Mkasa wa Idi Amin na Wake Zake

Abtali mwerevu

JF-Expert Member
May 5, 2013
637
432
Na: Mwalimu Makoba

1

Hadithi ya Idi Amin na wake zake ni miongoni mwa hadithi za kusisimua, kuchekesha na zilizojaa ukatili. Kuwa na wake watano na wote wazuri ni msisimko wa aina yake. Kuwa na michepuko thelathini na watoto thelathini na nne (namba ya idadi ya watoto wa Idi Amin haijawahi kuwa sawa, hutofautiana hata katika nyaraka rasmi).

Mke wa kwanza aliitwa Maryamu, mtoto wa mwalimu mkuu, Bwana Kibedi, na dada wa Waziri wa Mambo ya Nje, Wanume Kibedi.

Ingawa alizaa naye watoto kadhaa, hakufunga naye ndoa mpaka ilipofika mwaka 1966, mwaka alioshambulia makazi ya Kabaka na kujizolea umaarufu mkubwa. Kupata watoto bila kufunga ndoa siyo jambo la ajabu Uganda. Idi Amin alilipa mahari, ndoa ikatambulika.

Amin aliishi na mke huyu kwa miaka kumi na tatu. Alikuwa tayari kutafuta mke mdogo kama ilivyo desturi. Alihitaji mke kutoka kabila lake ndipo akampata Kay Adroa. Alimchagua Kay kwa sababu alikuwa msomi kutoka chuo Kikuu cha Makerere, mrembo, mpole na aliyekuwa na aliyekamilika kila idara.

Amin aliifahamu familia ya Kay vizuri. Hata mwaka 1966, bunge lilipoomba kusimamishwa kazi kwa Idi Amin kwa sababu ya tuhuma za wizi wa dhahabu, alikwenda mafichoni na Kay. Kay alikuwa mkiristo kama Malyam. Ndoa ya Idi Amin na Kay ilifungwa kiserikali. Kay alivalia shera nyeupe na Amin alivaa nguo za kivita kama anayeenda kupigana na adui! Sherehe ilifanyika Arua, nyumbani kwao Amin. Mpambe alikuwa Erinayo Oryema, ambaye baadae alizawadiwa uwaziri wa ardhi na maji, pamoja na yote, baadaye aliuawa!

Ndani ya mwaka mmoja, Amin aliongeza mke wa tatu, Nora, kabila lake mlangi kutoka nyumbani kwao Obote. Ndoa ya Amin na Nora ilikuwa ni mkakati wa kisiasa. Baada ya Amin kujizolea umaarufu, Obote akawa na mashaka kuhusu lengo hasa la Amin. Kuoa binti kutoka kabila la Obote, kungefanya ionekane kuwa tofauti yao ya makabila si tatizo na hivyo kupunguza wasiwasi. Mpaka inafika mwishoni mwa miaka ya 60, Amin alikuwa na watoto kumi au kumi na tano.

Inaendelea...

Soma: Jinsi ya Kuandika CV
 
Haya tupe/leta mwendelezo...
Nduli (Iddi Amini Dada) hili neno "NDULI"
Nalo Lina maana gani..!!?
 
2

Mke wa nne aliitwa Medina, mnenguaji kutoka Uganda. Alikuwa na umbo zuri lililofikia viwango vyote. Wanawake wengi wa Uganda wamejaa nyuma (kigezo hiki hutumika kama miongoni mwa vigezo vya urembo) lakini Medina hakuwa hivyo. Alikuwa na umbo jembamba namba nane, matiti yaliyotengenezwa vizuri yakajaa vyema na alikuwa mnenguaji mtundu. Hata hivyo hakuwa na akili nyingi kama Kay wala mama bora kama Malyam.

Mahusiano ya Amin na Medina yalianza kwa siri. Mara nyingi walinzi walikuwa wakimpeleka Medina chumbani kwa Amin usiku. Kabla mahusiano yake na Medina hayajajulikana, alipenda kuwaambia mawaziri wake kwamba yeyote ambaye angetaka kuwa na Medina, awe naye, yupo muda wote na ni mnenguaji mzuri. Kwa kufuata ushauri huo, waziri mmoja alimtongoza Medina bila mafanikio. Hata hivyo Waziri huyu alihamishwa wizara na baadaye alitenguliwa.

Amin alitangaza ndoa na Medina Septemba 1972, ni mwaka na mwezi huu majeshi ya Obote yakitokea Tanzania yalivamia Uganda, Amin aliweza kuyadhibiti vyema. Wakati watu wakisikiliza redio ili waweze kusikia habari za uvamizi wa majeshi ya Obote, walishangazwa kusikia tangazo la Amin kuongeza mke wa nne. Alidai kwamba, watu wa kabila la Baganda wamempa zawadi ya mke kama heshima kwa yote aliyowafanyia tangu apindue serikali. Habari hii iliwachanganya Baganda kwani Amin aliwaua wengi.

Mwaka 1973, Amin alikuwa na wake wanne na watoto ishirini, wakiwemo watoto aliozaa na michepuko.

Mnamo tarehe 26 mwezi machi, 1976, Amin aliwapa talaka wake zake watatu: Malyamu, Kay na Nora. Talaka zilitolewa kwa kuzingatia kanuni ya dini ya Kiislamu “Nakutaliki, nakutaliki, nakutaliki.” habari za talaka zilitangazwa redio ya taifa. Pia Amin alitangaza kwamba alihitaji kubaki na mke mmoja, Medina.

Sababu ya kutoa talaka iliyotajwa na Amin ilikuwa ya kizalendo. Aliwatuhumu Malyamu na Nora kujihusisha na biashara. Hata hivyo ilishangaza kwa sababu ni Amin mwenyewe aliwapa biashara hizo kipindi alipowafukuza wahindi na kupora mali zao. Kuhusu Kay, alisema alikuwa binamu yake na undugu ulikuwa wa karibu sana kuweza kuwa katika ndoa.

sababu zote zilizotolewa na Amin kuhusu kuachana na wake zake hazikuwa na mashiko na ulikuwa uongo mtupu! Nitakueleza sababu iliyopelekea Amin akaachana na wake zake. Walichepuka! Waogope wanawake, Amin aliyekuwa mbabe alimegewa matunda yake! Waogope wanawake! Pamoja na kwamba alijaza walinzi wa kuwalinda, walitafunwa na vidume waliokubuhu katika sekta ya uzinzi. Ni ujasiri kiasi gani unahitaji kuwa nao ili kulala na mke wa Dikteta wa viwango vya juu kama Idi Amin Dada, jina Dada halimaanishi dada mwanamke, Amin alipenda kujiita Dada akiwa na maana ya Babu, grandfather na pengine ‘Big Daddy’? lilikuwa jitu haswa tena bingwa la uzito wa juu katika ndondi! Amin akayamwaga machozi! Masikini Idi! His Excellency, President for Life, Field Marshal Al Hadji Doctor Idi Amin Dada, VC, DSO, MC, Lord of All the Beasts of the Earth and Fishes of the Sea, and Conqueror of the British Empire in Africa in General and Uganda in Particular, alijeruhiwa. Muogope mnyama aliyejeruhiwa, shughuli yake pevu.

Inaendelea...

Soma: Jinsi ya Kuandika CV na Barua ya Maombi ya Kazi
 
Sawa ngoja tujifunze kuandika CV
2

Mke wa nne aliitwa Medina, mnenguaji kutoka Uganda. Alikuwa na umbo zuri lililofikia viwango vyote. Wanawake wengi wa Uganda wamejaa nyuma (kigezo hiki hutumika kama miongoni mwa vigezo vya urembo) lakini Medina hakuwa hivyo. Alikuwa na umbo jembamba namba nane, matiti yaliyotengenezwa vizuri yakajaa vyema na alikuwa mnenguaji mtundu. Hata hivyo hakuwa na akili nyingi kama Kay wala mama bora kama Malyam.

Mahusiano ya Amin na Medina yalianza kwa siri. Mara nyingi walinzi walikuwa wakimpeleka Medina chumbani kwa Amin usiku. Kabla mahusiano yake na Medina hayajajulikana, alipenda kuwaambia mawaziri wake kwamba yeyote ambaye angetaka kuwa na Medina, awe naye, yupo muda wote na ni mnenguaji mzuri. Kwa kufuata ushauri huo, waziri mmoja alimtongoza Medina bila mafanikio. Hata hivyo Waziri huyu alihamishwa wizara na baadaye alitenguliwa.

Amin alitangaza ndoa na Medina Septemba 1972, ni mwaka na mwezi huu majeshi ya Obote yakitokea Tanzania yalivamia Uganda, Amin aliweza kuyadhibiti vyema. Wakati watu wakisikiliza redio ili waweze kusikia habari za uvamizi wa majeshi ya Obote, walishangazwa kusikia tangazo la Amin kuongeza mke wa nne. Alidai kwamba, watu wa kabila la Baganda wamempa zawadi ya mke kama heshima kwa yote aliyowafanyia tangu apindue serikali. Habari hii iliwachanganya Baganda kwani Amin aliwaua wengi.

Mwaka 1973, Amin alikuwa na wake wanne na watoto ishirini, wakiwemo watoto aliozaa na michepuko.

Mnamo tarehe 26 mwezi machi, 1976, Amin aliwapa talaka wake zake watatu: Malyamu, Kay na Nora. Talaka zilitolewa kwa kuzingatia kanuni ya dini ya Kiislamu “Nakutaliki, nakutaliki, nakutaliki.” habari za talaka zilitangazwa redio ya taifa. Pia Amin alitangaza kwamba alihitaji kubaki na mke mmoja, Medina.

Sababu ya kutoa talaka iliyotajwa na Amin ilikuwa ya kizalendo. Aliwatuhumu Malyamu na Nora kujihusisha na biashara. Hata hivyo ilishangaza kwa sababu ni Amin mwenyewe aliwapa biashara hizo kipindi alipowafukuza wahindi na kupora mali zao. Kuhusu Kay, alisema alikuwa binamu yake na undugu ulikuwa wa karibu sana kuweza kuwa katika ndoa.

sababu zote zilizotolewa na Amin kuhusu kuachana na wake zake hazikuwa na mashiko na ulikuwa uongo mtupu! Nitakueleza sababu iliyopelekea Amin akaachana na wake zake. Walichepuka! Waogope wanawake, Amin aliyekuwa mbabe alimegewa matunda yake! Waogope wanawake! Pamoja na kwamba alijaza walinzi wa kuwalinda, walitafunwa na vidume waliokubuhu katika sekta ya uzinzi. Ni ujasiri kiasi gani unahitaji kuwa nao ili kulala na mke wa Dikteta wa viwango vya juu kama Idi Amin Dada, jina Dada halimaanishi dada mwanamke, Amin alipenda kujiita Dada akiwa na maana ya Babu, grandfather na pengine ‘Big Daddy’? lilikuwa jitu haswa tena bingwa la uzito wa juu katika ndondi! Amin akayamwaga machozi! Masikini Idi! His Excellency, President for Life, Field Marshal Al Hadji Doctor Idi Amin Dada, VC, DSO, MC, Lord of All the Beasts of the Earth and Fishes of the Sea, and Conqueror of the British Empire in Africa in General and Uganda in Particular, alijeruhiwa. Muogope mnyama aliyejeruhiwa, shughuli yake pevu.

Inaendelea...

Soma: Jinsi ya Kuandika CV na Barua ya Maombi ya Kazi
 
Na: Mwalimu Makoba

1

Hadithi ya Idi Amin na wake zake ni miongoni mwa hadithi za kusisimua, kuchekesha na zilizojaa ukatili. Kuwa na wake watano na wote wazuri ni msisimko wa aina yake. Kuwa na michepuko thelathini na watoto thelathini na nne (namba ya idadi ya watoto wa Idi Amin haijawahi kuwa sawa, hutofautiana hata katika nyaraka rasmi).

Mke wa kwanza aliitwa Maryamu, mtoto wa mwalimu mkuu, Bwana Kibedi, na dada wa Waziri wa Mambo ya Nje, Wanume Kibedi.

Ingawa alizaa naye watoto kadhaa, hakufunga naye ndoa mpaka ilipofika mwaka 1966, mwaka alioshambulia makazi ya Kabaka na kujizolea umaarufu mkubwa. Kupata watoto bila kufunga ndoa siyo jambo la ajabu Uganda. Idi Amin alilipa mahari, ndoa ikatambulika.

Amin aliishi na mke huyu kwa miaka kumi na tatu. Alikuwa tayari kutafuta mke mdogo kama ilivyo desturi. Alihitaji mke kutoka kabila lake ndipo akampata Kay Adroa. Alimchagua Kay kwa sababu alikuwa msomi kutoka chuo Kikuu cha Makerere, mrembo, mpole na aliyekuwa na aliyekamilika kila idara.

Amin aliifahamu familia ya Kay vizuri. Hata mwaka 1966, bunge lilipoomba kusimamishwa kazi kwa Idi Amin kwa sababu ya tuhuma za wizi wa dhahabu, alikwenda mafichoni na Kay. Kay alikuwa mkiristo kama Malyam. Ndoa ya Idi Amin na Kay ilifungwa kiserikali. Kay alivalia shera nyeupe na Amin alivaa nguo za kivita kama anayeenda kupigana na adui! Sherehe ilifanyika Arua, nyumbani kwao Amin. Mpambe alikuwa Erinayo Oryema, ambaye baadae alizawadiwa uwaziri wa ardhi na maji, pamoja na yote, baadaye aliuawa!

Ndani ya mwaka mmoja, Amin aliongeza mke wa tatu, Nora, kabila lake mlangi kutoka nyumbani kwao Obote. Ndoa ya Amin na Nora ilikuwa ni mkakati wa kisiasa. Baada ya Amin kujizolea umaarufu, Obote akawa na mashaka kuhusu lengo hasa la Amin. Kuoa binti kutoka kabila la Obote, kungefanya ionekane kuwa tofauti yao ya makabila si tatizo na hivyo kupunguza wasiwasi. Mpaka inafika mwishoni mwa miaka ya 60, Amin alikuwa na watoto kumi au kumi na tano.

Inaendelea...

Soma: Jinsi ya Kuandika CV
Kuna sehemu umetupiga mzee..........Kabila la Obote sio MLANGI bali ni LANGO,hawa ni wajaluo kama Waacholi,Walur,Jonam au Jopadhola,Uganda imetawaliwa na Wajaluo wengi sana kuliko ata Kenya pamoja na sifa zao zote


Jitahidi kufanya utafiti kabla ya kuleta bandiko lako jukwaani
 
Kuna sehemu umetupiga mzee..........Kabila la Obote sio MLANGI bali ni LANGO,hawa ni wajaluo kama Waacholi,Walur,Jonam au Jopadhola,Uganda imetawaliwa na Wajaluo wengi sana kuliko ata Kenya pamoja na sifa zao zote


Jitahidi kufanya utafiti kabla ya kuleta bandiko lako jukwaani
Umelazimishwa kusoma mkuu ?
 
Kuna sehemu umetupiga mzee..........Kabila la Obote sio MLANGI bali ni LANGO,hawa ni wajaluo kama Waacholi,Walur,Jonam au Jopadhola,Uganda imetawaliwa na Wajaluo wengi sana kuliko ata Kenya pamoja na sifa zao zote


Jitahidi kufanya utafiti kabla ya kuleta bandiko lako jukwaani
Obote, oyite ojok, Tito okello, taja wengine. Hata Zanzibar ilitawaliwa na mjaluo John okello.
 
Kuna sehemu umetupiga mzee..........Kabila la Obote sio MLANGI bali ni LANGO,hawa ni wajaluo kama Waacholi,Walur,Jonam au Jopadhola,Uganda imetawaliwa na Wajaluo wengi sana kuliko ata Kenya pamoja na sifa zao zote


Jitahidi kufanya utafiti kabla ya kuleta bandiko lako jukwaani
Umeandika sahihi. Milton Obote kabila lake ni Lango. Hata hivyo Lango na Langi hutumika kuwakilisha kitu kimoja. kwa kimombo kilichonyooka wanasema, "The term "Langi" is sometimes used interchangeably with "Lango." Umenikumbusha kipindi nasoma nilipatwa na kizaazaa kubaini ipi sahihi, Ngoni au Nguni?
 
Umeandika sahihi. Milton Obote kabila lake ni Lango. Hata hivyo Lango na Langi hutumika kuwakilisha kitu kimoja. kwa kimombo kilichonyooka wanasema, "The term "Langi" is sometimes used interchangeably with "Lango." Umenikumbusha kipindi nasoma nilipatwa na kizaazaa kubaini ipi sahihi, Ngoni au Nguni?
Noted mkuu
 
Na: Mwalimu Makoba

1

Hadithi ya Idi Amin na wake zake ni miongoni mwa hadithi za kusisimua, kuchekesha na zilizojaa ukatili. Kuwa na wake watano na wote wazuri ni msisimko wa aina yake. Kuwa na michepuko thelathini na watoto thelathini na nne (namba ya idadi ya watoto wa Idi Amin haijawahi kuwa sawa, hutofautiana hata katika nyaraka rasmi).

Mke wa kwanza aliitwa Maryamu, mtoto wa mwalimu mkuu, Bwana Kibedi, na dada wa Waziri wa Mambo ya Nje, Wanume Kibedi.

Ingawa alizaa naye watoto kadhaa, hakufunga naye ndoa mpaka ilipofika mwaka 1966, mwaka alioshambulia makazi ya Kabaka na kujizolea umaarufu mkubwa. Kupata watoto bila kufunga ndoa siyo jambo la ajabu Uganda. Idi Amin alilipa mahari, ndoa ikatambulika.

Amin aliishi na mke huyu kwa miaka kumi na tatu. Alikuwa tayari kutafuta mke mdogo kama ilivyo desturi. Alihitaji mke kutoka kabila lake ndipo akampata Kay Adroa. Alimchagua Kay kwa sababu alikuwa msomi kutoka chuo Kikuu cha Makerere, mrembo, mpole na aliyekuwa na aliyekamilika kila idara.

Amin aliifahamu familia ya Kay vizuri. Hata mwaka 1966, bunge lilipoomba kusimamishwa kazi kwa Idi Amin kwa sababu ya tuhuma za wizi wa dhahabu, alikwenda mafichoni na Kay. Kay alikuwa mkiristo kama Malyam. Ndoa ya Idi Amin na Kay ilifungwa kiserikali. Kay alivalia shera nyeupe na Amin alivaa nguo za kivita kama anayeenda kupigana na adui! Sherehe ilifanyika Arua, nyumbani kwao Amin. Mpambe alikuwa Erinayo Oryema, ambaye baadae alizawadiwa uwaziri wa ardhi na maji, pamoja na yote, baadaye aliuawa!

Ndani ya mwaka mmoja, Amin aliongeza mke wa tatu, Nora, kabila lake mlangi kutoka nyumbani kwao Obote. Ndoa ya Amin na Nora ilikuwa ni mkakati wa kisiasa. Baada ya Amin kujizolea umaarufu, Obote akawa na mashaka kuhusu lengo hasa la Amin. Kuoa binti kutoka kabila la Obote, kungefanya ionekane kuwa tofauti yao ya makabila si tatizo na hivyo kupunguza wasiwasi. Mpaka inafika mwishoni mwa miaka ya 60, Amin alikuwa na watoto kumi au kumi na tano.

Inaendelea...

Soma: Jinsi ya Kuandika CV
Mkuu, weka basi picha za hao warembo wa idd Amin Dadaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom