lazima mila iheshimiwe...


1. Muache mkeo urithi mke wa marehemu kaka yako.

2. Usimrithi mke wa marehemu kaka yako uendelee kuishi kwa upendo na mkeo.
 
hicho kikao cha familia na wewe uliyeridhia hovyoooooo


au mnataka mali za marehemu? Maana kama mna nia ya dhati mnaweza kumsaidia shemeji yako bila kumridhi... Tena kamati nzima ya ukoo mmeshindwa kuja na njia endelevu ya kusaidia zaidi ya hiyo?

Na huyo mwanamke kakubali umridhi? Au mlikuwa mnatamaniana kabla mumewe hajafa?

Anyway najiuliza tu

Hata mi namshangaa, matamaaa tu yamemshika! Tamaa za mali, tamaa za kimwili nk, sidhani kama ishu ni mila!!!:nono:
 
Mkuu mila zetu zinasema hivyo, na mimi siwezi kukataa kwani nitaachiwa laana na wazee kwa kwenda kinyume na mila na desturi za kabila letu
sasa kama mila na desturi zenu zina sema hivyo, na waogopa laana,, humu umelileta la nn,,, nyambafu wewe...
 
Ni nani kakwambia kwamba kaka yangu kafa kwa ukimwi?
Nishasema kafa kwa ajali mwezi uliopita
Hata kama hajafa kwa ukimwi, inamaana wewe husikii yasemwayo na madhara yatokanayo na kurithi wake za ndugu? siyo vizuri mpeni uhuru, msaidie kulea watoto wa kaka yango, yaani unataka kuvaa viatu vya Bro wako? Acha hizo.
 
Kuna kabila moja huku kwenye visiwa vya ziwa victoria, wana tabia ya "KUWATAKASA WAJANE".eti kila mwanamke anayefiwa na mumewe, ili aweze kuolewa na mwanamme mwingine lazima "ATAKASWE", kwa maana kwamba kuna mwanaume(MTAKASAJI) ameteuliwa kwa kazi hii ya kuwatakasa(KUWAGEGEDA) wajane kabla hawajaolewa tena ili wasipate mikosi kwenye ndoa zao.
Sijajua kama huyu mtakasaji ameoa, na kama ameoa, mkewe anajisikiaje wanapoletwa wajane pale kwake kwa ajili ya kutakaswa?
Kisiwagani hicho? Ukerewe, Ukara,Uzinza, .....????? maana sijawahi kusikia hilo usemalo, maana mm mmoja wa wazazi wangu anatokea huko, so sijawahi kusikia hilo, embu niambie ni kisiwa gani hicho?
 
Kisiwagani hicho? Ukerewe, Ukara,Uzinza, .....????? maana sijawahi kusikia hilo usemalo, maana mm mmoja wa wazazi wangu anatokea huko, so sijawahi kusikia hilo, embu niambie ni kisiwa gani hicho?
Tembea uone.ni huko huko ukerewe.Siku moja wakati tunatoa health education on HIV and preventive measures, baadhi ya wazee wa kisiwa hicho walituomba wawezeshaji tufanye ziara katika kisiwa hicho ili tuweze kutoa elimu juu ya athari za MILA hii ya Utakasaji.This was my first time to know about this tradition
 
Tembea uone.ni huko huko ukerewe.Siku moja wakati tunatoa health education on HIV and preventive measures, baadhi ya wazee wa kisiwa hicho walituomba wawezeshaji tufanye ziara katika kisiwa hicho ili tuweze kutoa elimu juu ya athari za MILA hii ya Utakasaji.This was my first time to know about this tradition
Makubwaaaaaaaaaaaaaaa!!!!! umenifumbua macho, mh!! siwezi kukataa maana sisi wengine tumezaliwa mjini huko ni mpk likizo au kuna tatizo. Anyway asante kwa kuwaelimisha, maana huko elimu ilichelewa sana kufika ndiyo maana hayo yakatokea.
 
Temea chini rafiki yangu, hayo si mambo mazuri kusema hapa JF, mimi siwezi kumuua kaka yangu kwa sababu ya mkewe, mbona wanawake wapo wengi tu, tunachofanya ni kufuata matakwa ya mila zetu.

Mkuu hili jambo usiliangalie upande mmoja. Je haiwezekani yeye akawa amepanga hilo litokee? Huoni ulivyochanganyikiwa hadi huelewi ufanyeje kati ya kurithi na kuachana na mke? tafakari chukuwa hatua.
 
happiness win tamaa iko wapi hapo?

Huioni? Kitendo cha kukumbuka tabia za matusi ulizokuwa nazo kabla ya kuokoka ni "kutamani matapishi" kama wana wa Islaeli walivyotamani nyama za Misri.

Ukishaokoka; ya kale yamepita na sasa yamekuwa mapya! usitamani tena yaliyopita! wala usiyawaze kuwa "bahati yao wangenikuta sijaokoka wangenikoma kwa matusi" huo ni uchafu uliouacha, usiutamani.
 
Sasa kama mke wa marehemu ni mkali unafikiria nn??mwache wife aende ili umridhishe shemeji!!!by the way mbona Family resolution letter hujaiweka hapa ili tuone makubaliano???
 
Mm nilifikiri unatania kumbe uko serious, unatete hoja ya kipuuzi mpaka povu linakutoka, inaonekana akili zako umemuazima mkeo, ndo maana yeye anapingana na upumbavu wako, hata huyo mke wa kaka yako hayupo tayari kurithiwa kwa taarifa yako! Hajui tu chakufanya angejua ungeshia kumzea mate tu! hujui hilo? Watakucheka watu? Eti mila, unajua maana ya mila wewe, eti mnaiga utamaduni wa maghalibi, mbona umevaa suari? vua uvae ngozi kama kwel wew ni mtunza mila, kubwa jinga!! watakucheka watu!! Hata drs la pili halijakusaidia? Shame on you! Mpe taraka mkeo haraka usije ukamletea kifo kabla ya wakati wake! Mzinzi kubwa we!
 
Naomba tuheshimiane mkuu, mimi nafuata mila za kabila letu hata wewe una mila za kwenu sema tu umezitelekeza kwa kudanganywa na mila za Magharibi
Kama unaona sisi tunadanganywa, sasa si ungezifuata tu hizo mila zako bila kuja kuuliza huku? Unafanya mambo kama walimu wanauliza maswali kwenye mtihani wakati majibu wanayajuwa... Au nawe ulikuwa unatupima kama wafanyavyo walimu?
 
Kuna kabila moja huku kwenye visiwa vya ziwa victoria, wana tabia ya "KUWATAKASA WAJANE".eti kila mwanamke anayefiwa na mumewe, ili aweze kuolewa na mwanamme mwingine lazima "ATAKASWE", kwa maana kwamba kuna mwanaume(MTAKASAJI) ameteuliwa kwa kazi hii ya kuwatakasa(KUWAGEGEDA) wajane kabla hawajaolewa tena ili wasipate mikosi kwenye ndoa zao.
Sijajua kama huyu mtakasaji ameoa, na kama ameoa, mkewe anajisikiaje wanapoletwa wajane pale kwake kwa ajili ya kutakaswa?

Sipati picha hicho cheo cha utakasaji kinavyotamaniwa na wengi
 
Back
Top Bottom