Mke kazidi mizaha

Mke kazidi mizaha

Shida inaanzia hapo wewe kutompiga japovibao kadhaa. Kuna watu mpaka nguvu itumike ndio wanaelewa. Mwanamke kuna muda mwenyewe anamiss kupigwa, usimnyime kibao mke wako
Nilishawahi kufanya hivyo, ila nilijisikia vibaya sana, sitaki nirudie tena kumpiga
 
Acha kumpiga mkeo kwanza, ila pia mbona ni jambo la kawaida??? kwani Dini mnatofautiana au ni moja?? pale alipokuambia unasali uongo ungemuuliza kwanini kiutaratibu angekujuza inawezekana kuna jambo umefanya ila wewe umetoka umeenda kukaa barazani ndio tatizo kwa madai umesusa, ila waswahili husema ukisusa wenzio wala

Acha kumnunia mkeo kwa mambo madogo sana, kwanza miaka 10 kwenye ndoa hujakubali kumzoea mtu kweli??? jaribu kukubali kua hilo ndio dhaifu lake hivyo mbebee kama mkeo songa mbele..........
Angenisubiri kwanza nimalize afu aseme ni uongo wala nisingeumia ila nipo katikati ya ibada mtu anasema nasali uongo.

Sisi wote ni wa dini moja
 
Kuna wanawake wanapenda shari shari, inatokea tu anataka kuanzisha kaugomvi pasipo sababu ya msingi, na anasikia raha kufanya hivyo, inawezekana wako ni mmoja wa hilo kundi.
Mtu wa namna hii nafanyaje kumdhibiti?
 
Kwenye somo la Psychology kuna mada ya Peronality.
Ingia kwenye hiyo mada google ubainishe aina kadha,hasa zinazolandana na tabia ya mkeo,uone kama vinarekebishika au jinsi ya kwendana navyo.
Vinginevyo utaumiza akili yako/utatoa maamuzi yatakayo kugharimu wewe binafsi.
Asante sana kwa wazo zuri, nitafuatilia
 
Either unachepuka au yeye anahisi hivyo, anafahamu au anzihisi dhambi zako na anafahamu au anshisi unaziendeleza, hivyo anakwambia acha kumdhihaki Mungu.
Inawezekana, ila sichepuki, ila kwa hii tabia yake huenda nikafikiria.
 
Nawasalimu.

Mnisamehe kwa kutokuwa mwandishi mzuri.

Moja kwa moja kwenye hoja ya msingi.

Nimeishi kwenye ndoa na huyu mke wangu kwa miaka 10 na kujaliwa watoto wawili.

Kilichonifanya nije hapa kuomba msaada wa mawazo ni hili tatizo la midhaha ya huyu mke wangu, amekuwa mtu wa kujibu au kuongea bila ya kuweka mipaka ( kutenganisha kipi Cha kuongea na mpenzi na kipi Cha kuzungumza na mume ambaye ni mkuu wa kaya).

Ni kili ya kuwa katika maisha yetu yote nilishawahi mchapa makofi mara 3 kitu ambacho sitaki kukikumbuka na sitaki kitokee tena, ila nilifanya vile Ili tuu aweze kutambua kuwa sipendezwi na tabia zake.

Tabia hiyo ya kutokuwa na mipaka hasa ya kuzungumza haijawahi kwisha zaidi ya kupungua kwa muda na baadae kuanza tena.

Nimewahi kutumia kanuni ya kumtoa out na kwenda naye sehemu ya faragha na kumuambia kuhusu kutopendezwa na tabia zake huwa anaomba msamaha lakini baada ya muda hurudia tena.

Kiukweri ninampenda sana mke wangu, na mahusiano yetu yalianza tangu tukiwa secondary na baadae kuja kuoana.

Nje ya kumkanya mara kwa mara, niliona ni busara kufikisha jambo hili kwao, Ili waweze kumkanya binti yao, ila sikuona mabadariko yoyote yale.

Yote yaliyotendeka niliweza kuvumilia ila hili nililolipata wiki hii, limenizidi uwezo. Baada ya chakula Cha jioni tukaingia chumbani, alikuwa anapanga nguo Mimi nikatangulia kuoga, baada ya muda nikatoka yeye akiwa Bado busy, kama kawaida kabla ya kulala ni kumshukuru Mungu kwa ulinzi wake wa siku, nikasikia akiseme acha kusali uongo.

Niliumia sana, nikamaaliza sala na kumuuliza ulikuwa unamaana gani, nikaona anacheka, nikamuuliza hii midhaha yako itaisha lini lakini akawa anaendelea kucheka, kwa kweri nilipatwa na hasira sana ila niliishia kutoka kwenda barazani ningeendelea kuwa pale ningeweza kumpiga kitu ambacho sitaki kitokee tena.

Mimi nimemzidi miaka 4 huyu mke wangu , hata kielimu nimemzidi, kisalary nimemzidi zaidi ya mara 4. Nimeandika hivi Ili kutoa Ile dhana ya kuwa huenda nalelewa, nafanya majukumu yangu kama baba vizuri kabisa( ada, matibu, mavazi, afya, makazi) kwake na kwa watoto wetu.

Kutokana na hili huwa nakuwa na mawazo sana, kitu ambacho natamani kufanya maamuzi magumu ya kumwacha ila moyo unasita.

Ushauri wenu utaniponya.
Tunakusamehe kwa kutokuwa mwandishi mzuri.

Hakuna neno MIDHAHA bali tumia neno MIZAHA au MZAHA


Kuhusu mkeo, yupo poa ila shida ni malezi ya kwao. Muombee kwa Mungu kisha usimfuatilie hayo anayojibu maana kuna shetani kasimama kwenye kizingiti cha mlango na unapaswa kumshinda
 
Nakuelewa Sana mtoa mada Mimi ilinikuta hio kidogo niue toto la mtu..now sitaki Tena Ndoa kwa sababu ya mdomomdomo wa wanawake na dharau.kila siku ananipigia simu turudiane sometimes namuonea huruma nikikimbuka mauno yake SI unajua Tena watoto wa pwani huwa hawakosei kitandani hawafanyi makosa kwingine Huku ndo hivo dharau...anyway nakushauri wako mna muda mrefu na familia hivo usimuache endelea kuongea naye...me wangu hatukufunga ndoa na pia hatukuwa na mtoto so ni rahisi kumtema kucheki changamoto nyingine...all in all wanawake wanafanana tabia
Asante kwa ushauri kaka, ila inaumiza kichwa sana.

Kwa mfano kuna siku tulikuwa ibadani, kuna mzee wa kanisa alimuita kwa jina langu la ukoo, alimkatalia kuwa haitwi hivyo Bali akataja jina la ukoo wao, mke ambaye nimemuoa kwa ndoa tena kwa Mali kamili bila ya deni.

Yule mzee alikaa kimya na hakuongea tena, inaumiza sana.
 
Kusema kweli we ndo mwenye matatizo asee. We unataka kuishi kama mko Kambi ya jeshi? Shida unapimia kumzidi elimu na mshahara unataka akusujudie

Hapo baada ya kumaliza kusali wakati ye anapanga Nguo kabatini ungeenda kumkumbatia Kwa nyuma ukamuuliza na kumwambia unasemaje wewe? Subiri adhabu Yako kitandani ukimaliza kupanga Nguo, najua alikuwa na kanga Moja tu hapo

Ishi na mkeo kama Mshkaji wako bloo ufurahie maisha
Hahahahahaha , asante sana, nitajaribu siku nyingine, huenda ikaponya ndoa yangu.
 
Huyo mke hana mzaha bali ni mkorofi tu kuna wanawake wanapenda attention zetu kupitia ukorofi ukikasirika yeye ndio anaona raha atleast ume respond kwa feelings zake. Sasa sio wote tunamudu huo ujinga!

Cha msingi mkomeshe kitandani umkaze kweli kweli kisha umwambie ukileta uchizi nakuongeza tena ... Hio ndio adhabu nzuri na itakurahisishia kujua wakati ana mood ya kutafunwa.
Hahahahahahahaha, itabidi niongeze dozi
 
Ongeza mtoto wa tatu mkuu,huyo dada hana tatizo,tatizo unalo wewe unacomplicate vitu vidogo vidogo..kiufupi una ghubu,tafta mtaalamu wa saikolojia atakusaidia
Tunamtarajia kijana mwingine muda sio mrefu.
 
Kama nimekuelewa vizur huyo mwanamke ana changamoto zake kadhaa...pamoja na kumtoa out kiume na kuongelea changamoto zenu faragha ...umesema anaomba msamaha kisha baadae anarudia tena.....umesema ameshaitwa kwao na kusemwa lkn bado Tu....naona chukulia huo ni kama udhaifu wake Tu.... Na hio wala sio sababu ya kumwacha huyo mkeo.

Ila hili la kuleta mdhaha ktk sala linasikitisha Sana na ulikuwa na haki ya kukasirika....huo sio utani Bali upumbavu ambao ameuonyesha mkeo.

Watu wamekusema Sana labda hujui utani na mambo kama hayo....lkn najua wewe ni mwanaume na sio mvulana....Kwa maana unajua huu sasa ni utani na huu ni mdhaha...siamini kama wewe ni mpumbavu kiasi kwamba ushindwe kujua utani na mdhaha....tatizo la mkeo ni kwamba Hana Busara hiyo ndio shida yake ndio maana analeta utani mpaka kwenye sala! Na Busara ni kuliweka jambo ktk mahala pake.....mkeo Hana Hilo.

Jitahidi kumuweka Sawa Kwa hekima Sana....Kwa mfano ukipita Mda Fulani Bila kukuletea mdhaha ebu mnunulie zawadi au mpe hela akajinunulie zawadi na mwambie kipenz huwa nafurahi Sana pale unapoacha mdhaha unanifanya nizidi kukupenda ebu kajinunulie chochote unachopenda.....jaribu kuangalia kama mbinu hii itafanya kazi.

Kuna utani na mdhaha....mdhaha sio utani unakera na ni kama dharau Fulani hivi.

Ila usifikirie kumuacha hata kidogo....hayo ni ya kawaida tofauti na usaliti
Nimelichukua hili, nitalifanyia kazi. Asante sana kwa muda wako, kwa kweri umeniongezea kitu
 
Mzaha hadi kwenye sala..hapana nakataaa.
Jamani tuwe wakweli
Hiyo ni mbaya zaidi.
Ila pia watu hawafanani
Kuna watu wako hivyo yaani ndobyo walivyo
Wewe hapo unatamani ungekua na mwanamke siriaz flan hivi
Ila mpaka mnaoana hukuona hayo yote?au alikua anaficha?
Sawa ushamuoa na hilo jambo unaona linakukera mpaka mwisho
Ongea nae tu kila mara maana ndo mshaoana tena.hamna namna.
Hakuwahi kufanya anachofanya kifanya, ndio maana nikawa mwepesi kufunga naye ndoa
 
Wewe jamaa sijui unatokea Mkoa gani,sasa kama mke hakufanya utani na wewe afanye na nani,?..

Huyo mkeo ana mapenzi ya dhati na wewe,anakupenda sana na ndio maana anafanya mzaha na wewe..

Ati umekasirishwa kwasababu mke kakwambia unasali uongo!!!hicho sio kitu cha kukasirika

ungelimjibu nasali ili nizidi kukupenda mke wangu,ili upendo wetu uwe wa milele wa kufa na kuzikana..

Wanawake wa Kitanzania wanalalamika sana kuhusu wanaume zao kuwa hawana mapenzi,hawako romantic,wanaume wenyewe ndio kama wewe..

Kaka hii dunia nyengine kuwa humble kwa mke wako,elimu na kipato chako weka pembeni unapokuwa nyumbani na mkeo

Mke wako hana matatizo,matatizo unayo wewe,jirekebishe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom