Storika Tz
Member
- Dec 18, 2023
- 17
- 47
....01
Waswahili wanasema simulia sana ila omba yasikukute. Mwenzenu yamenikuta. Yaliyonikuta honeymoon sitakuja kuyasahau. Nilichofanywa milele kitabaki moyoni mwangu.Sitasahau kamwe. Naomba ungana nami kwenye hii simulizi ya kweli kujua lipi ni lipi.
Sehemu ya kwanza.
Tukiwa nyumbani baada ya kutoka kufunga ndoa kanisani, ndugu wa Mume wangu walifanya mambo ambayo sikuyaelewa .Kila nilipoyafikiria nilishindwa kupata majibu.
" Kwanini ndugu zako wanafanya hivi ? " Nilimuuliza Sam.
" Wanafanyaje? "
" Aaaah! Inamaana huoni wanachokifanya. "
" Ndio sioni! Kama ningeona nisingekuuliza. "
" Wananikosea heshima . Muda wote wanaangalia maungo yangu. Nikitembea wanaangalia makalio yangu na kuniteta. " Nilimwambia.
Ajabu, Sam badala ya kuchukia, alicheka .Tena alicheka kicheko kilichoniacha mdomo wangu.
" Hivi hili ni jambo la kuchekesha?" Nilimuuliza.
" Achana na hayo Judi. Jiandae twende ukumbini.Muda umeenda." Aliniambia.
Alinishika mkono na kunipeleka chumbani.
" Jiandae. Saa moja kamili yatakiwa tuwe ukumbini." .
" Lakini Sam...."
" Achana na mambo madogo madogo. Jiandae twende ukumbini." Aliniambia.
Nilikuwa mpole.
Niliamua kufanya alichokitaka .Nilioga na kujipodoa.
" Waoooooo.....umependeza sana Mke wangu." Aliniambia .Alinisogelea na kunibusu kwenye paji la uso.
" Ahsante.." Nilimjibu.
Tuliongozana kutoka chumbani. Tukiwa kwenye korido tulikutana na Baba yake mdogo. Baada ya kuniona nilivyopendeza ,alijishika kichwa.
" Eeeeh! wewe ni mzuri.. " Aliniambia. Alinisogelea na kunizunguka kwa nyuma. Alinishika makalio .
" Mmmmh ..." Aliguna.
Kitendo cha kunishika makalio kilinikera. Niligeuka na kutaka kumwambia, lakini kabla sijaongea ,Sam aliongea.
" Sichaguagi vitu vya ajabu ajabu . Si unaona mzigo ." Aliongea Sam.
Kauli yake ilimaanisha anaunga mkono kitendo cha baba yake mdogo kunishika makalio.
" Huyu mwanaume wa ajabu sana. Inamaana kitendo cha Baba yake mdogo kunishika makalio anakiona cha kawaida ?" Nilijiuliza. Nilimtazama nikiwa na maswali.
" Nitaongea naye baadae. Kama anaona kawaida nitamueleza hii sio kawaida, ni kunikosea heshima." Nilijiambia.
.............................................................
Ukumbini.
Tabia ya ndugu wa Mume wangu kuniangalia na kuniteta iliendelea.
Safari hiii tofauti na nyumbani, walikuwa wakiniteta huku wakioneshana kitu kwenye simu. Ni kama kwenye ile simu kulikuwa na picha yangu. Muda wote waliongea huku wakiniangalia na kuangalia ile simu.
" Hivi hii ni kawaida?" Nilimuuliza Sam.
" Judi acha kuharibu sherehe yako. Kwanza usiniulize vitu visivyokuwa na msingi. Tupo hapa kwa ajili ya Kunywa ,kula na kusherekea."
" Nitasherekeaje wakati mambo hayapo sawa. Ndugu zako wanayateta maungo yangu?" Nilimwambia.
Badala ya kunijibu, Sam alichukua simu yake na kupiga. Alisimama na kwenda pembeni kidogo. Aliongea kwa sekunde kadhaa kisha akarudi .
.....................................
Sherehe ikiwa inakaribia kuisha,majira ya saa tano usiku, wazazi wa Sam yaani wakwe zangu walikuja kutuaga .Wakiwa wanatuaga waliongea kitu kilichoniacha mdomo wazi.
" Tunatangulia hotelini.." Aliongea Mama Mkwe.
" Mmmh! Kwanini waende hotelini? Kwanini wasiende nyumbani?" Nilijiuliza. Nilimgeukia Sam na kumuuliza.
" Wanaenda Hotel gani? "
" Legend Hotel." Alinijibu
Legend Hotel ni Hotel ambayo tulipanga kufanya fungate letu. Kitendo cha kuniambia wazazi wake wanaenda pale kilinichanganya.Sikuelewa wanaenda kufanya nini.
" Lakini kwanini waende hotelini? Si wangeenda nyumbani ."
" Mmmmh! Judi unagubu sana." Aliongea kwa ukali Sam.
Sikutaka kuendelea kumuuzi,niliamua kukaa kimya. Lakini gafla, ndugu zake waliokuwa wananiteta sikuwaona . Niliangaza kila pande, hawakuwepo ukumbini.
" Ndugu zako wameenda wapi ?" Nilimuuliza Sam.
" Wametangulia." Alinijibu kifupi.
" Wametangulia wapi?"
" Wametangulia Legend Hotel" .
" Eeeh! Na wao wameenda legend Hotel? Lakini kwanini wameenda kule? Kumbuka leo tunaanza Honey moon,na tutaifanyia pale."
Hakunijibu kitu.
Kutokunijibu kulimaanisha hayupo tayari kuliongelea swala nililomuuliza. Niliamua kukaa kimya.Sikutaka kumuuzi kwa maswali japo kichwani nilijiuliza sababu ya wao kwenda hotelini. Maana kwenye ile hoteli tulipaswa kwenda wawili tu.Mimi na Sam.
...............................
Majira ya saa sita usiku,Sherehe ukumbini iliisha. Mimi na Sam tuliondoka kuelekea Hotelini.
" Leo ni usiku wetu wa kwanza, nataka uwe wa kukumbukwa."Aliniambia huku akinibusu shavuni. Alipeleka mkono wake Ikulu kwangu.
" aaaaashiii..taratibu bana..." Nilimwambia .Nilimtoa mkono wake ikulu .
Nilimsogelea na kumnongoneza. " Mimi ni wako,subiri tufike.".
" Leo…..” Alitamka Sam.
Hakukaa sana alitamka tena.
“ Leo…”
“Leo..”
“ Leo nini?” Nilimuuliza.
Hakunijibu. Alitamka tena.
“ .leo....leo....leo...." Alitamka mara tatu. Aliniangalia kisha akanibinyia jicho.
" Kwanini anatamka hivi?" Nilijiuliza moyoni. Sikupata jibu. Niliamua kupuuzia.
………………..
Tulifika Hotelini.
Alinishusha kwenye gari . Alinibeba juu juu kuelekea chumbani. Njia nzima alinibusu na kunipapasa . Ni kama alikuwa na wazimu.
Tuliingia kwenye chumba tulichoandaliwa. Chumba kilikuwa na giza totoro.Alinilaza kitandani na kuendelea kunibusu .Alinitoa nguo na kuniacha kama nilivyozaliwa.
“ Washa taa kwanza..” Nilimwambia.
" Hivi ndio safi. " Aliniambia.
" mmmmh!" Niliguna. Giza lilikuwa totoro sana.
" Tunafanyaje mapenzi kwenye giza hili?" Nilijiuliza. Moyo wangu haukuridhika ila niliamua kupotezea. Sam alinibusu na kunichombeza.Alinigusa na kunichezea sehemu dhaifu.
“ Aaaa…ai…aaaa….” Nililalamika kila aliponigusa.
Gafla, Mwili ulinisisimka. Nywele zilinisimama. Hofu ilinishika na moyo ulipiga kwa kasi.
" ndi ... ndi...ndi... " Moyo ulipiga.
Nilitetemeka kwa woga.
Sifahamu nini kilitokea .Nilikosa amani kabisa.
" Mbona hivyo ?" Aliniuliza.
"Mwenyewe Sielewi. ..'
"Mmmmh! Basi Usiogope?" Aliniambia . Alinishika na kunilaza kitandani. Bila kujali hali yangu aliendelea kunipapasa na kunichombeza.
Akiwa anakilamba kifua changu, ajabu,gafla, ............
Nakuja
Waswahili wanasema simulia sana ila omba yasikukute. Mwenzenu yamenikuta. Yaliyonikuta honeymoon sitakuja kuyasahau. Nilichofanywa milele kitabaki moyoni mwangu.Sitasahau kamwe. Naomba ungana nami kwenye hii simulizi ya kweli kujua lipi ni lipi.
Sehemu ya kwanza.
Tukiwa nyumbani baada ya kutoka kufunga ndoa kanisani, ndugu wa Mume wangu walifanya mambo ambayo sikuyaelewa .Kila nilipoyafikiria nilishindwa kupata majibu.
" Kwanini ndugu zako wanafanya hivi ? " Nilimuuliza Sam.
" Wanafanyaje? "
" Aaaah! Inamaana huoni wanachokifanya. "
" Ndio sioni! Kama ningeona nisingekuuliza. "
" Wananikosea heshima . Muda wote wanaangalia maungo yangu. Nikitembea wanaangalia makalio yangu na kuniteta. " Nilimwambia.
Ajabu, Sam badala ya kuchukia, alicheka .Tena alicheka kicheko kilichoniacha mdomo wangu.
" Hivi hili ni jambo la kuchekesha?" Nilimuuliza.
" Achana na hayo Judi. Jiandae twende ukumbini.Muda umeenda." Aliniambia.
Alinishika mkono na kunipeleka chumbani.
" Jiandae. Saa moja kamili yatakiwa tuwe ukumbini." .
" Lakini Sam...."
" Achana na mambo madogo madogo. Jiandae twende ukumbini." Aliniambia.
Nilikuwa mpole.
Niliamua kufanya alichokitaka .Nilioga na kujipodoa.
" Waoooooo.....umependeza sana Mke wangu." Aliniambia .Alinisogelea na kunibusu kwenye paji la uso.
" Ahsante.." Nilimjibu.
Tuliongozana kutoka chumbani. Tukiwa kwenye korido tulikutana na Baba yake mdogo. Baada ya kuniona nilivyopendeza ,alijishika kichwa.
" Eeeeh! wewe ni mzuri.. " Aliniambia. Alinisogelea na kunizunguka kwa nyuma. Alinishika makalio .
" Mmmmh ..." Aliguna.
Kitendo cha kunishika makalio kilinikera. Niligeuka na kutaka kumwambia, lakini kabla sijaongea ,Sam aliongea.
" Sichaguagi vitu vya ajabu ajabu . Si unaona mzigo ." Aliongea Sam.
Kauli yake ilimaanisha anaunga mkono kitendo cha baba yake mdogo kunishika makalio.
" Huyu mwanaume wa ajabu sana. Inamaana kitendo cha Baba yake mdogo kunishika makalio anakiona cha kawaida ?" Nilijiuliza. Nilimtazama nikiwa na maswali.
" Nitaongea naye baadae. Kama anaona kawaida nitamueleza hii sio kawaida, ni kunikosea heshima." Nilijiambia.
.............................................................
Ukumbini.
Tabia ya ndugu wa Mume wangu kuniangalia na kuniteta iliendelea.
Safari hiii tofauti na nyumbani, walikuwa wakiniteta huku wakioneshana kitu kwenye simu. Ni kama kwenye ile simu kulikuwa na picha yangu. Muda wote waliongea huku wakiniangalia na kuangalia ile simu.
" Hivi hii ni kawaida?" Nilimuuliza Sam.
" Judi acha kuharibu sherehe yako. Kwanza usiniulize vitu visivyokuwa na msingi. Tupo hapa kwa ajili ya Kunywa ,kula na kusherekea."
" Nitasherekeaje wakati mambo hayapo sawa. Ndugu zako wanayateta maungo yangu?" Nilimwambia.
Badala ya kunijibu, Sam alichukua simu yake na kupiga. Alisimama na kwenda pembeni kidogo. Aliongea kwa sekunde kadhaa kisha akarudi .
.....................................
Sherehe ikiwa inakaribia kuisha,majira ya saa tano usiku, wazazi wa Sam yaani wakwe zangu walikuja kutuaga .Wakiwa wanatuaga waliongea kitu kilichoniacha mdomo wazi.
" Tunatangulia hotelini.." Aliongea Mama Mkwe.
" Mmmh! Kwanini waende hotelini? Kwanini wasiende nyumbani?" Nilijiuliza. Nilimgeukia Sam na kumuuliza.
" Wanaenda Hotel gani? "
" Legend Hotel." Alinijibu
Legend Hotel ni Hotel ambayo tulipanga kufanya fungate letu. Kitendo cha kuniambia wazazi wake wanaenda pale kilinichanganya.Sikuelewa wanaenda kufanya nini.
" Lakini kwanini waende hotelini? Si wangeenda nyumbani ."
" Mmmmh! Judi unagubu sana." Aliongea kwa ukali Sam.
Sikutaka kuendelea kumuuzi,niliamua kukaa kimya. Lakini gafla, ndugu zake waliokuwa wananiteta sikuwaona . Niliangaza kila pande, hawakuwepo ukumbini.
" Ndugu zako wameenda wapi ?" Nilimuuliza Sam.
" Wametangulia." Alinijibu kifupi.
" Wametangulia wapi?"
" Wametangulia Legend Hotel" .
" Eeeh! Na wao wameenda legend Hotel? Lakini kwanini wameenda kule? Kumbuka leo tunaanza Honey moon,na tutaifanyia pale."
Hakunijibu kitu.
Kutokunijibu kulimaanisha hayupo tayari kuliongelea swala nililomuuliza. Niliamua kukaa kimya.Sikutaka kumuuzi kwa maswali japo kichwani nilijiuliza sababu ya wao kwenda hotelini. Maana kwenye ile hoteli tulipaswa kwenda wawili tu.Mimi na Sam.
...............................
Majira ya saa sita usiku,Sherehe ukumbini iliisha. Mimi na Sam tuliondoka kuelekea Hotelini.
" Leo ni usiku wetu wa kwanza, nataka uwe wa kukumbukwa."Aliniambia huku akinibusu shavuni. Alipeleka mkono wake Ikulu kwangu.
" aaaaashiii..taratibu bana..." Nilimwambia .Nilimtoa mkono wake ikulu .
Nilimsogelea na kumnongoneza. " Mimi ni wako,subiri tufike.".
" Leo…..” Alitamka Sam.
Hakukaa sana alitamka tena.
“ Leo…”
“Leo..”
“ Leo nini?” Nilimuuliza.
Hakunijibu. Alitamka tena.
“ .leo....leo....leo...." Alitamka mara tatu. Aliniangalia kisha akanibinyia jicho.
" Kwanini anatamka hivi?" Nilijiuliza moyoni. Sikupata jibu. Niliamua kupuuzia.
………………..
Tulifika Hotelini.
Alinishusha kwenye gari . Alinibeba juu juu kuelekea chumbani. Njia nzima alinibusu na kunipapasa . Ni kama alikuwa na wazimu.
Tuliingia kwenye chumba tulichoandaliwa. Chumba kilikuwa na giza totoro.Alinilaza kitandani na kuendelea kunibusu .Alinitoa nguo na kuniacha kama nilivyozaliwa.
“ Washa taa kwanza..” Nilimwambia.
" Hivi ndio safi. " Aliniambia.
" mmmmh!" Niliguna. Giza lilikuwa totoro sana.
" Tunafanyaje mapenzi kwenye giza hili?" Nilijiuliza. Moyo wangu haukuridhika ila niliamua kupotezea. Sam alinibusu na kunichombeza.Alinigusa na kunichezea sehemu dhaifu.
“ Aaaa…ai…aaaa….” Nililalamika kila aliponigusa.
Gafla, Mwili ulinisisimka. Nywele zilinisimama. Hofu ilinishika na moyo ulipiga kwa kasi.
" ndi ... ndi...ndi... " Moyo ulipiga.
Nilitetemeka kwa woga.
Sifahamu nini kilitokea .Nilikosa amani kabisa.
" Mbona hivyo ?" Aliniuliza.
"Mwenyewe Sielewi. ..'
"Mmmmh! Basi Usiogope?" Aliniambia . Alinishika na kunilaza kitandani. Bila kujali hali yangu aliendelea kunipapasa na kunichombeza.
Akiwa anakilamba kifua changu, ajabu,gafla, ............
Nakuja