Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 43,037
- 34,742
Katika maisha yangu sikuwahi kuwaza kuua hata nzi kutokana na huruma niliyokuwa nayo.
Watu wengi walipenda kuniita mlokole japo historia yangu yote niliishi maisha ya kutokuwa na dini nikiamini Mungu wa Wakristo ndiye Mungu wa Waislamu kutokana na mafundisho ya dini zote niliyoyafuatilia.
Utashangaa kwa nini niliishi bila kuwa na dini ikiwa wazazi wangu wana dini, tena dini tofauti, baba Muislamu na mama Mkristo. Katika maisha yao hakuna aliyekubali kumfuata mwenzake na kukubaliana, kila mmoja aishi katika imani yake. Hivyo basi, nikawa mtoto wa wazazi wa dini mbili, pamoja na wazazi wangu kuishi kila mmoja na dini yake, waliishi katika upendo wa hali ya juu kwa kila mmoja kuheshimu imani ya mwenzake.
Nilipopata ufahamu nilijikuta nipo njia panda kwa vile sikutaka kumuudhi mmoja wa wazazi wangu kwa kumpendelea mmoja. Halafu kitu cha ajabu nilikuwa mtoto mmoja kama roho, hivyo niliamua kusimama katikati ya wazazi wangu kwa kutochagua dini yoyote. Lakini nilikuwa nafahamu kipi mwanadamu anatakiwa kukifanya ili usimuudhi Mungu.
Katika maisha yangu yote niliamini tofauti ya dini mbili ni ndogo sana lakini anayetakiwa kuabudiwa ni Mungu mmoja. Tokea hapo niliishi nikiwa sina dini na kuishi kama mpagani, tofauti yangu nilikuwa najua Mungu ni mmoja na ndiye anayetakiwa kuabudiwa, lakini sikwenda msikitini wala kanisani na malumbano ya dini hizi mbili mimi yalikuwa hayanihusu.
Wazazi wangu nao walikubaliana na mimi baada ya ushawishi wa kila mmoja kugonga mwamba. Huu ulikuwa muktasari wa maisha yangu ya awali ya kunifanya nisiwe na dini kwa ajili ya mapenzi ya wazazi wangu.
Kutokana na malezi mazuri ya wazazi wangu, niliweza kuishi sehemu yoyote na mtu wa aina yeyote, siku zote heshima na ucheshi ndivyo vilinifanya watu wanipende.
Kama nilivyosema awali, nilikuwa mtu wa huruma na heshima kwa wakubwa na wadogo, lakini mateso ya mapenzi yalinifanya nigeuke niwe na roho mbaya kukiko shetani.
Kuna maelezo niliwahi kusikia wakati nakua kwamba kuna matendo mengine shetani anakimbia akimuona mwanadamu anatenda. Baada ya kuteswa sana na mapenzi ilifikia hatua kutoa roho ya mtu kwangu ilikuwa kitu cha kawaida hata kwa kosa dogo la kuombana msamaha kwa kuamini hakuna kiumbe kibaya duniani kama mwanadamu ambaye hatakiwi kupewa nafasi kwa vile kama ukimchekea basi atakuumiza wewe.
Mkasa wangu unaanzia pale nilipotimiza miaka 21, nilitoka kwa wazazi wangu na kusafiri nje ya mkoa kwenda kufanya kazi baada ya rafiki yangu kupata kazi ya ujenzi.
Hivyo, hakutaka kuondoka peke yake, alinichukua na mimi huku wazazi wangu wakiniasa niishi na watu kwa heshima na taadhima. Nami niliwaahidi wazazi wangu kuwa nitaishi kama walivyonielekeza.
Nilitengana na wazazi wangu kwa mara ya kwanza toka nitoke tumboni kwa mama wangu. Nilifika mkoani na kufikia kwa ndugu wa rafiki yangu. Kwa vile tulifika Jumamosi jioni sana, tulilala na kesho yake tulipumzika na kupata nafasi ya kupelekwa sehemu ya kazi.
Ulikuwa mradi mkubwa sana ambao tuliambiwa utachukua miaka mitano kwisha, siku ile tulipumzika na kesho yake tulikwenda kuanza kazi. Siku ya pili tuliamka asubuhi na mapema na kwenda eneo la ofisi ambapo ndipo mnapangiwa kazi. Ilikuwa kuna tofauti kubwa na vijana wengi tuliowakuta nje ya geti wakisubiri kuitwa, lakini sisi tulikuwa na mwenyeji, mjomba wa rafiki yangu ambaye alikuwa ndiye msimamizi mkuu wa mradi ule ambao ulikuwa chini ya Wataliano, tuliingia bila kuitwa.
Basi huo ndiyo ukawa mwanzo wa kuanza maisha ya kujitegemea, tulianza kwa kulipwa kwa kutwa kama wenzetu kwa wiki mbili, baada ya hapo tulichaguliwa vijana kama ishirini tuliopewa mkataba na kulipwa kwa mwezi na posho yetu kuongezeka tofauti na wenzetu waliokuwa wakilipatwa kwa kutwa.
Maisha yalikwenda vizuri huku mimi na mwenzangu tukihama kwa ndugu zake na kupanga chumba kimoja na kukaa wawili. Wazazi wangu nao walikula jasho langu kila mwezi kwani niliwatumia robo ya mshahara wangu nao walizidi kuniombea kwa Mungu ili niendelee kupata zaidi.
Siku zilikatika huku nami nikipevuka kiakili na mawazo kufikia hatua ya kuhitaji mwenza. Nyumba tuliyokuwa tumepanga kulikuwa na binti mmoja ambaye Mwenyezi Mungu alimjalia umbile dogo lakini nzuri na sura jamili (nzuri). Binti yule alitokea kunipenda sana kiasi cha kumueleza mama yake angependa aolewe na mimi.
Moja ya njia ya kuonesha ananipenda aliniomba mambo yote ya kike ayafanye yeye kama vile kunipikia chakula cha jioni baada ya kazi, kufua nguo na kusafisha chumba lakini sikumpa nafasi ile kwa kuhofia wazazi wake.
Pamoja na mimi kumpenda sana bado sikumkubalia kutokana na kuwaheshimu sana wazazi wake ambao siku zote walinilea kama mtoto wao.
Siku moja usiku baada ya kutoka kazini, mama mwenye nyumba ambaye ni mama mzazi wa yule binti aliniita kwa kumtumia yule binti. Nami niliitikia wito ule, baada ya kuingia sebuleni kwao, nilikaribisha kwenye kochi lililokuwa karibu na alipokaa mama mwenye nyumba.
Itaendelea baadae kidogo......
Watu wengi walipenda kuniita mlokole japo historia yangu yote niliishi maisha ya kutokuwa na dini nikiamini Mungu wa Wakristo ndiye Mungu wa Waislamu kutokana na mafundisho ya dini zote niliyoyafuatilia.
Utashangaa kwa nini niliishi bila kuwa na dini ikiwa wazazi wangu wana dini, tena dini tofauti, baba Muislamu na mama Mkristo. Katika maisha yao hakuna aliyekubali kumfuata mwenzake na kukubaliana, kila mmoja aishi katika imani yake. Hivyo basi, nikawa mtoto wa wazazi wa dini mbili, pamoja na wazazi wangu kuishi kila mmoja na dini yake, waliishi katika upendo wa hali ya juu kwa kila mmoja kuheshimu imani ya mwenzake.
Nilipopata ufahamu nilijikuta nipo njia panda kwa vile sikutaka kumuudhi mmoja wa wazazi wangu kwa kumpendelea mmoja. Halafu kitu cha ajabu nilikuwa mtoto mmoja kama roho, hivyo niliamua kusimama katikati ya wazazi wangu kwa kutochagua dini yoyote. Lakini nilikuwa nafahamu kipi mwanadamu anatakiwa kukifanya ili usimuudhi Mungu.
Katika maisha yangu yote niliamini tofauti ya dini mbili ni ndogo sana lakini anayetakiwa kuabudiwa ni Mungu mmoja. Tokea hapo niliishi nikiwa sina dini na kuishi kama mpagani, tofauti yangu nilikuwa najua Mungu ni mmoja na ndiye anayetakiwa kuabudiwa, lakini sikwenda msikitini wala kanisani na malumbano ya dini hizi mbili mimi yalikuwa hayanihusu.
Wazazi wangu nao walikubaliana na mimi baada ya ushawishi wa kila mmoja kugonga mwamba. Huu ulikuwa muktasari wa maisha yangu ya awali ya kunifanya nisiwe na dini kwa ajili ya mapenzi ya wazazi wangu.
Kutokana na malezi mazuri ya wazazi wangu, niliweza kuishi sehemu yoyote na mtu wa aina yeyote, siku zote heshima na ucheshi ndivyo vilinifanya watu wanipende.
Kama nilivyosema awali, nilikuwa mtu wa huruma na heshima kwa wakubwa na wadogo, lakini mateso ya mapenzi yalinifanya nigeuke niwe na roho mbaya kukiko shetani.
Kuna maelezo niliwahi kusikia wakati nakua kwamba kuna matendo mengine shetani anakimbia akimuona mwanadamu anatenda. Baada ya kuteswa sana na mapenzi ilifikia hatua kutoa roho ya mtu kwangu ilikuwa kitu cha kawaida hata kwa kosa dogo la kuombana msamaha kwa kuamini hakuna kiumbe kibaya duniani kama mwanadamu ambaye hatakiwi kupewa nafasi kwa vile kama ukimchekea basi atakuumiza wewe.
Mkasa wangu unaanzia pale nilipotimiza miaka 21, nilitoka kwa wazazi wangu na kusafiri nje ya mkoa kwenda kufanya kazi baada ya rafiki yangu kupata kazi ya ujenzi.
Hivyo, hakutaka kuondoka peke yake, alinichukua na mimi huku wazazi wangu wakiniasa niishi na watu kwa heshima na taadhima. Nami niliwaahidi wazazi wangu kuwa nitaishi kama walivyonielekeza.
Nilitengana na wazazi wangu kwa mara ya kwanza toka nitoke tumboni kwa mama wangu. Nilifika mkoani na kufikia kwa ndugu wa rafiki yangu. Kwa vile tulifika Jumamosi jioni sana, tulilala na kesho yake tulipumzika na kupata nafasi ya kupelekwa sehemu ya kazi.
Ulikuwa mradi mkubwa sana ambao tuliambiwa utachukua miaka mitano kwisha, siku ile tulipumzika na kesho yake tulikwenda kuanza kazi. Siku ya pili tuliamka asubuhi na mapema na kwenda eneo la ofisi ambapo ndipo mnapangiwa kazi. Ilikuwa kuna tofauti kubwa na vijana wengi tuliowakuta nje ya geti wakisubiri kuitwa, lakini sisi tulikuwa na mwenyeji, mjomba wa rafiki yangu ambaye alikuwa ndiye msimamizi mkuu wa mradi ule ambao ulikuwa chini ya Wataliano, tuliingia bila kuitwa.
Basi huo ndiyo ukawa mwanzo wa kuanza maisha ya kujitegemea, tulianza kwa kulipwa kwa kutwa kama wenzetu kwa wiki mbili, baada ya hapo tulichaguliwa vijana kama ishirini tuliopewa mkataba na kulipwa kwa mwezi na posho yetu kuongezeka tofauti na wenzetu waliokuwa wakilipatwa kwa kutwa.
Maisha yalikwenda vizuri huku mimi na mwenzangu tukihama kwa ndugu zake na kupanga chumba kimoja na kukaa wawili. Wazazi wangu nao walikula jasho langu kila mwezi kwani niliwatumia robo ya mshahara wangu nao walizidi kuniombea kwa Mungu ili niendelee kupata zaidi.
Siku zilikatika huku nami nikipevuka kiakili na mawazo kufikia hatua ya kuhitaji mwenza. Nyumba tuliyokuwa tumepanga kulikuwa na binti mmoja ambaye Mwenyezi Mungu alimjalia umbile dogo lakini nzuri na sura jamili (nzuri). Binti yule alitokea kunipenda sana kiasi cha kumueleza mama yake angependa aolewe na mimi.
Moja ya njia ya kuonesha ananipenda aliniomba mambo yote ya kike ayafanye yeye kama vile kunipikia chakula cha jioni baada ya kazi, kufua nguo na kusafisha chumba lakini sikumpa nafasi ile kwa kuhofia wazazi wake.
Pamoja na mimi kumpenda sana bado sikumkubalia kutokana na kuwaheshimu sana wazazi wake ambao siku zote walinilea kama mtoto wao.
Siku moja usiku baada ya kutoka kazini, mama mwenye nyumba ambaye ni mama mzazi wa yule binti aliniita kwa kumtumia yule binti. Nami niliitikia wito ule, baada ya kuingia sebuleni kwao, nilikaribisha kwenye kochi lililokuwa karibu na alipokaa mama mwenye nyumba.
Itaendelea baadae kidogo......