Mke wangu ananiumiza kichwa

Mke wangu ananiumiza kichwa

Habari za jumatano wanajamvi, bila shaka mmeamka salama kabisa.

Leo nimekuja huku kuomba ushauri maana tangu usiku sijalala kichwa kinawaka moto.Nimeoa miaka minne ilitopita, kabla ya hapo niliambiwa kabila la Mbulu sio la kuoa mie moyo ukawa umenasa hivyo na pete kanisani ikavaliwa. Nimebarikiwa mtoto mmoja wa kike.

Mwaka 2011 nilimfungulia account facebook mchumba kabla sijamuoa na nilikuwa namuamini sana.Tatizo Jana (Jumanne nikiwa kazini akaniambia account yake imesumbua halafu njia ndio mie hivyo nikiwa kazini nikalog in kwenye account yake (ikumbukwe tangu nimuunge sijawahi ingia kwenye inbox wala kugusa simu yake) baada ya kumrekebishia tatizo lake nikaona niingie inbox kwa mara ya kwanza.

Ukweli mie sinywi pombe lakini Jana nilijikuta naondoka kazini mapema na kwenda kuzimua kichwa. Nimekuta message nyingi anachat na vijana za ajabu ajabu mara mume wangu nitamuaga naenda kwa ndugu nitakuja kwako, mara mume wangu hayupo halafu nipo kitandani peke yangu baridi kali, Mara nimetoka kuoga ndio najifuta now, halafu anagawa namba yake ya simu kirahisi kwa kila anayemuomba namba. Yaani nusura nianguke ofisini maana mpaka wenzangu wamejua kuna tatizo ila sijafungua mdomo wangu.

Nimerudi nimemkuta ananichekea yani sijaongea kitu roho inaniuma vibaya, nahangaika kutoa jasho kwaajili ya kumpendezesha na mtoto wetu ila kaniona boya. Wakati naanza uhusiano nae nilikuta akiwa na elimu ya darasa la saba tu, nikamuendeleza QT na kumfundisha mpaka now ana diploma na October anaingia degree, sijui hata nifanye nini haki ya Mungu inanitesa sana.
Mkuu kwanza kabla ya yote kachekini afya kwanza ndo maamuzi mengine yaendelee dunia imeisha wakuu.
 
Kabla hujapata ganzi zaidi baada ya maongezi na huyo mwenza wako naona ni vyema ukampime mwanao DNA. Kuna uwezekano mkubwa ukawa unalea mtoto wa mwenzako.
 
Hiyo stereotype
Mi najua kila mwenye mbunye anaigawa, usiwaseme vibaya mawifi zangu ha ha ha ha ha
tofautisha kugawa na kugawa kirahisi,,yani kwa kila anaeitaka hyo mbunye

au na ww mbulu nn nianze kupga misele??
 
Evelyn kinachoniuma ni kwamba before sijakutana nae nilikuwa Malaya mbwa ila nlipokutana nae nikajua roho mtakatifu kanigusa na nikabadilika kabisa, nikiwaza hapa atakuwa ameshanisaliti mara ngapi mpaka hivi leo? Kazi yangu yenyewe ni mikoani mara kwa mara naweza kaa mkoani hadi miezi mitatu kama project ni ndefu kiaina...hapo Kati atakuwa ameshakung'utwa vya kutosha, kama Facebook anajirahisi kiasi hichi vipi vijana wa hapa mtaani? Naweza kuwa nasalimiana na vijana wenzangu mtaani kumbe wananicheka wanavyonimegea mke wangu, sijui naanzia wapi kuongea nae, Nina hasira za karibu na sijawahi mpiga hata siku moja, nahisi Naweza fanya kitu cha ajabu....kichwa kinaniuma vibaya hapa
 
Tatizo la mkeo ni ELIMU ELIMU ELIMU.

Hizo Elimu za kuunga unga Mara nyingi haziwasaidii saaana mana kwanza kusaidiwa kwingi na vijana.

Kwasababu inaonekana ana ulimbukeni mwingi, mpige kibano cha hatari asirudie tena akirudia cossovo inamhusu.
Kama elimu ingekuwa inasaidia watu kuacha usaliti kila mtu angeoa mwenye elimu ya juu sana.
 
pole sana mkuu kwa hayo yaliyokukuta.jipe moyo mkuu just kaa naye chini mwulize hayo uliyoyakuta huko kwenye message yake.pia usihukumu kabila nzima la watu kwa kosa la mtu moja .hiyo hulka ya mtu.hilo ni jaribu lako lakupasa ulishinde
 
Kijana account ulimfungulia mwenyewe cha kufanya blok hio accaunt lakini kwa elimu aliyonayo kwa sasa atafungua account nyingine amna jinsi kaza moyo
 
mkuu kwanza pole sana sana tena sana mungu akupe subra katika kipindo hiki kigumu sana kwako .

mandiko ya dini yanasema :mwanamke ni mtu wa kuishi nae kwa akili sana .na ndomana hata mtume alimwelezea mwanamke ni kiumbe aliyeumbwa kwa ubavu uliopinda .ukitumia nguvu sana utauvunja na ukiacha basi utazidi kupinda ..

maana ya maneno haya .ni kwamba unapoishi na mwanamke ni wakumwangalia sana hutakiwi umwache kwa uhuru sana bila kumwangalia .

ushauri wangu kwako kaka .mke ulimwacha sana huru na ukamwamini kupitiliza na matokeo yake ni hayo .badilika mkuu maana utawaona wanawake wote wabaya .maana jinsi walivyoumbwa wao ni watu ambao wanataka mara nyingi uwangalizi .maana hata shamba likiachwa bila uwangalizi na usimamizi.basi matokeo yake hugeuka shamba la bibi na kila mtu kuchuma mazao shambani.

Yangu ni hayo mungu akupe subra katika hili.
 
Pole sana kaka, ongea nae kwa upendo kwani huyo anaonekana maisha aliyoishi mwanzo hakuwa exposed sana, kwa hiyo anafurahia tuu kuchart hivyo na ukute wala hana mpango wa kukuchit ila basi tuu anajisikia raha kuchati
Mweleze kwa upendo,a umchimbe beat la ukweli naamini hatarudia tena.
 
Mkuu kwanza kabla ya yote kachekini afya kwanza ndo maamuzi mengine yaendelee dunia imeisha wakuu.
Mkuu kwenye mtoto sina Shaka mtoto kafanana na mama yangu kila kitu mpaka bimkubwa akamkabidhi jina lake, maana wakubwa zangu walitangulia kuzaa hakuna aliyekabidhi mwanae jina la mama ila alipozaliwa wangu mama akamtazama Akasema iwe isiwe lazima aitwe jina lake na wamefanana kweli...hapo sina Shaka ila kwenye kukung'utwa na watu wengine hapo ndio roho inaniuma maana sina ushahidi wa moja kwa moja ila message zimeniumiza vibaya
 
Bs mkuu km unamjua vizuri kuna kitu kimepelekea yeye kufanya hayo,na pengine usikimbilie kwny conclusions,usikute hajatombwa ba hao watu anaochat nao,inweza kuwa flirting,la msingi ongea nae msikilize.
 
Hii kamba ngumu, kaa jisikilize mwenyewe ufanye maamuzi yaliyosahihi ila ningekushauri tu, hili swala si vyema ukalitoa nje kabla ya kumwambia yeye mhusika. Ni vyema umwambie ili uone response ya uso wake, iwe ni ya kujutia au kuchukulia poa halaf ufanye maamuzi
 
hawa dada zetu sa hv wanatutesa kwel, pole ndgu nadhan comment ya victor j ya kwnzaukiifata ni vzur pia
 
Back
Top Bottom