Mkapa: Yote yanayosemwa juu yangu namuachia Mungu

Sasa huu ndio uongo ulizidi kifani maanake sijui kama ndugu yangu Nsesi ulikuwa mjenzi..Kufikia kusema ati 2005 mabati yalikuwa bei hiyo. Hivi unaweza kunambia ongezeko la gharama ya Ujenzi kwa mwananchi wakati wa Mkapa hadi JK ukilinganisha na ule wa Mwinyi kuingia Mkapa. Kumbuka tu Mwinyi aliondoka Dollar 1 ikiwa Tsh 500, nailifkia Tsh 1000 within 6 years, na aliondoka tayari tumegonga 1100. Sasa nambie mwananchi mkulima ambaye mazao yake yameshuka bei atalipa kiasi gani cha Tsh kwa mali ile ile aliyokuwa akinunua wakati wa Mwinyi.

Wakati wa Mkapa tulikuwa tuki budget kitu gani? maanake nakumbuka hadi anaondoka serikali inadaiwa fedha za walimu na wafanyakazi kibao wa halmashauri za wilaya na mikoa. hautuna shule Zahanati, maji, Umeme, Usafiri reli ya kati mwisho Dodoma..ATC chini ya SA imekwisha, Tanesco hoi bin taaban karibu kabisa kutaifishwa. Bandarini ndio hapasemeki Mombasa took over, tunapigwa VAT za asilimia za ajabu, exemption kwa matajiri na vigogo yaani hata haisemeki. hata uwekezaji ktk hisa ulikuwa ktk sigara na bia tu.. hakuna hata kitu kimoja kilichokuwa kikipanda ktk soko letu zaidi ya dhahabu ambayo hatukuwa na hisa hata moja. Kazi kubwa alikuwa nayo JK ni kujaribu hata kurekebisha moja na ameshindwa hivyo utawala wake wote umeonekana bure kwa sababu ya Mkapa.

Mradi wa IPTL ulianzishwa wakati wa Mwinyi lakini mkataba ulipita wakati wa Mkapa. soma report inayohusu IPTL utaelewa kilichofanyika.
 
Sema Mkapa sema, Maana Watanzania hatuna tunalolijua ila kulaumu, hao wanaomlaumu waulize tangu wempata akili za UTU UZIMA nini cha maana ambacho wakifa leo wataacha kama kumbukumbu hata kwa ngazi ya familia zao acha ngazi ya Taifa. Ni wapiga mbija hao watacheza wenyewe, hawana lolote wachimba Chumvi hhhhhhaaaaaaaaaaaaaooooooooooooooo!!!!!!!!!!!!! mmmmmhhhhhhhhh!!!!!!!!!!!
 
acjifanye mlokole-mungu saa hizi!! too lateeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
Hilo jina ungeongeza herufi moja tu ningekupa mji!
 
Ili tuwe wakweli kuna mabadiliko yalitokea katika enzi (regime) ya mkama rais ya w awamu ya tatu ya nchi yetu (chaguo la Nyerere).

Kikweli huyu bwana wakati anaingia madarakani hakuwa mtu mwenye makuu zaidi ya kuwa mtu aliyeonekana kama makini na historia ya utendaji kazi wake ulimlinda kabisa na ndipo bila kamapen watanzania wengi tulikubali kumuita (Mr Cleana) yaani mtu msafi.

Tatizo ni sehemu aliyo toka ki jiografia inasemekana kwamba huko kwao ni kabila dogo sana na wana tabia ya asili ya kupenda sana sifa hata za kijinga.

Kwa kufahamu hilo waendaji wake wa karibu walitumia mwanya huo kujinufaisha kwa kumshauri vibaya kupitia sifa za uongo walizompa. Kwa kuwa kwa asili wanapenda sifa haikuwa rahisi kwake kuwakwepa wajanja aliowachagua kama wassaidizi wake akiwemo, Basil, Andrew frederick na wengine wengi kama manavyo kumbuka.

Ushahidi uko wazi kwamba yeye kama kiongozi wa awamu yatatu ya uongozi katika taifa letu ndiye aliye fanga kashfaa za kipuuzi kuliko kiongozi yeyote katika taifa letu hili lisilo komaa.

Mifano rahisi niliyonayo ni miwili, nayo ni :

1.Kurudishwa kwa mgodi wa Kiwira Serikalini.

2.Skesi lukuki zinazo wakabili wasaidizi karibu wote wa iliyokuwa executive committee yake (Baraza la mawaziri).

Ni hivyo unfafiki na madaraka makubwa waliyonayo viongozi wetu ndio unaomfanya awe hana kesi kwa sasa vinginevyo tungekuwa na utawala wa kwelikweli wa sheria MKAPA ana kesi yakujibu mahakamani sambamba na wasaidizi wake.

Ndio maana wananchi wanaona uwepo wa kesi zinazowahusu kina Mramba mahakamani ni kama mchezo wa kuigiza kwa sababu, HUWEZI Kushtaki shingo ukaacha kichwa.
 

MzeePunch,
Sidhani ilikuwa ni tamaa. Kwa wale wanaomfahamu Mkapa wanasema alikuwa na hulka ya kifisadi lakini hakuwa na opportunity. Aliipata alipoingia Ikulu. Alikuwa akiwaambia marafiki zake kuwa role model yake ni arap Moi. Nikajiuliza, unawezaje kufanya kazi na Julius na kuadmire mwizi na muuaji kama Moi? Alipoingia mamlakani alikuwa akimwambia Yona wafanye madudu. Na kweli waliyafanya.
 
hii si ya kumsifiaa Mkapa, kwani yote haya yalikuwa ni mapendekezo ya world bank, iwe hiyo TRA au hiyo TANroads, kwamba baada ya kutoa mikopo ya kujenga barabara, walitushauri kwamba sasa tuzi maintain, na inapowezekana tujenge, wenyewe, na thoery rahisi or facts ni kwamba kuna kodi ya matumizi ya barabara ambao road users wanatozwa na hiyo inakatwa kwenye mafuta unapo nunua, sasa kwa fungu kama hilo halfa bado usiweze kujenge barabara, utakuwa ni mzito wa akili, na system hii inatumika duniani kote, hususana kwa nchi zenye nidhamu ya matumizi ya fedha, na world bank waliweka mtu wao pale tanroads ili nidhamu iwepo.
tra nayo ni conditions za world bank ambyo ilikwenda na kubadili mfumo wa tra, toka idara ya serikali kuwa chombo tofauti ilikuweza kutoa maslahi bora zaidi kwa wafanyakazi, hivyo utaona ni wazi kabisa mzee alikosa ubunifu wake binafsi.
kso lingine la kimsingi ni kuuza nbc, bila kujua madhara yake, jingine ni kushindwa kuendeleza TANESCO na miradi ya umeme kwa jumla, maana akili yake ilikuwa haina akili, jingine la kimsingi alilokosea na ndio maana ya kuweweseka kwake kutokana na laana za madini , ni hiii mikataba ya madini tunayo ambulia %3 as royality wakati kinachobaki na job creation ni kwa wawekezaji, sasa ukiongezea na ubinafsishaji holela wa ATC kwa makaburu, kiwira, uuzaji wa hovyo kabisa wa nyumba za serikali, nk utaona huyu mtu alienda kuharibu nchi badala ya kuitengeneza. na laana hiyo ya watanzania itaendelea kumtafuna mpaka hapo atakapo omba msamaha.
 
Mkuu wangu Nyerere alinunua kiwanja, Akajenga msingi wa nyumba ya vyumba sita.. Mwinyi yeye kaja kubomoa msingi wa mwalimu na kuuweka kwa ajili ya jengo la ghorofa kwa sababu haulingani na wakati,
Mkapa kuingia akajenga nguzo za jengo hilo zikasimama kwa miaka mitano ya kwanza ua ujenzi, kisha akaingia tamaa akaanza kuuza matofali, mabati, nondo na kwa makusudi hata kubadilisha title deed kuwa chini yake. JK amekuja na nguvu zote kujenga juu ya nguzo za Mkapa onlt to find out kwamba nguzo hizo haziwezi kupeba uzito wa jengo. Wataalam wanasema nguzo hizo hazifai, zibomolewe tuanze upya..Naye kwa hasira akijua wazi nyumba sii yetu tena.. Kaamua kuipiga bei kwa kubadilisha title deed..
Sasa mimisielewi haya maendeleo ya kia Mkpa ni yapi haswa kuona nguzo za gofu letu reefu mfano wa Twin Tower zimesimama au nini haswa..
 

Hahahaa,

Mkandara,

Bonge la analogy!
 

Chamaana tulichokifanya ni kumchagua yeye kama Rais tukitegemea kusaidiana nae ktk kulete maendeleo ndani ya nchi na si kumbukumbu za kifisadi kama za kwake.
Sina uhakika kama wawacheka wachimba chumvi au wajicheka mwenyewe..! Unanipa mashaka sana..!
 
mfano wako unanikumbusha hadithi au tukio la tajiri moja, yeye alikuwa na 10millioni tshs wakati huo akajenga nyumba ya 1tshs, sasa sijui huyu mtu utasema alikuwa na akili au ni basi tu change ilibaki ndio akajenga nyumba.
 
Binadamu hatuna shukrani, Nyerere mnamsema, Mwinyi mnamsema, Mkapa naye mnamsema...........Kikwete ndio kabisa hata muda wake haujaisha mshaanza kumsema.

Kwa mwendo huu Tanzania hata tupate rais mtakatifu, atasemwa tu.
 
Pretty,
Kweli huyo Mtakatifu atasemwa ikiwa hata Rwanda leo inatuzidi ktk maendeleo..ati tunawekwa kundi moja na Sudan, Chad jamani sii aibu hii, kisha hupendi tukisema kitu....
 
Pretty,
Kweli huyo Mtakatifu atasemwa ikiwa hata Rwanda leo inatuzidi ktk maendeleo..ati tunawekwa kundi moja na Sudan, Chad jamani sii aibu hii, kisha hupendi tukisema kitu....

Mkandara tatizo watu tunasema, vitendo hakuna. Tunaishia tu kulalamika online, kwa mwendo huu lazima tupitwe tu na Rwanda.
 
Pretty,
Tufanye kitu gani maanake hata nyie hamtoi ushauri kwa wananchi la kufanya..Kisha nyie msolaumu muwe mstari wa mbele kuwaonyesha wananchi mfano..Tutafuata wengi tu maanake sasa hivi viungo vyetu zimeganda..
 
rejea siku aliporejea saint joseph cathedral aliposoma misa yake ya shukrani kwa mungu mkuu.

Ukiipata hiyo maneno haya ya kejeli usingaliyatamka maana hata muumba hapendezwi nayo daima.

- Mkuu FDR kwa kawaida wewe huwa ni mmoja wa members wachache sana humu ambao nina heshima nao sana,

- Unajua mkuu kuna waumba wengi, wa kwangu mimi hapendezewi na unafiki wa kuwaibia wananchi na kuwaacha masikini huku wewe ukijenga mahekalu na kuanzisha mabiashara ya ajabu kwa migongo ya hao hao masikini!

Respect.


FMEs!
 
Tanzania ingekuwa nchi ya rule of law Mkapa angekuwa lupango siku nyingi tu.
 
Tanzania ingekuwa nchi ya rule of law Mkapa angekuwa lupango siku nyingi tu.
Niambie nchi iliyowahi kumfunga rais wake wa zamani, wote wamejaribu kuwapeleka mahakamani na hamna hata aliewahi kutolewa hukum...in short though law inasema no one is above the law, hawa watu wapo na kinga kubwa...hata wakipelekwa kesi zao haziishi, au ataishia kuchukua assylum.
 
Mavitu yamepanda bei sana from 2005 mpaka sasa, watanzania mnabaki kimya tu, mnang'ang'ania oo wapiganaji 11 sijui wakina nani, hao wapiganaji wanasema nini kuhusu inflation Tanzania.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…