Kazi kweli kweli, hadi nashindwa pa kuanzia.
Ila moja fukuza house boy, then fanya utaratibu mkae pamoja ninyi wawili myazungumze nadhani hamjachelewa.
Ninyi nyote mmekutana, hiyo ilikuwa janja tu hakuna cha kulipiza kisasi wala nini, kuna katabia hako kama wewe ulivyo pia.
Mwisho wa yote kubalini/ tukubari kuziheshimu ndoa zetu ni za thamani sana, tunaweza kuwa na tamaa ndio, lakini tusikubali tamaa itushinde na kuongoza maisha yetu ya mapenzi. Tutimize wajibu wetu kwa ndoa, tumpende Mungu na kutenda yampendezayo na kwa kufanya hivyo tutafaidi ndoa zetu katika hali ya amani.
Pole ila jitahidi yaishe ili ndoa iendelee kama awali.