Mke kazidi mizaha

Mke kazidi mizaha

duuu asa km ulivo hapo pichani mwakwetu ntaanzia wapi mie kukuudhi???......ukiona nimekujibu shit! Ujue najifanya tu...ukisema tu naondoka roho ni pwaa.tumbo la kuhara.....unatikisa na mie natikisa huku lkn ke mnatuweza sana.
Hizi ni picha tuu mkuu. Ila hata hyo pichani anapigwa matukio ya kutosha
 
Mkuu nadhani wewe ndo mwenye matatizo! Sasa kwa mfano hapo ulichokasirika mpaka kwenda kukaa barazani ni nini?
Mbona unacomplicate sana maisha? Kwa kweli kama mambo kama haya ndo ulienda kushtaki ukweni hakika walikushangaa sana!
 
Nawasalimu.

Mnisamehe kwa kutokuwa mwandishi mzuri.

Moja kwa moja kwenye hoja ya msingi.

Nimeishi kwenye ndoa na huyu mke wangu kwa miaka 10 na kujaliwa watoto wawili.

Kilichonifanya nije hapa kuomba msaada wa mawazo ni hili tatizo la mizaha ya huyu mke wangu, amekuwa mtu wa kujibu au kuongea bila ya kuweka mipaka (kutenganisha kipi Cha kuongea na mpenzi na kipi Cha kuzungumza na mume ambaye ni mkuu wa kaya).

Nikiri ya kuwa katika maisha yetu yote nilishawahi mchapa makofi mara 3 kitu ambacho sitaki kukikumbuka na sitaki kitokee tena, ila nilifanya vile Ili tuu aweze kutambua kuwa sipendezwi na tabia zake.

Tabia hiyo ya kutokuwa na mipaka hasa ya kuzungumza haijawahi kwisha zaidi ya kupungua kwa muda na baadae kuanza tena.

Nimewahi kutumia kanuni ya kumtoa out na kwenda naye sehemu ya faragha na kumuambia kuhusu kutopendezwa na tabia zake huwa anaomba msamaha lakini baada ya muda hurudia tena.

Kiukweli ninampenda sana mke wangu, na mahusiano yetu yalianza tangu tukiwa secondary na baadae kuja kuoana.

Nje ya kumkanya mara kwa mara, niliona ni busara kufikisha jambo hili kwao, Ili waweze kumkanya binti yao, ila sikuona mabadaliko yoyote yale.

Yote yaliyotendeka niliweza kuvumilia ila hili nililolipata wiki hii, limenizidi uwezo. Baada ya chakula Cha jioni tukaingia chumbani, alikuwa anapanga nguo Mimi nikatangulia kuoga, baada ya muda nikatoka yeye akiwa Bado busy, kama kawaida kabla ya kulala ni kumshukuru Mungu kwa ulinzi wake wa siku, nikasikia akiseme acha kusali uongo.

Niliumia sana, nikamaaliza sala na kumuuliza ulikuwa unamaana gani, nikaona anacheka, nikamuuliza hii midhaha yako itaisha lini lakini akawa anaendelea kucheka, kwa kweri nilipatwa na hasira sana ila niliishia kutoka kwenda barazani ningeendelea kuwa pale ningeweza kumpiga kitu ambacho sitaki kitokee tena.

Mimi nimemzidi miaka 4 huyu mke wangu, hata kielimu nimemzidi, kisalary nimemzidi zaidi ya mara 4.

Nimeandika hivi Ili kutoa Ile dhana ya kuwa huenda nalelewa, nafanya majukumu yangu kama baba vizuri kabisa(ada, matibu, mavazi, afya, makazi) kwake na kwa watoto wetu.

Kutokana na hili huwa nakuwa na mawazo sana, kitu ambacho natamani kufanya maamuzi magumu ya kumwacha ila moyo unasita.

Ushauri wenu utaniponya.
Mmeshaishi miaka 10, nafikiri mnajuana vya kutosha. Kama ni mzaha, nafikiri kweli ana mzaha, kama hukumjua tangu mkiwa shule, hiyo imekula kwako. Endeleeni kuishi na kulea watoto wenu, rekebishaneni kwa upole. Ila kwa wengine, huo mfano uliotoa, si sababu na wala si tatizo la kupelekea kumuacha mke. Kama unahitaji mapumziko kidogo, jipe muda uende Kijijini au sehemu tofauti update kubadili mazingira, na maisha yaendelee.
 
Kwanza utasalije peke yako mkuu yeye akiwa anapanga nguo?

Japo kilichofanyika (utani) kwangu siyo issue lakini inaonyesha kuna vitu wewe mwenyewe umeviendekeza.
Hili neno! Familia huomba, husali pamoja, sio na mke tu, bali hata na watoto.
Nafikiri kujikweza, na dharau za jamaa ndio tatizo.
Mambo ya elimu, kipato si kigezo cha kutaka usujudiwe na mkeo. Mkeo ni mwema tu, ila kama unataka umtafutie sababu hivi! Utakuja juta!
 
Nawasalimu.

Mnisamehe kwa kutokuwa mwandishi mzuri.

Moja kwa moja kwenye hoja ya msingi.

Nimeishi kwenye ndoa na huyu mke wangu kwa miaka 10 na kujaliwa watoto wawili.

Kilichonifanya nije hapa kuomba msaada wa mawazo ni hili tatizo la mizaha ya huyu mke wangu, amekuwa mtu wa kujibu au kuongea bila ya kuweka mipaka (kutenganisha kipi Cha kuongea na mpenzi na kipi Cha kuzungumza na mume ambaye ni mkuu wa kaya).

Nikiri ya kuwa katika maisha yetu yote nilishawahi mchapa makofi mara 3 kitu ambacho sitaki kukikumbuka na sitaki kitokee tena, ila nilifanya vile Ili tuu aweze kutambua kuwa sipendezwi na tabia zake.

Tabia hiyo ya kutokuwa na mipaka hasa ya kuzungumza haijawahi kwisha zaidi ya kupungua kwa muda na baadae kuanza tena.

Nimewahi kutumia kanuni ya kumtoa out na kwenda naye sehemu ya faragha na kumuambia kuhusu kutopendezwa na tabia zake huwa anaomba msamaha lakini baada ya muda hurudia tena.

Kiukweli ninampenda sana mke wangu, na mahusiano yetu yalianza tangu tukiwa secondary na baadae kuja kuoana.

Nje ya kumkanya mara kwa mara, niliona ni busara kufikisha jambo hili kwao, Ili waweze kumkanya binti yao, ila sikuona mabadaliko yoyote yale.

Yote yaliyotendeka niliweza kuvumilia ila hili nililolipata wiki hii, limenizidi uwezo. Baada ya chakula Cha jioni tukaingia chumbani, alikuwa anapanga nguo Mimi nikatangulia kuoga, baada ya muda nikatoka yeye akiwa Bado busy, kama kawaida kabla ya kulala ni kumshukuru Mungu kwa ulinzi wake wa siku, nikasikia akiseme acha kusali uongo.

Niliumia sana, nikamaaliza sala na kumuuliza ulikuwa unamaana gani, nikaona anacheka, nikamuuliza hii midhaha yako itaisha lini lakini akawa anaendelea kucheka, kwa kweri nilipatwa na hasira sana ila niliishia kutoka kwenda barazani ningeendelea kuwa pale ningeweza kumpiga kitu ambacho sitaki kitokee tena.

Mimi nimemzidi miaka 4 huyu mke wangu, hata kielimu nimemzidi, kisalary nimemzidi zaidi ya mara 4.

Nimeandika hivi Ili kutoa Ile dhana ya kuwa huenda nalelewa, nafanya majukumu yangu kama baba vizuri kabisa(ada, matibu, mavazi, afya, makazi) kwake na kwa watoto wetu.

Kutokana na hili huwa nakuwa na mawazo sana, kitu ambacho natamani kufanya maamuzi magumu ya kumwacha ila moyo unasita.

Ushauri wenu utaniponya.
Huyo Ni mtu wa mizaa,sioni Kama Kuna tatizo mkuu,

ndio mapenzi yalivyo sometimes lazima mtaniane kidogo!
 
Mkuu nadhani wewe ndo mwenye matatizo! Sasa kwa mfano hapo ulichokasirika mpaka kwenda kukaa barazani ni nini?
Mbona unacomplicate sana maisha? Kwa kweli kama mambo kama haya ndo ulienda kushtaki ukweni hakika walikushangaa sana!
Jamaa inaonekana Ni mtu wakupenda kususa Susa, na mwanamke kamshajua
 
Tatizo sio mke wako tatizo ni wewe kushindwa kumatch na sense of humor ya mkeo. Mkeo ni mcheshi sana af we unaonekana upo serious mkuu.
 
Utani Hadi kwenye Sala?! Anyway.. nenda naye taratibu. Mwanamke anapaswa kulelewa hata Kama Ana miaka 80. Hata Kama mna miaka 10 pamoja Ukileta ubabe atakuacha amtafute anayependa utani.
Hapo kwenye sala akikutania unacheka unamwambia acha bas masihara mi nasali, na ye atacheka af mambo yanaisha hivyo.
 
Asante kwa ushauri kaka, ila inaumiza kichwa sana.

Kwa mfano kuna siku tulikuwa ibadani, kuna mzee wa kanisa alimuita kwa jina langu la ukoo, alimkatalia kuwa haitwi hivyo Bali akataja jina la ukoo wao, mke ambaye nimemuoa kwa ndoa tena kwa Mali kamili bila ya deni.

Yule mzee alikaa kimya na hakuongea tena, inaumiza sana.
Duuuh basi amekuzoea kama chupi chupili huyoo

Sema kiboko ya mwanamke na mwanamke mwenzie...nadhan umenielewa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom