Mke kagoma kujiita jina la Mumewe, mume afanyeje?

Ni jirani zangu na nimeisha wasuluhisha sana lakini kila upande unadai uko sahihi..
Jamaa kaoa mwaka watano huu lakini mkewe ambaye ni mfanyakazi serikalini amekataa kutumia jina la mumewe kama ilivyo zoeleka kwa kina mama wengi wakiolewa. K.m vile Mama maria Nyrere, Magret Sitta,Hilary Clinton, Lwiza Mbutu n.k
Yaani Mrs kang'ang'nia tu kutumia jina la baba yake kitendo ambacho mume kinamuumiza mno! na anaona mkewe anampuuza eti kwa vile hana hadhi kubwa kama baba wa mke.
Jamani hii inakuwaje ni lazima mke abadili jina akiolewa na kujiita jina la mumewe?
Hii kali sasa! Kutumia jina la mume ni uamuzi wa mtu, ni makubaliano. Mke aweza kulitumia au anaweza kubaki na jina la ukoo wake, wala hakna shida. Sasa mwanaume analalamikia nini? Aridhike na penzi analoewa, na maelewano waliyo nayo kati yao. Ndomambo ya maana. Haya ya majina ni mambo ya kigeni tu. Tangu zamani wamama wa kiafrika hata baada ya kuolewa wameendelea kutumia majina yao ya usichana.
 
Jamani hii inakuwaje ni lazima mke abadili jina akiolewa na kujiita jina la mumewe?

Inaelekea huyo mwanamke hataki/hapendi kujibainisha na ukoo wa mumewe. Sasa kama mtu hataki/hapendi jina fulani (kwa sababu yoyote ile), kwa nini umlazimishe?

Lakini kuna nyakati mambo haya ya majina yanaweza kuleta confusion pale ambapo mwanamke ambaye atataka kujibainisha kuwa kaolewa na hapohapo bado anatumia jina la ukoo wao (baba yake). Kama kwa mfano anitwa Anna Temu na ameolewa na Peter Mosha. Akijitambulisha/andika jina lake hivi: Anna Temu (Mrs) au Mrs Anna Temu haitaleta maana anayokusudia.

But generally, sioni kama issue ya jina inapaswa kuleta ugomvi ndani ya nyumba!
 
Imenifurahisha sana hii.. Nimedunga SENKSI Mkuu..


Huyu mke anajua akitumia jina la baba labda linamsaidia katika mihangaiko yake, si ana jina kubwa? Jina la baba yake linalipa kuliko la jamaa yako.
Anatakia aelewe kwamba mkewe yupo kikazi zaidi!
Kwa mfano uoe mke mwenye surname ya Nyerere halafu abadilishe na kutumia Mkude? Sidhani. Jamaa aelewe tu au apandishe jina lake chati
 
whats so important? kwani huyo mume anaumia nini? aah, mambo mengine bwana, just to think that they bring tensions to a marriages makes me sick.
 
halafu mnajiuliza nyumba ndogo zinaanziaga wapi!!!!!! watu kama hawa amani nyumban sifuri, akipata wa kumpa amani huko nje kwa nini asibobee huko???.................. jamani tieni akili vichwani.............
 
Huyu mke anajua akitumia jina la baba labda linamsaidia katika mihangaiko yake, si ana jina kubwa? Jina la baba yake linalipa kuliko la jamaa yako.
Anatakia aelewe kwamba mkewe yupo kikazi zaidi!
Kwa mfano uoe mke mwenye surname ya Nyerere halafu abadilishe na kutumia Mkude? Sidhani. Jamaa aelewe tu au apandishe jina lake chati

Hahahahaaaaa! mkuu...Mkude!....
Lakini mbona Sauda Kilumanga mtoto wa Idd Simba kachanganya? anatumia la Mumewe na Baba yake...nadhani aliona angetumia la mumewe pekee watuy wasingemjua kuwa ni mtoto wa Idd Simba.
 
Hahahahaaaaa! mkuu...Mkude!....
Lakini mbona Sauda Kilumanga mtoto wa Idd Simba kachanganya? anatumia la Mumewe na Baba yake...nadhani aliona angetumia la mumewe pekee watuy wasingemjua kuwa ni mtoto wa Idd Simba.

Aliona noma kumtosa jamaa kimoja, kwa hiyo katumia busara ya kuchanganya majina (ukimwambia achague moja atachagua Simba, nadhani)
 
Hahahahaaaaa! mkuu...Mkude!....
Lakini mbona Sauda Kilumanga mtoto wa Idd Simba kachanganya? anatumia la Mumewe na Baba yake...nadhani aliona angetumia la mumewe pekee watuy wasingemjua kuwa ni mtoto wa Idd Simba.

Anybody can be anybody in this World. Nani alikuwa anamfahamua Barack Obama mika 10 iliyopita? Kwa hiyo hata huyo mumewe anaweza kuja kuwa na jina kubwa zaidi. Mimi ushauri wangu aichukulie hiyo kama chalenji kwenye maisha yake na mafanikio yake binafsi!

Sio lazima siasa, anaweza kutengeneza jina kwa kuwa mfanyabiashara mkubwa au vinginevyo! La sivyo watoto wake nao mama yao atawambukiza ugonjwa wa jina kubwa na babu yao mzaa mama, wakiwa wakubwa watataka kutumia hilo badala ya la baba yao! Mambo mengine siyo ya kuyachukulia kimzaha mzaha!
 
Aliona noma kumtosa jamaa kimoja, kwa hiyo katumia busara ya kuchanganya majina (ukimwambia achague moja atachagua Simba, nadhani)

Duh, kama ni hivyo wanaume tutafute "uwezo" jamani, lasivyo unaweza kupuuzwa ukakosa raha ya dunia.
 
Nimeoa.
sioni tatizo mke wangu kutumia ubini aupendao yeye wala sina haki ya kumlazimisha.

Hizi taratibu za kubadili ubini huleta matatizo sana wakati wa mirathi endapo mume atatangulia kufariki. na hata ktk masuala ya kazi ofisi za serikali huwa na utata wake endapo utabadili ubini wako pasina kuapa mahakamani.

Mwache aitwe kwa jina la baba yake kwani ni heshima na asilazimishwe kubadili wala usijifili sori fo dhati
 
Mwambie jamaa agombenia urais na mungu akimsaidia apate utaona ,wife wake atataka kubadili jina
Hiyo ni jeuri ya wadada wetu wa siku hizi na kiasi kikubwa inatokana na maporomoko ya mila na desturi,unajua siku hizi ukioa mwanamke mko sawa kielimu kama wote ni Graduates usitegemee respects za mume kuzipata ni nadra sana,hata service ambazo baba na babu zetu walikuwa wanapata toka kwa mama na bibi zetu hupati.Siku hizi ni Beijing muda si mrefu watadai wanaume watumie majina ya wake zao.Ukitaka kujua ni jeuri mbona hamna first lady anayekataa kuitwa jina la mumewe? Ikumbukwe mke atamwacha baba na mama yake ataambatana na mumewe,na Adamu akatiwa usingizi akachomolewa ubavu wake ukapuliziwa pumzi ukawa mke,Adamu alipoamka akafurahi akasema huyu sasa ni nyama katika nyama na mfupa ktk mifupa yangu ndiyo akamwita mwanamke......hebu mwanawane Chrispin changia hapo au aya hazipandi?
 
Nimeoa.
sioni tatizo mke wangu kutumia ubini aupendao yeye wala sina haki ya kumlazimisha.

Hizi taratibu za kubadili ubini huleta matatizo sana wakati wa mirathi endapo mume atatangulia kufariki. na hata ktk masuala ya kazi ofisi za serikali huwa na utata wake endapo utabadili ubini wako pasina kuapa mahakamani.

Mwache aitwe kwa jina la baba yake kwani ni heshima na asilazimishwe kubadili wala usijifili sori fo dhati
tuambie na mali ambazo ni za familia itakuwaje?haya majina kiwanja kina jina la mume na gari lina jina la mke kama amekopa yeye,akaunti ina jina la mume,ngoja uone mume atangulie kufariki au hata mke afariki na wawe na ndugu wakorofi wenye njaa uone watakavyokomaa kuwa gari ni ndugu yetu,au nyumba ni ya ndugu yetu angalieni majina ktk hati na kadi,acheni tu haya mambo yafuatwe mtawanyima mirathi ndugu zenu
 
Mila inasemaje? acheni ukisasa jamani, mambo uanza taratibu leo hii watu wanatangaza ndoa za jinsia moja kanisani

what next baada ya kukataa jina la mume wake?
 
halafu mnajiuliza nyumba ndogo zinaanziaga wapi!!!!!! watu kama hawa amani nyumban sifuri, akipata wa kumpa amani huko nje kwa nini asibobee huko???.................. jamani tieni akili vichwani.............

we waache mtu wangu!
 
Wanao badili majina wanamatatizo gani kama siyo muhimu, au nini kinacho wafanya wabadili?

Hii imekaa kiutamaduni na mazoea zaidi so far hakuna ulazima wa kubadili jina na kufanya kuwa la mume hata kwa watoto pia kuna baadhi ya sehemu wankuwa na majina tofauti kabisa yaani hayafanani na baba kabisa
 
.......Hili jambo la kubadili jina baada ya kuolewa kwa sisi wadada ni issue kubwa sana siku hizi, wadada wengi hatupendi kubadili majina yetu.........hata mie mwenyewe nilikuwa nakataa kubadili jina langu, maana vyeti vyangu vya shule vyote vipo kwa jina la baba yangu, halafu leo tena nibadili niliona kama haitaleta maana.

Baada ya Mr kulalamika sana kwa nini sibadili jina, niliamua kubadili tu ili nimridhishe.......hivyo natumia majina yangu kama ilivyokuwa yaani jina la ukoo wangu halafu mwishoni ndio naongeza jina la kwake.

Hii kitu haina umuhimu sana, ila kwa kuwa ndoa ni makubaliano ya watu wawili, na kama mwanaume anataka utumie jina lake, mie naona bora tu utumie ili kulinda amani/ masikilizano yenu ya ndoa.......ukitumia jina la mr wako wala hupungukiwi chochote.
 
.......Hili jambo la kubadili jina baada ya kuolewa kwa sisi wadada ni issue kubwa sana siku hizi, wadada wengi hatupendi kubadili majina yetu.........hata mie mwenyewe nilikuwa nakataa kubadili jina langu, maana vyeti vyangu vya shule vyote vipo kwa jina la baba yangu, halafu leo tena nibadili niliona kama haitaleta maana.

Baada ya Mr kulalamika sana kwa nini sibadili jina, niliamua kubadili tu ili nimridhishe.......hivyo natumia majina yangu kama ilivyokuwa yaani jina la ukoo wangu halafu mwishoni ndio naongeza jina la kwake.

Hii kitu haina umuhimu sana, ila kwa kuwa ndoa ni makubaliano ya watu wawili, na kama mwanaume anataka utumie jina lake, mie naona bora tu utumie ili kulinda amani/ masikilizano yenu ya ndoa.......ukitumia jina la mr wako wala hupungukiwi chochote.

dada prety nashukuru kwa kuliona tatizo linainyemelea nyumba yako na kuchukua hatua kuliepuka kwa faida ya familia nzima............. hongera sana na Mungu akubariki na akuzidishie furaha na amani katika ndoa yako............... umechukua uamuzi wa makusudi kulinda amani na furaha nyumbani kwako hivyo hakika unaistahili amani hiyo na kuraha hiyo................ naam na kubwa kuliko hiyo unastahili............. Mungu ni mwema na hataiacha familia yako........... ubarikiwe sana................


wanawake wengi wapumbavu huvunja nyumba zao wenyewe tena kwa mikon yao wenyewe........... hizo ni mila tu, tena hata wanaume wanpotaka utumie jina lao hawafanyi makosa kwani nao walizikuta hizo mila zipo............. hata sarah alimheshimu ibrahimu akamwita "Bwana"............... angalia jinsi alovyobarikiwa....... sembuse jina tu? je wakiambiwa wawaite waume zao "Bwana" itakuwaje?............
 
Mimi tulikubalina kutofautiana. I never demanded she change her name and she never asked to change. Najiona mtu huru zaidi ikiwa mke wangu hatumii jina langu. Nahisi ni upungufu tu kwa mwanaume kung'ang'ania mkeo abadili na kutumia majina ya ukoo wako.

Ni vizuri kwani ukinunua kitu kwa jina lako ni chako! Naye akinunua kitu kwa jina lake ni chake. Sasa hapa nadhani huwa kuna ka sababu fulani ka kiufundi mahakamani ndo maana wanawake wengi hubadili majina. Sina uhakika sana kwani si mwanasheria. Ila niko huru zaidi mke akitumia la kwake. Simlazimishi kuji identify na ukoo wangu! Na sioni kuwa hilo ni tatizo.

Mshauri huyo mwanaume kuwa tuko wanaume wengi ambao kwanza hatupendi wake zetu watumie majina yetu na tuko happy kabisa na ndoa zinabaki vile vile.
 
Ni jirani zangu na nimeisha wasuluhisha sana lakini kila upande unadai uko sahihi..
Jamaa kaoa mwaka watano huu lakini mkewe ambaye ni mfanyakazi serikalini amekataa kutumia jina la mumewe kama ilivyo zoeleka kwa kina mama wengi wakiolewa. K.m vile Mama maria Nyrere, Magret Sitta,Hilary Clinton, Lwiza Mbutu n.k
Yaani Mrs kang'ang'nia tu kutumia jina la baba yake kitendo ambacho mume kinamuumiza mno! na anaona mkewe anampuuza eti kwa vile hana hadhi kubwa kama baba wa mke.
Jamani hii inakuwaje ni lazima mke abadili jina akiolewa na kujiita jina la mumewe?

Issue ya kubadili jina au kutobadili jina imekaa kidini zaidi. Kwa wanao fuata imani ya Kiislamu Uislam umekataza kubadilisha jina la baba na kutumia jina lolote jengine kama kutumia jina la mume.

Waiteni kwa baba zao, maana huo ndio uadilifu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu
Al-Ahzaab: 5

Na tabia ya mke kubadilisha jina kutumia jina la mume, mfano kuitwa Mrs Juma, ni tabia zisizolingana na maadili na mafundisho ya Kiislam kabisa!

Kufanya hivyo vile vile kuna madhara yake. Kwanza tabu ya kubadiisha pasipoti na vyeti vinginevyo kwa ajili ya utambulisho katika idara za serikali.

Pili, inapotokea kifo cha mume au talaka, inabidi mke arudie kubadilisha pasipoti na vyeti vyake vyote vingine kuweka jina la baba badala ya jina mume, hivyo ni usumbufu unaompotezea mtu fedha na wakati wake.

Kwa hiyo Muislamu ni bora kubakia katika amri na mafunzo ya dini yake ili kupata ridha ya Mola wake na pia kujiepusha na usumbufu mbali mbali.

Ila kwa wale wanao fuata kanuni za kimila na kikristo na kimagharibi ni jambo lililo zoeleka kwa mke kujiita kwa jina la ukoo wa mume wake.

...akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?
Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe
.
Matt 19:5-6
 
Back
Top Bottom