Sasa huu ndio uongo ulizidi kifani maanake sijui kama ndugu yangu Nsesi ulikuwa mjenzi..Kufikia kusema ati 2005 mabati yalikuwa bei hiyo. Hivi unaweza kunambia ongezeko la gharama ya Ujenzi kwa mwananchi wakati wa Mkapa hadi JK ukilinganisha na ule wa Mwinyi kuingia Mkapa. Kumbuka tu Mwinyi aliondoka Dollar 1 ikiwa Tsh 500, nailifkia Tsh 1000 within 6 years, na aliondoka tayari tumegonga 1100. Sasa nambie mwananchi mkulima ambaye mazao yake yameshuka bei atalipa kiasi gani cha Tsh kwa mali ile ile aliyokuwa akinunua wakati wa Mwinyi.Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, pamoja na kuibuliwa kwa uchafu wakati wa utawala wake ukweli unabaki pale pale mengi mazuri.
Wakati anaondoka madarakani bundle moja ya bati tulinunua 87,000/= lakini ilipofioka January 2008 ilishafika 280,000/=, nauli za daladala zilisimama kwa miaka yake yote ya utawala katika 100/=; haya ndiyo mambo sisi watu wa kawaida tunayoyaangalia;
Wakati wa Mkapa tulikuwa tuki budget, leo hii haiwezekani, tumebaki kuishi kwa matumaini tu.
Sio sahihi kabisa kumbeza mzee huyu kwamba hajafanya kitu, hapana amefanya makubwa kuliko hayo mabaya.
Kwanza mikataba ya madini ilianzia kwake, tuwe wakweli, IPTL nani alikuwa waziri wa madini na nishati na nani alikuwa rais!!!!
Mwacheni mzee wa watu apumzike.
Hilo jina ungeongeza herufi moja tu ningekupa mji!Sema Mkapa sema, Maana Watanzania hatuna tunalolijua ila kulaumu, hao wanaomlaumu waulize tangu wempata akili za UTU UZIMA nini cha maana ambacho wakifa leo wataacha kama kumbukumbu hata kwa ngazi ya familia zao acha ngazi ya Taifa. Ni wapiga mbija hao watacheza wenyewe, hawana lolote wachimba Chumvi hhhhhhaaaaaaaaaaaaaooooooooooooooo!!!!!!!!!!!!! mmmmmhhhhhhhhh!!!!!!!!!!!
Kama isingekuwa tamaa (bila shaka kutokana na kuwa na washauri wabovu), huyu jamaa alifanya mambo mazuri mengi kwa maendeleo ya nchi. Mpaka sasa sielewi kwa nini alikubali kununuliwa na makaburu walioitwaa NBC yetu. Sijui ilikuwaje pia akapata kichaa cha kutumia vibaya madaraka yake na kununua Kiwira. Ukiondoa dosari hizo na kiburi chake cha Kimachinga, alifanya vizuri.
hii si ya kumsifiaa Mkapa, kwani yote haya yalikuwa ni mapendekezo ya world bank, iwe hiyo TRA au hiyo TANroads, kwamba baada ya kutoa mikopo ya kujenga barabara, walitushauri kwamba sasa tuzi maintain, na inapowezekana tujenge, wenyewe, na thoery rahisi or facts ni kwamba kuna kodi ya matumizi ya barabara ambao road users wanatozwa na hiyo inakatwa kwenye mafuta unapo nunua, sasa kwa fungu kama hilo halfa bado usiweze kujenge barabara, utakuwa ni mzito wa akili, na system hii inatumika duniani kote, hususana kwa nchi zenye nidhamu ya matumizi ya fedha, na world bank waliweka mtu wao pale tanroads ili nidhamu iwepo.Jamani Mkapa leo ni mnyonge, myonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.
Mkapa pamoja na kufanya makosa mengi ambayo inaelekea "alijisahau", kuna mengi vilevile aliyafanya mazuri kabisa.
Kosa kubwa la Mkapa ni kuingia tamaa,watu wanaomfahafu vizuri wanashindwa kueleza ibilisi huyu katoka wapi, maana Benjamin hakuwa na unyonge huo.
Kati ya makubwa yaliyofanyika na yatendelea kuliendeleza Taifa hili ni Restructuring ya Ukusanyaji kodi na kuanzisha TRA.Tusisahau kuwa Idara ya Kodi na Mapato wakati huo ilikuwa inakusanya around 15-25bil kwa mwezi.TRA ilipoingia ikaanza kukusanya over 150bil hadi 200bil.Haya si mambo madogo.Kabla ya mabadiliko haya wafanyakazi serikalini walikuwa wanyonge kwa mishahara midogo leo suti na mashangingi kila kona.
Vile vile mafanikio makubwa ya Mkapa ni kule kuRestructure Idara ya ujenzi wa Barabara na kuanzisha TANROADS.Miaka ya kabla ya hapo ilikuwa haingii akilini hata kwa viongozi wakuu kuwa ujenzi wa barabara ni lazima ufanywe na makampuni ya nje na kwa hela za nje.
Leo kwa hela zetu ni kawaida naimeingia akilini kuwa tunaweza kujenga barabara zetu kwa HELA ZETU WENYEWE. Haya ni mabadiliko makubwa katika fikra za watanzania na kiutendaji.
Pamoja na mafanikio haya namhurumia sana Mzee Mkapa maana katika awamu yake kukaingia CONSPICUOUS MORAL DECAY AND CONSUMPTION katika uendeshaji wa Serikali na hata Chama.
Sasa hivi si wakati wa kulia lia, Watanzania ni waelewa na wengi wanahuruma.Kuomba radhi wananchi bado liko katika uwezo wa Mkapa.
Akifanya hivyo pengine atarudisha heshima yake na kusaidia kuendeleza yale mazuri mengi aliyoyajenga.
Mkuu wangu Nyerere alinunua kiwanja, Akajenga msingi wa nyumba ya vyumba sita.. Mwinyi yeye kaja kubomoa msingi wa mwalimu na kuuweka kwa ajili ya jengo la ghorofa kwa sababu haulingani na wakati,
Mkapa kuingia akajenga nguzo za jengo hilo zikasimama kwa miaka mitano ya kwanza ua ujenzi, kisha akaingia tamaa akaanza kuuza matofali, mabati, nondo na kwa makusudi hata kubadilisha title deed kuwa chini yake. JK amekuja na nguvu zote kujenga juu ya nguzo za Mkapa onlt to find out kwamba nguzo hizo haziwezi kupeba uzito wa jengo. Wataalam wanasema nguzo hizo hazifai, zibomolewe tuanze upya..Naye kwa hasira akijua wazi nyumba sii yetu tena.. Kaamua kuipiga bei kwa kubadilisha title deed..
Sasa mimisielewi haya maendeleo ya kia Mkpa ni yapi haswa kuona nguzo za gofu letu reefu mfano wa Twin Tower zimesimama au nini haswa..
Sema Mkapa sema, Maana Watanzania hatuna tunalolijua ila kulaumu, hao wanaomlaumu waulize tangu wempata akili za UTU UZIMA nini cha maana ambacho wakifa leo wataacha kama kumbukumbu hata kwa ngazi ya familia zao acha ngazi ya Taifa. Ni wapiga mbija hao watacheza wenyewe, hawana lolote wachimba Chumvi hhhhhhaaaaaaaaaaaaaooooooooooooooo!!!!!!!!!!!!! mmmmmhhhhhhhhh!!!!!!!!!!!
mfano wako unanikumbusha hadithi au tukio la tajiri moja, yeye alikuwa na 10millioni tshs wakati huo akajenga nyumba ya 1tshs, sasa sijui huyu mtu utasema alikuwa na akili au ni basi tu change ilibaki ndio akajenga nyumba.Pamoja na mabaya yote aliyofanya Mheshimiwa Mkapa kuna mazuri yake pia. Alikuwa rais wa pekee Tanzania kujenga barabara kwa kodi za watanzania, alilipa madeni ya nje ambayo nchi ilikuwa inadaiwa, alihakikisha uchumi wa nchi unakuwa na inflation inabaki a single digit. Uwanja wa mpira pia ni kipimo kizuri wamepita viongozi hapo kabla lakini uwanja wa mpira wa kisasa haukujengwa.
Pretty,
Kweli huyo Mtakatifu atasemwa ikiwa hata Rwanda leo inatuzidi ktk maendeleo..ati tunawekwa kundi moja na Sudan, Chad jamani sii aibu hii, kisha hupendi tukisema kitu....
rejea siku aliporejea saint joseph cathedral aliposoma misa yake ya shukrani kwa mungu mkuu.
Ukiipata hiyo maneno haya ya kejeli usingaliyatamka maana hata muumba hapendezwi nayo daima.
Niambie nchi iliyowahi kumfunga rais wake wa zamani, wote wamejaribu kuwapeleka mahakamani na hamna hata aliewahi kutolewa hukum...in short though law inasema no one is above the law, hawa watu wapo na kinga kubwa...hata wakipelekwa kesi zao haziishi, au ataishia kuchukua assylum.Tanzania ingekuwa nchi ya rule of law Mkapa angekuwa lupango siku nyingi tu.