Mkasa: Jinsi nilivyofunzwa uchawi na mama yangu

DR SANTOS

JF-Expert Member
Mar 11, 2019
10,519
21,439
SEHEMU YA KWANZA.
Nikiwa nimerudi kutoka shuleni nilikutana na mama nje ambaye alinambia tumepata mgeni ambaye atakua akitusaidia kazi za ndani yaani dada wa kazi, kutokana na uchovu na fimbo za siku hio hata sikua na hamu ya kutaka kujua zaidi kuhusu jambo hilo nilimjibu mama kwa kifupi.

“haya”. Huku nikielekea ndani ambapo nilifika na kumkuta dada mmoja aliyekua na umri kati na miaka kumi na saba hadi ishirini ambaye alinichangamkia kama mtu tuliyejuana siku nyingi.

“mambo clara habari ya shule”. Aliongea dada Yule. Na kunifanya nishangae kalijuaje jina langu lakini nilihisi huenda mama alishamwambia kwamba ana mtoto anaeitwa clara.

“nzuri shikamoo dada,”. Niimjibu kwa heshima kwa kua alikua ameninzidi ki umri hivyo alistahili heshima kwani mimi nilikua darasa la nne tu, baada ya kumjibu nilielekea ndani na kulitua begi langu pia nilikuta mizigo ya dada Yule ambaye ilionesha hakua amefika muda mrefu.

Kwakua tulikua tukipata chakula shuleni nilipitiliza kulala ambapo usingizi ulinipitia na nilikuja kustuka majira ya saa sita usiku ambapo nilimuona dada Yule akiwa ameketi kitandani uchi wa mnyama huku akiwa ameinguanisha mikono yake kama mtu aliyekua akisali.

Moyo wangu uliogopa sana na nililazimika kufikicha macho ili nijue kwamba ilikua ndoto au la na niligundua kwamba haikua ndoto bali ilikua ni ukweli kabisa.

Kisha dada Yule akasimama na kuanza kutembea tembea ndani ya chumba changu huku mikono akiwa ameikunja vile vile na macho yake yakiwa yamefungwa, na kisha baada ya muda, alirudi kitandani na kuketi kama alivyokua awali.

Baada ya dakika tano nilimshuhudia mama nae akija chumbani akiwa amevaa kama dada Yule, hapo nilishindwa kujizuia na kutamka.

“haaa, mama kumbe nawe mchawi”. Niliongea kwa mashangao kauli ambayo ilimstua sana mama na kisha akanisogelea bila uwoga na kuniambia.

“shhhhhhhhh, hakuna haja ya kujificha sasa mimi ni mchawi ndio na hata wewe ni lazima uwe mchawi au laa nikuue kama nilivyomfanya baba yako”.aiongea mama maneno ambayo yalinistua sana na kunifanya nianze kutetemeka.

“unaogopa nini? Mimi ni mchawi toka nilipokua na umri kama wewe umewahi kunigundua? Umewahi kuniona nikitisha? Acha ujinga mwanangu”. Aliongea mama na baada ya muda tulimshuhudia dada Yule wa kazi akiinuka huku macho yake yakiwa yanawaka kama tochi. Na hapo nilimshuhudia mama akipiga goti na kuanza kumsujudu dada Yule.

“naam mkuu, nimekuletea binti huyu akiwa kama mwanachama mpya”. Aliongea mama ambapo dada Yule alinitazama kwa makini sana kisha kumgeukia mama.

“inabidi tumfundishe taratibu kabla ya kumtambulisha kwa wenzetu”. Aliongea dada Yule kisha nilimshuhudia mama akiinuka na kunigeukia.

“mwanangu clara, wewe ndiye wa pekee kwangu na nimekuteua wewe upate kujua vitu vyangu vya ndani, na mbona sikuwaambia kaka zako? Naomba uniisitiri”. Aliongea mama na kunipa mtihani mgumu sana katika umri mdogo na mpaka apo sikua nimesema jambo lolote.

Mwisho mama alichukua unga mweupe na kunipaka katika paji la uso kisha tulijikuta sehemu nyingine kabisa ambayo ilikua ngeni kabisa lakini iionesha ilikua ni katika msitu uliopo kando ya barabara.

Kwani magari yalikua yakisikika yakipiita,
“mwanangu, huu ni msitu wa wachawi msitu ambao ukiingia kama si mchawi basi huwezi toka na utafanywa kafara”. Aliongea mama kauli ambayo ilinifanya niwaone wachawi ni watu wabaya.

“Watu wengi wamepotea katika msitu huu na vifo vyao vilikua vya kutatanisha , hiii ni kwasababu wanachukuliwa na mizimu na kufanywa kafara lakini mchawi si mtu mbaya ila wapo ambao wanautumia uchwi vibaya kwa kufanya visasi na mauaji”. Aliongea mama mambo mengi kuhusu uchawi kisha alinifundisha dawa nyingi sana za kichwawi ikiwemo za kupotea na kiini macho.

Kwakua muda ulikua umekwenda tulirejea nyumbani ambapo bado nilikua na maswali mengi sana na siku hio nilipanga ktoka na kwenda kwa rafiki yangu zuwena nipate kumuuliza mambo kadhaa kuhusu hali iliyonitokea jana usiku.

Nilimuaga mama vizuri na kumwambia nilikua nikienda kwa rafiki yang na alichonisisitiza ni kuwahi kurudi.
Nilipofika nyumbani kwa rafiki yangu kulikua kimya sana ambapo nilibisha hodi mara tatu na kufunguliwa na zuwena mwenyewe
“mambo clara”. Alinisalimu zuwena huku akinikaribisha ndani ambapo tulipiga storiza hapa na pale mwisho niliamua kumuuliza swali.

“eti unawafahamu wachawi”. Nilihoji
“eee, ni wanatisha sana na ni wabaya, wauaji na hawana huruma”. Zuwena aliongea kana kwamba ni mtu anaejua mambo mengi sana kuhusu uchawi.

“basi nikwambie kitu zuwena, mwenzio mama yangu ni……”. Kabla sijamaliza ilikuja sauti kichwani mwangu ambayo niliitambua kwamba ni ya mama.

“clara unataka kufanya nini?” iliskika sauti hio
Je nini kilifuata
 
Mchawi analoga mazao yasikue kisha ni yeye anakuja athirika kwa kununua mazao kwa bei juu sababu ya mavuno haba, mchawi anabeba mimba kwa tabu zote KISHA anakuja mtoa sadaka mwanae kwa shetani tena kwa lazima sio ombi faida yake nini sasa. Kama sio akili ndogo kuliko yai la kuku.
 
SEHEMU YA KWANZA.
Nikiwa nimerudi kutoka shuleni nilikutana na mama nje ambaye alinambia tumepata mgeni ambaye atakua akitusaidia kazi za ndani yaani dada wa kazi, kutokna na uchovu na fimbo za siku hio hata sikua na hamu ya kutaka kujua zaidi kuhusu jambo hilo nilimjibu mama kwa kifupi.

“haya”. Huku nikielekea ndani ambapo nilifika na kumkuta dada mmoja aliyekua na umri kati na miaka kumi na saba hadi ishirini ambaye alinichangamkia kama mtu tuliyejuana siku nyingi.

“mambo clara habari ya shule”. Aliongea dada Yule. Na kunifanya nishangae kalijuaje jina langu lakini nilihisi huenda mama alishamwambia kwamba ana mtoto anaeitwa clara.

“nzuri shikamoo dada,”. Niimjibu kwa heshima kwa kua alikua ameninzidi ki umri hivyo alistahili heshima kwani mimi nilikua darasa la nne tu, baada ya kumjibu nilielekea ndani na kulitua begi langu pia nilikuta mizigo ya dada Yule ambaye ilionesha hakua amefika muda mrefu.

Kwakua tulikua tukipata chakula shuleni nilipitiliza kulala ambapo usingizi ulinipitia na nilikuja kustuka majira ya saa sita usiku ambapo nilimuona dada Yule akiwa ameketi kitandani uchi wa mnyama huku akiwa ameinguanisha mikono yake kama mtu aliyekua akisali.

Moyo wangu uliogopa sana na nililazimika kufikicha macho ili nijue kwamba ilikua ndoto au la na niligundua kwamba haikua ndoto bali ilikua ni ukweli kabisa.

Kisha dada Yule akasimama na kuanza kutembea tembea ndani ya chumba changu huku mikono akiwa ameikunja vile vile na macho yake yakiwa yamefungwa, na kisha baada ya muda, alirudi kitandani na kuketi kama alivyokua awali.

Baada ya dakika tano nilimshuhudia mama nae akija chumbani akiwa amevaa kama dada Yule, hapo nilishindwa kujizuia na kutamka.

“haaa, mama kumbe nawe mchawi”. Niliongea kwa mashangao kauli ambayo ilimstua sana mama na kisha akanisogelea bila uwoga na kuniambia.

“shhhhhhhhh, hakuna haja ya kujificha sasa mimi ni mchawi ndio na hata wewe ni lazima uwe mchawi au laa nikuue kama nilivyomfanya baba yako”.aiongea mama maneno ambayo yalinistua sana na kunifanya nianze kutetemeka.

“unaogopa nini? Mimi ni mchawi toka nilipokua na umri kama wewe umewahi kunigundua? Umewahi kuniona nikitisha? Acha ujinga mwanangu”. Aliongea mama na baada ya muda tulimshuhudia dada Yule wa kazi akiinuka huku macho yake yakiwa yanawaka kama tochi. Na hapo nilimshuhudia mama akipiga goti na kuanza kumsujudu dada Yule.

“naam mkuu, nimekuletea binti huyu akiwa kama mwanachama mpya”. Aliongea mama ambapo dada Yule alinitazama kwa makini sana kisha kumgeukia mama.

“inabidi tumfundishe taratibu kabla ya kumtambulisha kwa wenzetu”. Aliongea dada Yule kisha nilimshuhudia mama akiinuka na kunigeukia.

“mwanangu clara, wewe ndiye wa pekee kwangu na nimekuteua wewe upate kujua vitu vyangu vya ndani, na mbona sikuwaambia kaka zako? Naomba uniisitiri”. Aliongea mama na kunipa mtihani mgumu sana katika umri mdogo na mpaka apo sikua nimesema jambo lolote.

Mwisho mama alichukua unga mweupe na kunipaka katika paji la uso kisha tulijikuta sehemu nyingine kabisa ambayo ilikua ngeni kabisa lakini iionesha ilikua ni katika msitu uliopo kando ya barabara.

Kwani magari yalikua yakisikika yakipiita,
“mwanangu, huu ni msitu wa wachawi msitu ambao ukiingia kama si mchawi basi huwezi toka na utafanywa kafara”. Aliongea mama kauli ambayo ilinifanya niwaone wachawi ni watu wabaya.

“Watu wengi wamepotea katika msitu huu na vifo vyao vilikua vya kutatanisha , hiii ni kwasababu wanachukuliwa na mizimu na kufanywa kafara lakini mchawi si mtu mbaya ila wapo ambao wanautumia uchwi vibaya kwa kufanya visasi na mauaji”. Aliongea mama mambo mengi kuhusu uchawi kisha alinifundisha dawa nyingi sana za kichwawi ikiwemo za kupotea na kiini macho.

Kwakua muda ulikua umekwenda tulirejea nyumbani ambapo bado nilikua na maswali mengi sana na siku hio nilipanga ktoka na kwenda kwa rafiki yangu zuwena nipate kumuuliza mambo kadhaa kuhusu hali iliyonitokea jana usiku.

Nilimuaga mama vizuri na kumwambia nilikua nikienda kwa rafiki yang na alichonisisitiza ni kuwahi kurudi.
Nilipofika nyumbani kwa raf

iki yangu kulikua kimya sana ambapo nilibisha hodi mara tatu na kufunguliwa na zuwena mwenyewe
“mambo clara”. Alinisalimu zuwena huku akinikaribisha ndani ambapo tulipiga storiza hapa na pale mwisho niliamua kumuuliza swali.

“eti unawafahamu wachawi”. Nilihoji
“eee, ni wanatisha sana na ni wabaya, wauaji na hawana huruma”. Zuwena aliongea kana kwamba ni mtu anaejua mambo mengi sana kuhusu uchawi.

“basi nikwambie kitu zuwena, mwenzio mama yangu ni……”. Kabla sijamaliza ilikuja sauti kichwani mwangu ambayo niliitambua kwamba ni ya mama.

“clara unataka kufanya nini?” iliskika sauti hio
Je nini kilifuata
Tuendelee na hii...... Wakati tukiendelea kumsubili UMUGHAKA
 
SEHEMU YA KWANZA.
Nikiwa nimerudi kutoka shuleni nilikutana na mama nje ambaye alinambia tumepata mgeni ambaye atakua akitusaidia kazi za ndani yaani dada wa kazi, kutokana na uchovu na fimbo za siku hio hata sikua na hamu ya kutaka kujua zaidi kuhusu jambo hilo nilimjibu mama kwa kifupi.

“haya”. Huku nikielekea ndani ambapo nilifika na kumkuta dada mmoja aliyekua na umri kati na miaka kumi na saba hadi ishirini ambaye alinichangamkia kama mtu tuliyejuana siku nyingi.

“mambo clara habari ya shule”. Aliongea dada Yule. Na kunifanya nishangae kalijuaje jina langu lakini nilihisi huenda mama alishamwambia kwamba ana mtoto anaeitwa clara.

“nzuri shikamoo dada,”. Niimjibu kwa heshima kwa kua alikua ameninzidi ki umri hivyo alistahili heshima kwani mimi nilikua darasa la nne tu, baada ya kumjibu nilielekea ndani na kulitua begi langu pia nilikuta mizigo ya dada Yule ambaye ilionesha hakua amefika muda mrefu.

Kwakua tulikua tukipata chakula shuleni nilipitiliza kulala ambapo usingizi ulinipitia na nilikuja kustuka majira ya saa sita usiku ambapo nilimuona dada Yule akiwa ameketi kitandani uchi wa mnyama huku akiwa ameinguanisha mikono yake kama mtu aliyekua akisali.

Moyo wangu uliogopa sana na nililazimika kufikicha macho ili nijue kwamba ilikua ndoto au la na niligundua kwamba haikua ndoto bali ilikua ni ukweli kabisa.

Kisha dada Yule akasimama na kuanza kutembea tembea ndani ya chumba changu huku mikono akiwa ameikunja vile vile na macho yake yakiwa yamefungwa, na kisha baada ya muda, alirudi kitandani na kuketi kama alivyokua awali.

Baada ya dakika tano nilimshuhudia mama nae akija chumbani akiwa amevaa kama dada Yule, hapo nilishindwa kujizuia na kutamka.

“haaa, mama kumbe nawe mchawi”. Niliongea kwa mashangao kauli ambayo ilimstua sana mama na kisha akanisogelea bila uwoga na kuniambia.

“shhhhhhhhh, hakuna haja ya kujificha sasa mimi ni mchawi ndio na hata wewe ni lazima uwe mchawi au laa nikuue kama nilivyomfanya baba yako”.aiongea mama maneno ambayo yalinistua sana na kunifanya nianze kutetemeka.

“unaogopa nini? Mimi ni mchawi toka nilipokua na umri kama wewe umewahi kunigundua? Umewahi kuniona nikitisha? Acha ujinga mwanangu”. Aliongea mama na baada ya muda tulimshuhudia dada Yule wa kazi akiinuka huku macho yake yakiwa yanawaka kama tochi. Na hapo nilimshuhudia mama akipiga goti na kuanza kumsujudu dada Yule.

“naam mkuu, nimekuletea binti huyu akiwa kama mwanachama mpya”. Aliongea mama ambapo dada Yule alinitazama kwa makini sana kisha kumgeukia mama.

“inabidi tumfundishe taratibu kabla ya kumtambulisha kwa wenzetu”. Aliongea dada Yule kisha nilimshuhudia mama akiinuka na kunigeukia.

“mwanangu clara, wewe ndiye wa pekee kwangu na nimekuteua wewe upate kujua vitu vyangu vya ndani, na mbona sikuwaambia kaka zako? Naomba uniisitiri”. Aliongea mama na kunipa mtihani mgumu sana katika umri mdogo na mpaka apo sikua nimesema jambo lolote.

Mwisho mama alichukua unga mweupe na kunipaka katika paji la uso kisha tulijikuta sehemu nyingine kabisa ambayo ilikua ngeni kabisa lakini iionesha ilikua ni katika msitu uliopo kando ya barabara.

Kwani magari yalikua yakisikika yakipiita,
“mwanangu, huu ni msitu wa wachawi msitu ambao ukiingia kama si mchawi basi huwezi toka na utafanywa kafara”. Aliongea mama kauli ambayo ilinifanya niwaone wachawi ni watu wabaya.

“Watu wengi wamepotea katika msitu huu na vifo vyao vilikua vya kutatanisha , hiii ni kwasababu wanachukuliwa na mizimu na kufanywa kafara lakini mchawi si mtu mbaya ila wapo ambao wanautumia uchwi vibaya kwa kufanya visasi na mauaji”. Aliongea mama mambo mengi kuhusu uchawi kisha alinifundisha dawa nyingi sana za kichwawi ikiwemo za kupotea na kiini macho.

Kwakua muda ulikua umekwenda tulirejea nyumbani ambapo bado nilikua na maswali mengi sana na siku hio nilipanga ktoka na kwenda kwa rafiki yangu zuwena nipate kumuuliza mambo kadhaa kuhusu hali iliyonitokea jana usiku.

Nilimuaga mama vizuri na kumwambia nilikua nikienda kwa rafiki yang na alichonisisitiza ni kuwahi kurudi.
Nilipofika nyumbani kwa rafiki yangu kulikua kimya sana ambapo nilibisha hodi mara tatu na kufunguliwa na zuwena mwenyewe
“mambo clara”. Alinisalimu zuwena huku akinikaribisha ndani ambapo tulipiga storiza hapa na pale mwisho niliamua kumuuliza swali.

“eti unawafahamu wachawi”. Nilihoji
“eee, ni wanatisha sana na ni wabaya, wauaji na hawana huruma”. Zuwena aliongea kana kwamba ni mtu anaejua mambo mengi sana kuhusu uchawi.

“basi nikwambie kitu zuwena, mwenzio mama yangu ni……”. Kabla sijamaliza ilikuja sauti kichwani mwangu ambayo niliitambua kwamba ni ya mama.

“clara unataka kufanya nini?” iliskika sauti hio
Je nini kilifuata
Santos06, kwa hiyo wewe ni kama Mzee MAKONO, kama Monica na mama yake, au siyo mwanangu?

Au wewe level za Ally Mpemba, uchawi wa majini?
 
SEHEMU YA PILi:
INAENDELEA: uso ulinishuka ghafla baada ya kujikuta nikitaka kutoa siri ya mama kwa rafiki yangu zuwena.
“rudi nyumbani haraka”. Iliskika sauti ya mama ambapo haukupita muda zuwena alipitiwa na usingizi nami nilitumia afasi hio kuondoka haraka huku nikiwaza jambo la kumweleza mama endapo nikirudi nyumbani.

Nilipofika nyumbani nilimkuta mama akiwa nje uso wake akiwa ameukunja hadi nilianza kutetemeka kwani sijawahi kumwona mama akiwa amefura namna ile na nilijua lazima jambo lile litakua limemuudhi sana.

“sasa na ugemwambia ungefaidika nini”. Alihoji mama ambapo nami sikua na jibu kwani ukweli ni kwamba sikua nikipata faida yoyote. Baada ya mama kunisema nilirudi nyumbani na kukutana na dada wa kazi ambaye alikua ameketi.

“naona umerudi lakini ni mwiko kutoa siri a wachawi la sivyo kifo kitakuhusu”. Aliongea dada Yule nami sikujibu chochote zaidi ya kwenda chumbani ambapo nilifika na kuanza kulia kilio cha kwikwi kwani sikuona kimbilio langu.

Kama mama alimuua baba na anataka mimi niwe mchawi basi niliona kabisa jambo la kua mchawi haliepukiki kabisa.

Akili yangu ilianza kubadilika taratibu ambapo nilianza kufikiria jinsi nitakavyowakomesha maadui zangu na wale wote wanaonikosea hasa walimu wanaochapa sana bakora, wakati nikiendelea kuwaza hayo usingizi ulinipitia.

Nikiwa katika usingizi mzito nilijiwa na njozi iliyonionesha nikiwa katika msitu wa wachawi nikiwa na mama aliyekua akinionesha mambo mengi na dawa nyingi za kichawi, ambapo alinionesha mti mmoja aliouita mti mweupe kutokana na rangi yake ambao ulikua a magamba meupe ambapo alinitajia baadhi ya kazi za mti ule na una maana gani katika uchawi.

“kuna aina mbili za uchawi mwanangu, mweupe na mweusi na uchawi wenye asili ya khali iliogunduliwa nchini uajemi pia kuna uchawi wa kutabiri nyota peke lakini unaotumika sana ni huu mweupe na mweusi kwani hauhitaji elimu ukilinganisha na aina zingine za uchawi hambazo huhitaji mtu ajue kusoma na kuandika”.

Mama alinielekeza mambo mengi jinsi uchawi mweupe na mweusi unavyofanya kazi na yeye alitumia aina ipi ya uchawi

“uchawi mweupe na mweusi vinategemena kwa kiasi kikubwa kwani uchawi mweupe hutumika kutengeneza uchawi mweusi ambao huu ndio wenye kuweka watu misukule na wenye kuhitaji kafara ya damu ili uwe na nguvu maradufu”.

Aliogeza mama na wakati huo sikua nimesema chochote alikua akiongea yeye tu mwisho aliniambia angenifundisha kutengeneza dawa za kichawi kupitia mizizi ya miti mbalimbali pia angenifundisha kutega mitego ya kichawi pamoja na kafara kwani ili nipokelewe ilihitajika kafara ya damu.

Nilistuka jioni na nilikua na jaa kali sana, siku hio mvua ilinyesha muda mrefu sana na kutokana nyumba yetu haikua na dari basi nilijikuta nikikosa usingizi baada ya kupata chakula cha usiku sikuweza kupata tena usingizi kutokana na kulala mchana hadi mama alipokuja kuiamsha majira ya saa saba usiku.

“mwanangu amka twende tukafanye kazi niliyokuelekeza mchana”. Aliogea mama ambapo nami sikua na ubishi ambapo mama alinielekeza nivue nguo zote kisha akipa vazi la kaniki yenye rangi nyeusi na kunielekeza namna ya kufunga baada ya hapo aliamka na dada ambaye hata sikumjua jina lake kisha tuliketi chini na kushikana mikono kisha tulijikuta katika eneo jingine ambalo hakika lilikua geni katika macho yangu.

“mwanangu umeuona huo mti, majani yake hutumika kuona visivyoonekana mfano misukule na pesa za chuma ulete, pia ukisaga maganda yake na kupaka unga wake wewe unakua huonekani hutumika na wachawi katika shuguli za kuwanga na ulozi”. Alongea mama kisha akaendelea kunifundisha na kunielekeza namna ya kuchimba mizizi ile kisha alinielekeza vitu vingi sana pamoja na dawa za kutega mitego ya kichawi mfano ajali za kichawi pia dawa za kutolea kafara.

Mwisho tulishikana tena tukiwa tumeketi chini na tulijikuta tumetokea mbele ya nyumba moja nzuri ambayo ni ya tajiri mmoja pale kijijini.

“hapa tunaenda kufanya nini”. Nilihoji
“tunakwenda kuifungulia misukule yake kwani wachawi hua tuna tabia ya kuumbuana, hapa tunakwenda kumkomoa kwani

hata yeye anatumia utajiri wa nguvu za giza”.
Aliongea mama kisha akanipaka unga kwenye paji la uso na sehemu ya makalio alinambia nijipake, baada ya hapo mama na dada, waligeuka na kutembea kinyume nyume na kuusogelea ukuta wa nyumba hio ambapo nilishangaa kuona uwazi mkubwa kisha tukaingia na uwazi huo ukapotea.

Ajabu tulipofika chumbani kwa mzee Yule aliyetambulika kama mzee konzo hatukukuta mtu na hakukua na kutanda bali ni bwawa kubwa sana ambalo lilianza kujaa maji ghafla na nilijikuta nikipaliwa kuokana na maji kufikia shingoni na hatimaye kichwani, mama alinibeba mabegani na kakukua na ujanja wa kupotea kwani dawa zetu zilikua zimeshaloa.

Niliona kifo kikiwa mbele yetu.
Je nini kilifuata
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom