Mke wangu kachachamaa anataka tuachane!

Mke wangu kachachamaa anataka tuachane!

Eti ni kwa sababu kikao cha ukoo kilichokaa juzi kimeamua nimrithi mke wa marehemu kaka yangu aliyefariki mwezi uliopita kwa ajali ya gari.

Kwa mila na desturi zetu inaruhusu mdogo mtu au kaka mtu kumrithi mke wa ndugu yake pale anapofariki. Sasa namshangaa mke wangu kanuna wiki sasa anataka talaka yake aondoke.

Hivi hapa nimechanganyikiwa sijui nifanye nini maana mke wangu nampenda lakini pia nisingependa damu ya kaka yangu ipotee. Lazima mila iheshimiwe...

Nani alikudanganya kuwa damu ya mke wa kaka yako ni sawa na damu ya kaka yako? Wenye damu ya kaka yako hapo ni watotowa marehemu tu huyo mama hana uhusiano wowote wa kibaiolojia na wewe. Labda kuna vitu vingine unavyotamani kwa huyo mwanamama.
 
Tegelezeni Tegelezeni mbona hivi lakini??? Damu ipi isipotee?? Mke wa marehemu kaka yako amekuwa ndugu yako? Watoto wa marehemu kaka yako na shemeji yako ndio ndugu zako wa damu sasa inakuwaje hii? Hizi mila zingine wajameni ni ngumu sana. Mwacheni naye akatafute riziki nyingine mbele ya safari kwa nini kumuweka kifungoni....Mkeo ana haki ya kudai talaka kwani kabla ya kumuoa ulimpa maelekezo kuhusiana na mila zenu? kama hukufanya hivyo basi ni haki yake kuomba talaka naye akatafute riziki mbele ya safari. Huu umangimeza utakuponza mkuu
 
Mimi ni mzaliwa wa mkoa wa Tanga.
Ukoo na mwengine sitakueleza
Hivi ukishindwa kumtimizia halafu ukakuta shambaBoy ndio anakung'uta na Mimba mnaletewa utauambiaje ukoo wenu
Nashauri mtimizie Mkeo kwanza maana utasababisha wote wakapuliwe nje kwa hasira wakati huna ubavu (Avatrtar yako)
 
kinachotakiwa hapo ni kuheshimu mila na desturi,achana na hawa vijana wasiojua walipotoka wanabaki kukumbatia mila na desturi za kimagharibi kwani ni mental slaves
ukweli ndio huo mtu huwez kulea 100% familia ya mwenzako lazima utawapunja tu lakini ukimrithi utaweza kujitolea 100% kusaidia familia

ila kabla ya kumrithi ningekushauri mkapime ili wote muwe salama

wife pia jaribu kumwelewesha ni mambo ya kawaida tu mbona waislamu wanaoa wake 4 na watu hawasemi?

na unamrithi ili kuisaidia familia ya kakako,waweze kupata malez ya mama na upendo kama wa baba yao wa mwanzo na kuweza kujitolea kulea watoto kikamilifu kama wa kwako vile,kwani ni uongo kuwalea wale watoto kwa upendo kama hakuna kinachounganisha kati ya mama na mlezi baba

halaf watu wengi wanapinga kwa sabab ni mila za mwafrika basi inakua nongwa kwao wanakuona primitive, ila kiukweli unajitambua zaidi kuliko wao
 
sion sababu ya kumshauri lililo bora kwa bado anapngana na weng humu ndan...mi kwa ushaur wangu acha pendo la dhat nenda karith kwa kuwa ndio chaguo lako,sembuse hiv ulivotoa hii coment yako tayar usharith.mi naona hata ushauriwe vp hutokubali.kaka unaonekana ulipenda shemejio toka kitambo na ukataman hata hilo litimie,chukulia wife wa kaka yako angekuwa ana maradh na c mzur kuzid wa kwako je ungemuacha wa kwako na kumshobokea shemejio?tafakar ndg we c mtoto utakaye wembe
 
kinachotakiwa hapo ni kuheshimu mila na desturi,achana na hawa vijana wasiojua walipotoka wanabaki kukumbatia mila na desturi za kimagharibi kwani ni mental slaves
ukweli ndio huo mtu huwez kulea 100% familia ya mwenzako lazima utawapunja tu lakini ukimrithi utaweza kujitolea 100% kusaidia familia

ila kabla ya kumrithi ningekushauri mkapime ili wote muwe salama

wife pia jaribu kumwelewesha ni mambo ya kawaida tu mbona waislamu wanaoa wake 4 na watu hawasemi?

na unamrithi ili kuisaidia familia ya kakako,waweze kupata malez ya mama na upendo kama wa baba yao wa mwanzo na kuweza kujitolea kulea watoto kikamilifu kama wa kwako vile,kwani ni uongo kuwalea wale watoto kwa upendo kama hakuna kinachounganisha kati ya mama na mlezi baba

halaf watu wengi wanapinga kwa sabab ni mila za mwafrika basi inakua nongwa kwao wanakuona primitive, ila kiukweli unajitambua zaidi kuliko wao

Katika wote waliochangia huu uzi, ni wewe peke yako ndio umeongea pwenti, hawa wanaotokwa na povu humu haiyumkini wengine ni watoto wa baba wa kurithi sasa kwa kuwa labda hilo limewakera sasa weshapata pa kupunguzia hasira zao
 
sion sababu ya kumshauri lililo bora kwa bado anapngana na weng humu ndan...mi kwa ushaur wangu acha pendo la dhat nenda karith kwa kuwa ndio chaguo lako,sembuse hiv ulivotoa hii coment yako tayar usharith.mi naona hata ushauriwe vp hutokubali.kaka unaonekana ulipenda shemejio toka kitambo na ukataman hata hilo litimie,chukulia wife wa kaka yako angekuwa ana maradh na c mzur kuzid wa kwako je ungemuacha wa kwako na kumshobokea shemejio?tafakar ndg we c mtoto utakaye wembe
Wale waleee
Kwetu kurithi hatuangalii uzuri bali tunaangalia majukumu ya kulea familia ya marehemu na kuhakikisha inapata huduma zote
 
Wale waleee
Kwetu kurithi hatuangalii uzuri bali tunaangalia majukumu ya kulea familia ya marehemu na kuhakikisha inapata huduma zote

Huna lolote sema we ulimtaka kummega shemejio kitambo.....nahisi hata msiba hukuhuzunika
 
Ni nani kakwambia kwamba kaka yangu kafa kwa ukimwi?
Nishasema kafa kwa ajali mwezi uliopita

Hawa pepo wengine ni noma, mie naona kama mleta thread kaleta makusudi ili kuwakasirisha wanaMMU, iwe kafa kwa ajali ama kwa kuchukuliwa msukule bado mambo ya kurithi yashapitwa na wakati. siafiki hata kidogo nyie ndo wale wale mnaowaombea kaka zenu wafe ili mrithi wake zao, so unaona ni vema kuachana na mkeo ili umrithi shemeji yako? fikiria kwanza ni kwa nini usiwafikirie watoto wa kaka yako kwa kuwaendeleza kuliko kurithi? acha nisiongee sana maana nazidi kujaa sumu bureee.
 
Mkubwa mzma unakaa na kuandika Uzi kama huu kweli?,,je kama kaka yako angekuwa kama amekufa na UGONJWA WETU ULE ungefuata MILA?
2013 hii mkuu sio kipindi cha Giza tena
 
Jamani, damu ya kaka yako inapotea kwa kutokumuoa mke wake!? Kama una uezo si umtunze na wanae huko huko kwake aliko? Au kumtunza ni mpaka 'umuoe'?

Hivi karne hii bado tunarithishana wake?
 
Tatizo kubwa naona kuwa ana majibu na maamuzi tayari ndiyo maana kila anayemshauri kutomrithi shemeji yake anapingana naye. Alitegemea wanaJf wana mawazo kama yake.

Endelea na maamuzi yako kama unavyofikiria, muache mkeo akatafuta mwelekeo mwingine.
 
Samahani mleta mada,
hata mimi ningeomba talaka ili niondoke.
 
Back
Top Bottom