Mke wa Profesa Jay afunguka, familia yaomba msaada wa matibabu

John Haramba

JF-Expert Member
Feb 4, 2022
365
1,373
Familia ya msanii wa Bongo Fleva, Joseph Haule ‘Profesa Jay’ imejitokeza hadharani na kuelezea juu ya hali ya kiafya anayopitia staa huyo na kuomba msaada wa matibabu yake.

Jay ambaye pia alikuwa ni Mbunge wa Mikumi, alipoanza kuugua alipelekwa katika hospitali mitaa ya Tegeta, akahamishwa kupelekwa Lugalo na baadaye akahamishiwa Muhimbili ambapo ndipo alipo hadi sasa, lakini baadaye kukawa na ukimya wa taarifa.

Wakizungumza katika mahojiano ya Kituo cha Clouds FM, leo Jumatano, familia hiyo ikiongozwa na mke wa Jay, Grace Mgonjo pamoja na mdogo wa Jay, Black Rhino, wameelezea kuwa Profesa ni mgonjwa na wamekuwa wakitumia gharama kubwa katika matibabu yake bila kufafanua zaidi kuhusu ugonjwa unaomsumbua.

“Wakati tunaanza kuuguza hatukutarajia kama itakuwa serious, tulijua ni kitu cha muda mfupi kisha atapona.

“Jay ni mtu wa watu, sababu ya kuamua kuzungumza hadharani ni kwa kuwa ana mashabiki wengi, tukaona hatumtendei haki, tunaomba watu waungane nasi zaidi tumuingize lwenye maombi yetu ili apone, lakini suala la pesa nalo ni muhimu pia,” alisema Grace.

Baadhi ya wasanii na watu maarufu walipiga simu redioni hapo na kuchangia matibabu akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds FM, Joseph Kusaga ambaye alitoa mchango wa Sh milioni 2.

Walitaja namba na njia wanazoweza kutuma michango ya kusaidia matibabu ya msanii huyo kuwa ni:

MPESA: 0757919192 Joseph Haule,
TiGOPesa: 0715919192 Joseph Haule,
CRDB account no: 0112044845200 Joseph Leonard Haule
 
Tatizo la wasanii wanaishi maisha ya kifahari sana na kuwaona raia wa kawaida kama kinyesi ila wakiumwa haraka sana wanatembeza bakuli tuwachangie.
Tenda Wema uendezako usingoje kurudishiwa..., Anyway binafsi mimi hata michango yenye masimango au masharti huwa naona bora mtu asitoe...

Back to the point at hand...., Msanii kama huyu nadhani kwa Taifa / Jamii amelitendea mengi kwa kutoa kazi nzuri ambazo wengi wameburudika (tena kwa piracy wala sio kwa kulipia) hivyo kwangu amekuwa na mchango mkubwa zaidi kuliko tungeonana angenisalimia au hata kuniangalia
 
si waseme tu nini kina msumbua ili tujue na sisi hata tujue tunamuombea je kwa Mwenyezi Mungu.

Anyway ngoja ni change na mimi maana ni Kamanda mwenzangu.
Kikubwa Anaumwa
Huyo hanaga Shida na Mtu
hana Majivuno
Ni mgonjwa kama umejaaliwa Msaidie
kama Huna Usikatishe Tamaa Wengine
sio kila Ugonjwa lazima Uwekwe wazi
Jua Anaumwa na nikweli Mgonjwa
 
Tatizo la wasanii wanaishi maisha ya kifahari sana na kuwaona raia wa kawaida kama kinyesi ila wakiumwa haraka sana wanatembeza bakuli tuwachangie.
Wacha chuki kuna mwenzio niliona kakoment kweny post ya AY kwamba si mwanae anasoma Feza izo mambo acha kabisa matatizo sio kitoto pro j mpaka wapinzani wanamkubali yaani CCM hana kik za kitoto wala show off za kishamba
 
Back
Top Bottom