Mkandarasi Yapı Merkezi anayejenga Reli ya SGR atoa ufafanuzi taarifa za kushindwa kuwalipa wafanyakazi wake raia wa Uturuki

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,814
11,991
TAARIFA KWA UMMA​
UFAFANUZI WA TAARIFA ZINAZOSAMBAA ZIKIHUSISHWA NA SERIKALI YA TANZANIA KUSHINDWA KUMLIPA MKANDARASI YAPI MERKEZI NA KUPELEKEA KUSHINDWA KULIPA MISHAHARA WAFANYAKAZI WA KITURUKI

Dar es Salaam, Tarehe 15 Agosti 2023

Kampuni ya YAPI MERKEZI inayofanya ujenzi wa reli ya yenye kiwango cha kimataifa (SGR) kati ya Dar es salaam - Isaka inapenda kutoa ufafanuzi wa taarifa zilizotolewa kupitia mitandao ya kijamii na kituo cha televisheni nchini Uturuki, juu ya changamoto ya wafanyakazi wa kituruki wanaoshiriki kwenye ujenzi wa reli ya SGR chini ya Mkandarasi Kampuni ya Yapi Merkezi kutokulipwa mishahara kwa zaidi ya miezi saba (7) ikihusishwa na Serikali kushindwa kumlipa mkandarasi (YAPI MERKEZI).

YAPI inapenda kuutarifu Umma wa Watanzania na Raia wa Kigeni wanaoshiriki kwenye Mradi wa SGR taarifa hizo si za kweli. Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC) haidaiwi na Yapi Merkezi na imelipa hundi zote zilizothibitishwa kwaajili ya kazi zilizokwisha tekelezwa na kukidhi viwango vya ujenzi wa reli ya SGR.

Hadi kufikia mwezi juni 2023 Serikali imelipa jumla ya Shilingi Trilioni 8.13 kwa YAPI Merkezi ambapo malipo yake kwa kila kipande ni kama ifuatavyo: Dar es salaam - Morogoro hundi 60 zenye jumla ya Shilingi Trilioni 2.55, Morogoro Makutupora hundi 59 sawa na Shilingi Trilioni 3.75, Makutupora- Tabora hundi 10 sawa na Shilingi Billioni 883.25, Tabora - Isaka hundi 4 na malipo ya awali sawa na Shilingi Bilioni 951.6.

YAPI inaomba radhi kwa changamoto zilizojitokeza na kuleta taharuki kwa watanzania.

Kampuni ya Yapi Merkezi kwa kushirikiana na Shirika la Reli Tanzania inaendelea kutatatua changamoto zilizojitokeza na kuhakikisha mradi wa SGR unatekelezwa na kukamilika kwa wakati.

Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano YAPI MERKEZI
Amisa Juma

scan0008_page-0001.jpg

Pia soma > Waturuki wanaojenga Reli ya SGR wapo katika mgomo, inadaiwa haijalipwa fedha zao
 
Kampuni ya Yapi Merkezi kwa kushirikiana na Shirika la Reli Tanzania inaendelea kutatatua changamoto zilizojitokeza na kuhakikisha mradi wa SGR unatekelezwa na kukamilika kwa wakati.

KAMU BİLDİRİMİ
TANZANYA HÜKÜMETİNİN MÜTEAHHİT YAPI MERKEZİ'NE ÖDEME YAPMAMASI VE TÜRK ÇALIŞANLARINA ÖDEME YAPMAMASINA İLİŞKİN BİLGİLERİN AÇIKLANMASI

Darüsselam, 15 Ağustos 2023

Dar es Salaam - Isaka arasında dünya standartlarında bir demiryolu (SGR) inşa eden YAPI MERKEZİ şirketi, inşaata katılan Türk işçilerinin meydan okumasıyla ilgili olarak Türkiye'de sosyal ağlar ve bir televizyon kanalı aracılığıyla verilen bilgilere açıklık getirmek istiyor. Yüklenici Yapı Merkezi Şirketi'ne bağlı SGR demiryolunun yedi (7) ayı aşkın bir süredir maaşlarının ödenmemesi, Hükümetin yükleniciye (YAPI MERKEZİ) ödeme yapmamasına bağlıdır.

YAPI, SGR Projesine katılan Tanzanyalılar ve Yabancı Uyrukluların kamuoyuna bilgilerin doğru olmadığını bildirmek ister. Tanzanya Demiryolları Kurumu (TRC) aracılığıyla Hükümet, Yapı Merkezi'ne borçlu değildir ve yürütülen ve SGR demiryolu inşaat standartlarını karşılayan işler için tüm doğrulanmış çekleri ödemiştir.

Haziran 2023'e kadar Devlet YAPI Merkezi'ne toplam 8,13 Trilyon Şilin ödedi ve her bir parça için ödeme şu şekilde: Darüsselam - Morogoro toplam 2,55 Trilyon Şiline karşılık gelen 60 çek, Morogoro Makutupora 3,75 Trilyon'a eşit 59 çek Şilin, Makutupora - 883,25 Milyar Şiline eşit Tabora 10 çek, 951,6 Milyar Şiline eşit Tabora - Isaka 4 çek ve ön ödeme.

YAPI, Tanzanyalılar için ortaya çıkan ve kafa karışıklığına neden olan zorluklardan dolayı özür diler.

Tanzanya Demiryolları ile işbirliği içinde olan Yapı Merkezi şirketi, ortaya çıkan zorlukları çözmeye ve SGR projesinin zamanında uygulanmasını ve tamamlanmasını sağlamaya devam ediyor.

İlişkiler Birimi Başkanı YAPI MERKEZİ
Amisa Cuma
 
Back
Top Bottom