Mpatanishi na wengine
,Habarini za jioni nimeshindwa kuwataja wote niwieni radhi, sijawahi kumtapeli mtu na sidhani kama nitakuja kumtapeli mtu hata kama shida zitanibana kiasi gani, kuna vitu nimevisoma nimeshangaa sana lakini pia mniwie radhi niliowashangaa kwa comment zenu, nimechelewa kujibu coment zenu maana mpaka niende kwenye internet cafe, kwa wale waliojitoa kunisaidi na kutaka kupata uthibitisho, nikuwa mwaka jana nilifanya mtihani wa QT kidato cha pili kwa jina langu hili halisi Mbaga Michael kwa namba M1791-0019 katika kituo cha Mvumi Mkulu Secondary School Centre, ingia katika tovuti ya Necta tafuta yalipo matokeo ya QT tafuta hicho kituo utaona jina langu, ila kwa mtihani wa kidato cha nne nitajisajili katika shule ya Dodoma Secondary, kwa hivyo sasa wale wanaojaribu kupotosha kuwa sijui niliwatapeli niliwatapeli vipi? sina haja ya kujibizana nao kwa kifupi ndo hivyo, kwa wale mlioko dodoma nipigieni simu yangu hiyo hapo juu ili kupata kile kinachowatatiza ahsanteni sana, nipo dodoma nitafuteni tukutane.