Herbalist Dr MziziMkavu
Platinum Member
- Feb 3, 2009
- 43,073
- 34,844
- Thread starter
- #101
Mke wangu alinifanya niwe Mchawi - 44....
ILIPOISHIA;
Nilikumbuka siku moja ambayo nina imani katika kusimulia sikulisema hili. Ni kweli siku moja nikiwa kazini baada ya kazi ya kutoa vifaa ambavyo vilikuwa vingi na kunifanya nisimame kwa muda mrefu.
Nilipokaa kichwa kilianza kuniuma kama kinapasuka kikifuatiwa na kutokwa damu nyingi puani. SASA ENDELEA...
Nilikimbizwa hospitali ambako nilikutwa na malaria. Baada ya matibabu nilijisikia vizuri na kuruhusiwa kutoka hospitali. Hali ile haikujirudia tena na kuamini yale yalikuwa malaria tu.
Basi yale hayakuwa malaria ilikuwa ndiyo safari, shukuru kupelekwa kwenye mizimu, uchawi uliofanyiwa mbaya sana. Kutoka damu puani ilikuwa safari isiyo na kwaheri. Lile lilikuwa jini la kutumwa, jini Makata lilikuwa likukate palepale.
Baada ya kuona kwako ngoma nzito walibadilisha mashambulizi na kuyaelekeza kwenye familia yako. Wameanza na baba yako baada ya hapo atatafutwa mtu mwingine.
He! Ina maana wamepanga kuiteketeza familia yangu yote? nilishtuka kusikia vile.
Ndiyo.
Wanatumia uchawi wa ndizi, wanaroga kwenye mkungu wa ndizi wenye ndizi mbichi, ikiiva ndizi moja na kudondoka, basi katika familia yako anaondoka mtu mmoja.
Mungu wangu! nilishika kichwa kwa mshtuko.
Mtego wao haukuwasumbua kukunasa kwa vile kilikuwa kisasi cha kuuawa ndugu yao, hivyo ilikuwa rahisi kukupata.
Sasa utanisaidiaje?
Kazi hii kwa uwezo wangu nzito sana, ila nitakuelekeza kwa mzee mmoja ambaye alikuwa swahiba wa baba, naye yupo vizuri kama mzee Kidereko.
Anakaa wapi?
Maeneo ya mbele kidogo japo kuna kamwendo kadogo.
Tunaweza kwenda leo?
Tunaweza kwa vile muda bado.
Tunaweza kutumia gari?
Hatuwezi kwenda na gari kutokana na eneo lenyewe, lazima tupande kilima na kushuka.
Usiku hakuna wanyama wakali?
Hakuna.
Tulikubaliana kwenda kwa mganga mwingine baada ya ngoma yangu kuwa nzito kwake. Tuliongozana wawili kuelekea kwa mganga, ilikuwa safari ya kupanda na kushuka milima mpaka kufika kwa mganga nikiwa nimechoka na kutokwa na jasho chapachapa.
Toka nilipouachia mwili nilikuwa mzembe, safari ya nusu saa ilikuwa kama nimetembea zaidi ya saa sita. Tulipofika kwanza nilikaa chini kupumua, kwani hata kuongea nilishindwa kutokana na kifua kujaa pumzi.
Mtoto wa mzee Kidereko aliniacha nimepumzika kwenye gogo la mnazi na yeye kuingia ndani kwa mganga. Ilionesha pale ni mwenyeji kwa jinsi walivyompokea.
Nilitulia kwenye gogo huku giza likianza kuimeza nuru ya mchana. Baada ya muda alirudi na kunieleza jambo ambalo lilinishtua kidogo.
Ndugu yangu tumefeli.
Una maana gani?
Mzee amekwenda mkoani, kuna watu wamemchukua jana.
Atarudi lini?
Mmh! Haijulikani.
Kwani ndiyo mara yake ya kwanza kusafiri kikazi?
Mara nyingi, huwa akiondoka kwenda kufanya kazi za watu mikoani, anaweza kumaliza hata mwezi mzima.
Mmh! Sasa itakuwaje, hana msaidizi?
Yupo, lakini kazi yako si ya kutumwa mtu mwepesi, unaweza kumpoteza kama mchezo.
Kwani ni nzito sana?
Hauna tofauti na uliyosababisha ugonjwa kwa baba uliopelekea mauti yake.
Mmh! Sasa nitafanyaje, hakuna waganga wengine?
Kwa kweli mimi niliyekuleta kwake ndiye niliyekuwa naye karibu pia nina mahusiano mazuri. Hata kazi zao walikuwa wakisaidiana na marehemu baba.
Uliniambia uchawi wao ni wa ndizi, kwa hiyo kuna mkungu unaendelea kuiva?
Ndiyo, tena uchawi huu ni mbaya sana, unaweza kumaliza ukoo wako kwa muda mfupi.
Mungu wangu sasa nitafanya nini ikiwa hakuna mtu wa kunisaidia? nilijikuta nazidi kuchanganyikiwa.
Mmh! Hebu turudi nyumbani nataka nikajaribu kutafuta ufumbuzi, mtoto wa mzee Kidereko aliniambia.
Ukishindwa?
Tumuombe Mungu nisishindwe, shida yangu ni kuzuia, kwani ukifanya mzaha wiki nzima unaweza kuzika familia nzima.
Eti? Kauli ile ilizidi kunitisha.
Uchawi waliotumia ni mbaya sana, ule haubakizi ukoo.
Tukiwa katikati ya mazungumzo alitoka kijana mmoja aliyeonekana amevalia nguo za kiganga na kunisalimia.
Za saizi kaka?
Nzuri.
Pole sana, nimefuatilia mazungumzo yako na maneno aliyoniambia Maghinde kwa kweli yamenishtua. Wakati nyinyi mkizungumza, niliangalia tatizo lako. Kwa kweli ni vita nzito sana.
Jamani badala ya kunisaidia mnazidi kunikata maini, nilitamani kulia na kuiona kama dunia imeniinamia na hakuna wa kunipa msaada.
Itaendelea baadae...........
ILIPOISHIA;
Nilikumbuka siku moja ambayo nina imani katika kusimulia sikulisema hili. Ni kweli siku moja nikiwa kazini baada ya kazi ya kutoa vifaa ambavyo vilikuwa vingi na kunifanya nisimame kwa muda mrefu.
Nilipokaa kichwa kilianza kuniuma kama kinapasuka kikifuatiwa na kutokwa damu nyingi puani. SASA ENDELEA...
Nilikimbizwa hospitali ambako nilikutwa na malaria. Baada ya matibabu nilijisikia vizuri na kuruhusiwa kutoka hospitali. Hali ile haikujirudia tena na kuamini yale yalikuwa malaria tu.
Basi yale hayakuwa malaria ilikuwa ndiyo safari, shukuru kupelekwa kwenye mizimu, uchawi uliofanyiwa mbaya sana. Kutoka damu puani ilikuwa safari isiyo na kwaheri. Lile lilikuwa jini la kutumwa, jini Makata lilikuwa likukate palepale.
Baada ya kuona kwako ngoma nzito walibadilisha mashambulizi na kuyaelekeza kwenye familia yako. Wameanza na baba yako baada ya hapo atatafutwa mtu mwingine.
He! Ina maana wamepanga kuiteketeza familia yangu yote? nilishtuka kusikia vile.
Ndiyo.
Wanatumia uchawi wa ndizi, wanaroga kwenye mkungu wa ndizi wenye ndizi mbichi, ikiiva ndizi moja na kudondoka, basi katika familia yako anaondoka mtu mmoja.
Mungu wangu! nilishika kichwa kwa mshtuko.
Mtego wao haukuwasumbua kukunasa kwa vile kilikuwa kisasi cha kuuawa ndugu yao, hivyo ilikuwa rahisi kukupata.
Sasa utanisaidiaje?
Kazi hii kwa uwezo wangu nzito sana, ila nitakuelekeza kwa mzee mmoja ambaye alikuwa swahiba wa baba, naye yupo vizuri kama mzee Kidereko.
Anakaa wapi?
Maeneo ya mbele kidogo japo kuna kamwendo kadogo.
Tunaweza kwenda leo?
Tunaweza kwa vile muda bado.
Tunaweza kutumia gari?
Hatuwezi kwenda na gari kutokana na eneo lenyewe, lazima tupande kilima na kushuka.
Usiku hakuna wanyama wakali?
Hakuna.
Tulikubaliana kwenda kwa mganga mwingine baada ya ngoma yangu kuwa nzito kwake. Tuliongozana wawili kuelekea kwa mganga, ilikuwa safari ya kupanda na kushuka milima mpaka kufika kwa mganga nikiwa nimechoka na kutokwa na jasho chapachapa.
Toka nilipouachia mwili nilikuwa mzembe, safari ya nusu saa ilikuwa kama nimetembea zaidi ya saa sita. Tulipofika kwanza nilikaa chini kupumua, kwani hata kuongea nilishindwa kutokana na kifua kujaa pumzi.
Mtoto wa mzee Kidereko aliniacha nimepumzika kwenye gogo la mnazi na yeye kuingia ndani kwa mganga. Ilionesha pale ni mwenyeji kwa jinsi walivyompokea.
Nilitulia kwenye gogo huku giza likianza kuimeza nuru ya mchana. Baada ya muda alirudi na kunieleza jambo ambalo lilinishtua kidogo.
Ndugu yangu tumefeli.
Una maana gani?
Mzee amekwenda mkoani, kuna watu wamemchukua jana.
Atarudi lini?
Mmh! Haijulikani.
Kwani ndiyo mara yake ya kwanza kusafiri kikazi?
Mara nyingi, huwa akiondoka kwenda kufanya kazi za watu mikoani, anaweza kumaliza hata mwezi mzima.
Mmh! Sasa itakuwaje, hana msaidizi?
Yupo, lakini kazi yako si ya kutumwa mtu mwepesi, unaweza kumpoteza kama mchezo.
Kwani ni nzito sana?
Hauna tofauti na uliyosababisha ugonjwa kwa baba uliopelekea mauti yake.
Mmh! Sasa nitafanyaje, hakuna waganga wengine?
Kwa kweli mimi niliyekuleta kwake ndiye niliyekuwa naye karibu pia nina mahusiano mazuri. Hata kazi zao walikuwa wakisaidiana na marehemu baba.
Uliniambia uchawi wao ni wa ndizi, kwa hiyo kuna mkungu unaendelea kuiva?
Ndiyo, tena uchawi huu ni mbaya sana, unaweza kumaliza ukoo wako kwa muda mfupi.
Mungu wangu sasa nitafanya nini ikiwa hakuna mtu wa kunisaidia? nilijikuta nazidi kuchanganyikiwa.
Mmh! Hebu turudi nyumbani nataka nikajaribu kutafuta ufumbuzi, mtoto wa mzee Kidereko aliniambia.
Ukishindwa?
Tumuombe Mungu nisishindwe, shida yangu ni kuzuia, kwani ukifanya mzaha wiki nzima unaweza kuzika familia nzima.
Eti? Kauli ile ilizidi kunitisha.
Uchawi waliotumia ni mbaya sana, ule haubakizi ukoo.
Tukiwa katikati ya mazungumzo alitoka kijana mmoja aliyeonekana amevalia nguo za kiganga na kunisalimia.
Za saizi kaka?
Nzuri.
Pole sana, nimefuatilia mazungumzo yako na maneno aliyoniambia Maghinde kwa kweli yamenishtua. Wakati nyinyi mkizungumza, niliangalia tatizo lako. Kwa kweli ni vita nzito sana.
Jamani badala ya kunisaidia mnazidi kunikata maini, nilitamani kulia na kuiona kama dunia imeniinamia na hakuna wa kunipa msaada.
Itaendelea baadae...........