Mke wangu ananiumiza kichwa

Mke wangu ananiumiza kichwa

Pole ya kawaida hayo, ongea nae delete hiyo account Facebook, jipe muda maumivu yapungue msamehe maisha yaendelee.....
Ile habari ya tuoe makabila gani inaendelea.
Hatua ya kwanza kaa ongea nae mweleze madhara ya anachofany baada ya hapo angalia mienendo. Ukiona bado fata hatua za kushirikisha wasimamizi wa ndoa, ikishindikana hapo peleka kwa kasisi wako, Sina imani kama kote kitakataa
 
Mim nasema tabia haubadiliki ya mtu na wale tu wenye roho ya mungu ndio wawezao kusamehe usalit pole sana mungu akutie nguvu....!Watu wanaudhi jamani???Palipo na usalit hata baada ya msamaha raha ya wawili haiwezi kuwa the same as b4...Muheshimu anayekuheshimu
 
Habari za jumatano wanajamvi, bila shaka mmeamka salama kabisa.

Leo nimekuja huku kuomba ushauri maana tangu usiku sijalala kichwa kinawaka moto.Nimeoa miaka minne ilitopita, kabla ya hapo niliambiwa kabila la Mbulu sio la kuoa mie moyo ukawa umenasa hivyo na pete kanisani ikavaliwa. Nimebarikiwa mtoto mmoja wa kike.

Mwaka 2011 nilimfungulia account facebook mchumba kabla sijamuoa na nilikuwa namuamini sana.Tatizo Jana (Jumanne nikiwa kazini akaniambia account yake imesumbua halafu njia ndio mie hivyo nikiwa kazini nikalog in kwenye account yake (ikumbukwe tangu nimuunge sijawahi ingia kwenye inbox wala kugusa simu yake) baada ya kumrekebishia tatizo lake nikaona niingie inbox kwa mara ya kwanza.

Ukweli mie sinywi pombe lakini Jana nilijikuta naondoka kazini mapema na kwenda kuzimua kichwa. Nimekuta message nyingi anachat na vijana za ajabu ajabu mara mume wangu nitamuaga naenda kwa ndugu nitakuja kwako, mara mume wangu hayupo halafu nipo kitandani peke yangu baridi kali, Mara nimetoka kuoga ndio najifuta now, halafu anagawa namba yake ya simu kirahisi kwa kila anayemuomba namba. Yaani nusura nianguke ofisini maana mpaka wenzangu wamejua kuna tatizo ila sijafungua mdomo wangu.

Nimerudi nimemkuta ananichekea yani sijaongea kitu roho inaniuma vibaya, nahangaika kutoa jasho kwaajili ya kumpendezesha na mtoto wetu ila kaniona boya. Wakati naanza uhusiano nae nilikuta akiwa na elimu ya darasa la saba tu, nikamuendeleza QT na kumfundisha mpaka now ana diploma na October anaingia degree, sijui hata nifanye nini haki ya Mungu inanitesa sana.

Pole sana kaka. Pole sana sana.... Ila inaonekana bado hajaliwa kwi kwi kwi kwi kwi kwi.... Kaa naye chini muulize kwa upole ukiwa na evidence.... Print some of the messages ...Nafikiri atakupatia majibu kwa anachokifanya... Labda kuna vitu anavikosa kwako....
 
Mkuu kwenye mtoto sina Shaka mtoto kafanana na mama yangu kila kitu mpaka bimkubwa akamkabidhi jina lake, maana wakubwa zangu walitangulia kuzaa hakuna aliyekabidhi mwanae jina la mama ila alipozaliwa wangu mama akamtazama Akasema iwe isiwe lazima aitwe jina lake na wamefanana kweli...hapo sina Shaka ila kwenye kukung'utwa na watu wengine hapo ndio roho inaniuma maana sina ushahidi wa moja kwa moja ila message zimeniumiza vibaya
Ilo ni sawa mkuu,ila pia kamcheki yeye mwenyewe afya yake ni salama namaanisha HIV ndo maamuzi mengine,nakushauri kwa hilo maana yalishanikuta ya namna hiyo
 
tabia za wanawake wengi sana hasa wa facebook,hata mm nachat nao sana unaweza hata kumtongoza mwanamke facebook na asikwambie ukweli wowote kuwa ana mwanaume au lah! na hata ukisema uangalie inform zao unakuta wengi wao wameandika #SINGLE wakati mtu yupo #INLOVE......facebook ni shida sana, fanya tu kudelete hiyo account
 
Gonga goli saba afu mwambie hutaki mchezo kizembe. Tatizo litakwisha, tatizo lenu vijana mkioa mnaacha style zenu za kisera afu wasera wanawageuzia michezo.
 
tabia za wanawake wengi sana hasa wa facebook,hata mm nachat nao sana unaweza hata kumtongoza mwanamke facebook na asikwambie ukweli wowote kuwa ana mwanaume au lah! na hata ukisema uangalie inform zao unakuta wengi wao wameandika #SINGLE wakati mtu yupo #INLOVE......facebook ni shida sana, fanya tu kudelete hiyo account
Mkuu kudelete account sio solution, nakumbuka 2006 niliwahi kuwa na mwanamke mmoja alikuwa akisoma Uganda, Akasema anaboreka Facebook hivyo akadelete account yake nikajua hayumo...baadae nikaja jua anatumia account nyingine tena miongoni mwa list ya friends zangu, nilitambua kwakua nilikuwa najua namna anavyochat, swaga zake na connection ya vitu alivyokuwa anapost...ulimwengu wa Sasa hata nikidelete account anaweza fungua nyingine au pia kumbuka anagawa namba hovyo maana yake hata nikidelete account ni kazi bure, kuna whatsapp, telegram, viber n.k mambo yatakuwa yale yale tu...hapo sijui whatsapp na kwingineko anachat nini huko na kina nani mpaka leo
 
Mkuu kudelete account sio solution, nakumbuka 2006 niliwahi kuwa na mwanamke mmoja alikuwa akisoma Uganda, Akasema anaboreka Facebook hivyo akadelete account yake nikajua hayumo...baadae nikaja jua anatumia account nyingine tena miongoni mwa list ya friends zangu, nilitambua kwakua nilikuwa najua namna anavyochat, swaga zake na connection ya vitu alivyokuwa anapost...ulimwengu wa Sasa hata nikidelete account anaweza fungua nyingine au pia kumbuka anagawa namba hovyo maana yake hata nikidelete account ni kazi bure, kuna whatsapp, telegram, viber n.k mambo yatakuwa yale yale tu...hapo sijui whatsapp na kwingineko anachat nini huko na kina nani mpaka leo
duuuh! pole sana
 
Hiki kiherehere cha wanaume wezangu kitawapoza sana,
.na kwa ushauri usimuulize mwambie tu akueshimu kuliwa ataliwa tu,
Ukiona mambo magumu jipange umwache kimya kimya!!
Swala la kuwa. Mbulu sio ishu!
Kwa sasa mabinti wote wanafanana vitabia kikubwa ni.kupata anaye kueshimu.
 
Kabila hilo hata ubadili lugha atapigwa tu nje. Nina mfano hai kabisa wa ndg yangu wa karibu kabisa alichofanyiwa hadi leo kuoa tena kaingiwa ganzi. Zamani nilijua wanawasingizia tu, ila toka hilo litokee nimeconclude mazima
 
Mkuu kwenye mtoto sina Shaka mtoto kafanana na mama yangu kila kitu mpaka bimkubwa akamkabidhi jina lake, maana wakubwa zangu walitangulia kuzaa hakuna aliyekabidhi mwanae jina la mama ila alipozaliwa wangu mama akamtazama Akasema iwe isiwe lazima aitwe jina lake na wamefanana kweli...hapo sina Shaka ila kwenye kukung'utwa na watu wengine hapo ndio roho inaniuma maana sina ushahidi wa moja kwa moja ila message zimeniumiza vibaya
Kaka huyo wala hajakuchit, wake za watu wanaochit wala hawachati chati hovyo huyo ni kutojitambua tuu, the good enough ni Mungu amekuonyesha ili umzindue kwenye hiyo mitego ya hivyo.
Ongea nae tuu ataelewa nawe jitahidi sana kumepnda na kuongeza kuchart nae ili kumweka karibu.
Tatizo mkishaowa mnajifanya busy sana.
 
Hawa kina katarina wa mbulu wametuumiza wengi sana, wao kukataa hawajui
 
Mkuu hapo huna Mke! Wote ni vijana, na tuna account facebook pia, tunakutana na wanawake maharage ya mbeya, but wapo wengine wana msimamo, akiona husikii unamsumbua Anaku block, kwa jinsi ulivyosema tena Mkeo ni Mbulu!!!? Utakuja kufa na ukimwi bure, mbaya zaidi wanawake wa hivyo hata Condom hakumbuki........huwa inauma Kama mwanaume unajitambua, unatunza familia yako, umetulia na unatambua hatari ya Ukimwi, hafu mke ni kicheche, hajari kila kitu anachukulia rahisi, ulichoona sio habari za kuambiwa umeona messages mwenyewe, hata uka delete fb yake, ukamzuia na simu, mwanamke wa hivyo anaweza kugongwa hata bafuni Kama ni uswazi, atagongwa na hata shamba boy, amekua mtoto huyo wa kumchunga? Huwezi kumbadilisha sasa!

Piga chini huyo mke! Uhai wako kwanza!
 
Unaweza kuta hajawahi toka nje ya ndoa ila ni tabia tu za wengi pindi anapoingia kwenye mitandao na kuanza kuchat na kila mtu ilimradi anapoteza mda tu.

Wengi wa binadamu sasa unaweza mkuta anachat na mphilipino huko Manila na hata ndege hajawahi panda lakini kakazana tu.

Sio wote wanafanya kweli ila huenda amekuwa bored inabidi uwe unamtoa out (kama hamtoki) ili ajisikie.

Utakuta hata wewe unachat na marafiki hewa 1000 lakini in reality hujatembea nao hata wawili katika hao.

Take it easy[/QUOTE
Your very positive ! yaan nyie ndio watu wachache ambao wamebakia hutaki kufikiri negative zaidi simu ya mkeo au mpenzi haijapokelewa unawaza atakuwa mbali na simu anaoga au kuna kazi anafanya .Lakini kuna wengine ni kuwaza hasi! hasi!muda wote
 
2009-2011 akafanya mtihani wa form four, 2012 February inshallah akapata matokeo sio mazuri sana wala sio mabaya akaingia certificate ila 28 July akadaka ujauzito, 21 November 2012 ndoa..15/4/2013 akajifungua mtoto wa kike. 2013-2015 Diploma kamaliza Mwaka Jana akapumzika Mwaka huu anaapply degree, mtoto wetu ana miaka mitatu now...nikutaarifu tu huyu binti alijaa vyema nilianza kumsomesha QT January kabla sijapata jibu kuwa ni demu wangu kisha April 2009 ndio akakubali kuwa kwenye uhusiano akiwa anasoma.
Sawa nimekuelewa
 
Mzunguke kwa kumpa nasaha za ndoa,na heshm ya mke inavyotakiwa kua ikiwemo maswala ya mavazi,kauli na ustaarabu na uaminifu...ukifika katika ustaarabu na uaminifu lenga jinsi mitandao ya kijamii inavyovunja ndoa za watu hapa weka mfano wa ufska wanaofanya watu FB msisitize mkeo jinsi unavyompenda na usihitaji upuuzi katika ndoa yako,kama unamfano wowote anuai mpe,hapo nadhani atajistukia na anaweza kujirekebisha.JAZBA,HASRA NA MAAMUZI YA HARAKA YAMEWAJUTISHA WENGI.
 
Back
Top Bottom