FYATU
JF-Expert Member
- Dec 7, 2011
- 5,392
- 4,468
"Hawezi kukufanya chochote bana yule mimi namjua" haya ndio maneno yake anayoyarudiarudia kila mara ninapomsisitizia kuwa siwezi kufanya hivyo...Huyu Dada tuna ukaribu naye kibiashara na sina uhusiano nae wa kimapenzi na wala sitarajii kufanya hivyo.
Mumewe tunafahamiana juujuu tu ila naye ameshajiridhisha kuwa sina hatari yoyote kwa mkewe zaidi ya kazi.
Ingawa Mwana Dada haweki wazi sana ni nini lengo lake la kutaka ionekane hivyo zaidi ya kusema tu anataka ampe jamaa tumbo joto bila kujali madhara gani yanayoweza kunikuta mimi "Muigizaji".
Nikimuuliza anataka nifanye nini husema anataka niwe namrudisha nyumbani kwake usiku na Mumewe ajue kuwa alikuwa na mimi, ingawa yeye atakuwa anamwambia alikuwa na mimi kikazi huku akijua wazi Jamaa atapatwa na jekejeke...na hilo ndio haswa lengo lake.
Ukisikia mtihani ndio huu.
Mumewe tunafahamiana juujuu tu ila naye ameshajiridhisha kuwa sina hatari yoyote kwa mkewe zaidi ya kazi.
Ingawa Mwana Dada haweki wazi sana ni nini lengo lake la kutaka ionekane hivyo zaidi ya kusema tu anataka ampe jamaa tumbo joto bila kujali madhara gani yanayoweza kunikuta mimi "Muigizaji".
Nikimuuliza anataka nifanye nini husema anataka niwe namrudisha nyumbani kwake usiku na Mumewe ajue kuwa alikuwa na mimi, ingawa yeye atakuwa anamwambia alikuwa na mimi kikazi huku akijua wazi Jamaa atapatwa na jekejeke...na hilo ndio haswa lengo lake.
Ukisikia mtihani ndio huu.