Mke wangu kachachamaa anataka tuachane!

Mke wangu kachachamaa anataka tuachane!

Angalia utapata laana mwanamke, mambo ya mila sio ya kuchezea utaokota makopo ohooooo!!!!
Mila gani wewe za kishenzi hizo.... Kuendekeza umalaya tu huko. Kama vipi toa talaka halafu umuoe mle wa marehemu
 
.....Unajua kaka yako kafa na nini? Utakufa kwa ukimwi shauri yako.
Hebu muache huyo mkeo usije muua bure!!
 
Eti ni kwa sababu kikao cha ukoo kilichokaa juzi kimeamua nimrithi mke wa marehemu kaka yangu aliyefariki mwezi uliopita kwa ajali ya gari.

Kwa mila na desturi zetu inaruhusu mdogo mtu au kaka mtu kumrithi mke wa ndugu yake pale anapofariki. Sasa namshangaa mke wangu kanuna wiki sasa anataka talaka yake aondoke.

Hivi hapa nimechanganyikiwa sijui nifanye nini maana mke wangu nampenda lakini pia nisingependa damu ya kaka yangu ipotee. Lazima mila iheshimiwe...

Hivi mke wa nduguyo ni damu ya nduguyo kweli? Au wewe umekosa la kujitetea
 
hana la kujitetea huyo mpenda wake za marehemu a.k.a wajane
Naomba tuheshimiane mkuu, mimi nafuata mila za kabila letu hata wewe una mila za kwenu sema tu umezitelekeza kwa kudanganywa na mila za Magharibi
 
.....Unajua kaka yako kafa na nini? Utakufa kwa ukimwi shauri yako.
Hebu muache huyo mkeo usije muua bure!!
Acha kashfa, kufa kwa ajali ndio ukimwi?
Nawashangaa mnanishupalia wakati hamjua lolote zaidi ya kukurupuka, mila zetu zina historia na tunazienzi kwa sababu ya kutukuza uafrika wetu sio kama ninyi mnafuata mila za watu na kutelekeza zakwenu
 
Mikosi gani kwa mfano?

Je ukitunza watoto afu usitoe unyumba kwa mjane?

Disown you? Do they own you? - Nkem Owoh
Wewe hujui mambo ya mila ndio maana unadharau, ngoja yakukute utakuja hapa kusimulia, labda ufanye siri
 
kwani aliyekufa kwa ajali hawezi kuwa alikuwa nao kabla we una hakika gani na afya yake? Mila nyingine inabidi zifutwe tu hali ya sasa au we mwenzetu unaishi nchi gani, mana nashangaa eti mpaka leo hii bado hizo mila na desturi........tafakari na chukua hatua!!!!!! Achana na mambo ya kizamani
Hivi unaweza kuniambia ni lini mila za kale zilifutwa? na kwa mamlaka ya nani?
Nyie mmedandia mila za watu na kutelekeza zakwenu na ndio maana mnashangaa, huku kwetu haya mbona ni mambo ya kawaida sana tu.
Tembeeni muone, muondoe hizo tongotongo
 
Duh, hii mila hata kwenye jamii yangu ipo na niliwahi kuiona inatekelezwa kwenye ukoo, lakini baadaye tuliipiga marufuku isiendelee na wajane wa familia yetu walituunga mkono na kutushangilia sana baadhi yetu japo tuliwakwaza sana baadhi ya njemba za wana ukoo.

Mara nyingi hizi ni tamaa tu za sisi wanaume hakuna cha mila wala nini
 
haya mambo ya kurithishana bado yapo.....bora mke aende zake akuache na mkeo wa kurithi asije naye akarithiwa
 
Mpe talaka yake aende zake kwa amani na MUNGU amjalie huko aendako afanikiwe wala asikukumbuke tena ubaki na mjane wako, unataka kumuua mwenzio na virus. Bado watu badala ya kutafuta hela mnakaa vikao vya uzinzi.

Umejuaje kama huyo mke wa kaka yako anakupenda? Unahisi watoto wake watajisikiaje wakikuona unalala kitanda cha baba yao? Ingekuwa ni mama yako anatembea na baba yako mdogo ungejisikiaje?

Inaelekea ulikuwa unamtamani toka kaka yako akiwa hai!
Hahahahaha kweli hapo naona inafagiliwa ngono tu si bure. Yaani hata enjili huko aliko huyu bwana haijafika au hata ustarabu wa kawaida nao hakuna loh mbona kazi ipo. Kuna mila njema na mila mbovu , mila mbovu yafaa zikaachwa na njema zikaendelezwa. Hivi huwezi mtu kutoa msaada mpaka na wewe upate kitu loooooooooooh shame on him
 
Kuna kabila moja huku kwenye visiwa vya ziwa victoria, wana tabia ya "KUWATAKASA WAJANE".eti kila mwanamke anayefiwa na mumewe, ili aweze kuolewa na mwanamme mwingine lazima "ATAKASWE", kwa maana kwamba kuna mwanaume(MTAKASAJI) ameteuliwa kwa kazi hii ya kuwatakasa(KUWAGEGEDA) wajane kabla hawajaolewa tena ili wasipate mikosi kwenye ndoa zao.
Sijajua kama huyu mtakasaji ameoa, na kama ameoa, mkewe anajisikiaje wanapoletwa wajane pale kwake kwa ajili ya kutakaswa?

Tanzania kuna mambo
 
marehemu kaka yako alipima???????swali lingine...hivi huko kwenu tarehe mnazotumia zimeshafika ANGALAU 1900?swali la mwisho tafadhali......unaishi misitu ya kongo au tanzania hii hii?

Hahaaaaa umeniacha hoi kweli,,jaman huyu atakua mtu wa wapi lol hvi haya mambo bado yapo cku hziiii hawa ndo wale wanaooshaga condom na maji nakumwazima mwenzie kahhh eti kumrithi mke wa kakako hata haya uoni!!! Ebu tutolee ubwege hapa
 
mnh wanaume wangine,akili zao zimebaki za kuvukia barabarani yaani leo kisa kuna k free umepewa basi na wewe unajipeleka hapo,haujali litavuruga equilibriam ya ndoa yako uliyoijenga miaka kadhaa,wahiii the best your wife could do is to divorce your sorry ass,hufai hata kwa kulumangia aka si riziki:nono::nono:
 
hahahaaaaaaaaaaaaaa
MC Tillya umenichekesha ujue...
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom