TANZIA Mke wa msanii Mrisho Mpoto afariki dunia

TANZIA Mke wa msanii Mrisho Mpoto afariki dunia

.
Msanii maarufu wa muziki wa asili nchini Tanzania, Mrisho Mpoto, amepatwa na msiba mzito baada ya mke wake kufariki dunia mapema leo kufuatia kuugua kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na msanii huyo marehemu alizidiwa ghafla jana na kukimbizwa hospitalini kwa matibabu, lakini jitihada za madaktari hazikuweza kuokoa uhai wake.

Taarifa hiyo ameishia Mrisho Mpoto mwenyewe akiandika 👉"Ngumu kuamini nimefiwa na Mke wangu".

#RIP
View attachment 3406814
Kifo ni kifo tu
 
Kifo huongea.. Hutoa taarifa ya mapema❗

"Mke wangu alinipigia simu akaniambia mume wangu naona kama hali sio nzuri presha imepanda, tukamchukua tukampeleka Temeke [Hospitali] akatibiwa vizuri saa nane usiku tukarudi nyumbani...

...akaniambia hivi mume wangu mara ya mwisho mimi na wewe kuoga pamoja ni lini yani tukawa tunataniana utani utani, akaniambia bwana nataka leo uniogeshe, si unajua mke wako mgonjwa bwana siwezi kuoga mwenyewe nipeleke ukaniogeshe...

...basi nikaenda kwenye jakuzi nikajaza maji nikamwambia twende nikamuogesha vizuri saa nane usiku hiyo tukalala, akaniambia nikumbatie tukakumbatiana tukashikana mikono tukapitiwa na usingizi wote." Mrisho Mpoto akizungumzia kifo cha mkewe kilichotokea Julai 15, 2025.
1752729828672.jpg
 
Back
Top Bottom