Mkakati wa Kumuhujumu JK na Lowassa

Siasa chafu ndio hizi. Tusisubiri kuona na kusikia mengine. Sasa pengine kila mtu anafikiria kummaliza mwenzake. Lakini in real fact URAIS ni kama cheo chochote cha kidini ambapo mtu anatakiwa kuwa loyal kwa Mungu na wanadamu wenzake. God bless Kikwete.
 
Ama kweli!!! UONGO MWINGINE UNAHITAJI UJASRI WA KIFISADI KAMA WAKO KKUTUNGA NA KUTKATA WATU WAUAMINI! NINAMASHAKA NA UJAZO WA UBONGO WAKO, TUKIUPIMA NA WAKUKU, WAKUKU UNAWEZA KUWA MKUBWA. POLE SANA, MTAHANGAIKA SANA!

nape mbona unapenda sana matusi na kebehi, si ukanushe kiungwana mkuu,sasa hapa mwenye ubongo wa kuku nani kama si wewe!NAPE huwezi kujenga hoja za kimantiki!
 
waache tu wawahujumu, mbona unawatetea EL na JK wameisha leta damage kubwa sana nchi hii..lets them GO....
 
Mkuu zomba kayasema haya hapa chini:

Faiza, ahsante sana kwa kunipigia simu na kunitaka nitoe maoni yangu katika hili. Kwa kuwa sina muda mrefu wa kuwepo jamvini ntaingia moja kwa moja kwa nnayoyaona,

Nampa hongera hapo juu aliesema "Lowassa at work". Hivi mnafikiri toka Lowassa alipowachia madaraka ya Uwaziri mkuu alikuwa kakaa tu bure, anangoja nini hatma yake? Hapana. Hajakaa bure.

Lowassa alikuwa yuko "very busy" usiku na mchana na hakuwacha niwa au hila yoyote au hata kanukta kadogo kukapitia katika kujua ni vipi atarudisha heshima yake. Haya ni matokeo ya kazi yake kubwa aliyoifanya, na anarudisha heshima yake kwa njia yoyote anayo ijua. Kaanza na kawaweka sawa waandishi, akawawweka sawa makada, akwaweka sawa mawaziri (hata Sitta kwa sasa yupo nae), usishangae ukisikia na Anna Makinda nae ni mdau.

Tishio kubwa kuliko yote katika kurudisha hadhi yake ni mtu mmoja tu, nae ni Membe, huyu Bernard Membe. Kwa kuwa Membe ana akili kupita kiasi na anafata nyayo za Kikwete, kwa kuanzia kajijenga nje ya nchi ambapo anajua kuwa humu ndani hata afanye nini, nje kama hawamtaki hatofanikiwa. Membe kwa sasa ndio kikwazo cha Lowassa, goli la Lowassa si kurudisha hadhi tu, kurudisha hadhi na kuujulisha uma kuwa yeye ni zaidi ya waziri mkuu. Na menbe gali lake ni kuwa rais wa nchi hii, na kwa kichwa na maarifa aliyokuwa nayo anaweza kuupata urais kiulaini kabisa, tatizo ni maskini na hana fedha na Lowassa anatumia fedha kuhakikisha anakubakika.

Hayo ni maoni kwa yangu kwa ufupi. Samahani jamani, huku nilipo inabidi nialale mapema niamke mapema tunatumia Generator la umeme na imebaki dakika tano kuzimwa na mimi sijamaliza mengi na dakika dakika zina yoyoma. Maasalaam.

Faiza, inshalla naja mjini week end inayo kuja, nakuja kula chakula cha mchana kwako, Ijumaa baada ya salaa, naomba el forno.

Huyu Mheshimiwa ana-comment hivi kutokana na kauli ya zomba hapo juu:

Asante Mungu kwa kunifanya nizaliwe nje ya Uislam.

Hivi kweli kuna uhusiano hapo?! au ni mimi ambae nimeachwa njia panda au ni jirani hapa!!
 
Nimesoma kila post inayoelezea hujuma hii na naishia kuamini kuwa huu ni mkakati wa Lowassa na team yake kuwachafua wale aonao ni vikwazo kwenye kufanikisha nia yake ya kugombea urais 2015.

Lowassa anajua fika kwamba kizingizi kilicho mbele yake ni Mh Benard Membe pekee.

Hivyo Jitihada nyingi zaelekezwa kummaliza kisiasa ili kufanikisha nia yake na ndio maana sishangai wanavyojaribu kumgombanisha na JK jambo ambalo kwao litakuwa ni faraja japo naona ni gumu kidogo kutokea.

Simlaumu Lowassa kwa kufanya hivi kwani akili zake ndivyo zinavyomtuma japo wanaomfahamu Membe wanajua kuwa ubongo wake hauna matundu kama wa lowassa hivyo kujua nini anafanya.

CCM imejaa mapoyoyo wengi sana na lowassa ni mmoja wao.

Kama ni kutoa Rais basi naamini kabisa afaae ni Membe vinginevyo ni bora tukawapa upinzani na wao wakajaribu kuongoza nchi.

OTIS

Nakubaliana na wewe kwa 100%! Na ni kweli kabisa kwamba Lowassa anamuogopa zaidi Membe kuliko anavyowaogopa akina Sitta. Ni rahisi kuwaingiza kundini akina Sitta kwa kuwaahidi ki2 huko mbeleni kuliko kumwingiza Membe kwa staili hiyo. Membe kuwa kundini ni atake mwenyewe lakini sio kwa kumrubuni kwa chochote. Na wanaemuogopa Membe sio Lowassa pekee, bali hata kambi ya akina Mwakyembe. Kambi hii nayo inamuogopa Membe kuliko Lowassa. Naamini, bila shaka yoyote kwamba hata ile simulizi iliyotungwa na Mwakyembe ya kwamba anataka kuuawa na Al Shabab ililenga kumfitinisha Membe na wale anaowaamini. Inabidi uwe makini sana kuweza kuelewa lengo la hekaya ile ya Mwakyembe!
 
memba na lowasa wote hawafai kuongoza nchi hii.......membe hana tofauti na kikwete...lowasa ni mwizi mkubwa
 
Kinachoshangaza ni Salim Ahmed Salim pamoja na kuaminika ni mtu safi ni kama hayupo kabisa! Hatajwi! Sijui kwanini hatajwi!
Huyu ni liablity kwa watanzania na sio assets,nilikuwa mtoto enzi hizo leo mtu mizma, nikimuadmile sana huyu mzee wakti huo namuona kwenye magazeti ya Sunday News na Daily news bonge ya handsome man na statesman. Hakuna mtu kaniangusha katika historia ya Taifa hili kama huyu jamaa.Hata yesu aliwachapa viboko walio ingia kufanya biashara ndani ya nyumba ya baba yake.

Huyu jamaa ni mwoga sana kitu ambacho ni aibu kwa mtu alie amua kuwa mwanasiasa na statesman.Kwa kuwa leo hii Nyerere au Mandera hata Rais wa kike wa Brazil wasingekuwa viongozi wa kuheshimka kama wasingekuwa vichwa ngumu kubishana na mfumo,ili kusimamia vile ambavyo wao wanaamini kuwa ni haki kwa jamii.Leo hii Rais huyo Mwanamke amezindua sheria ya kuwashitaki viongozi wakuu wa kijeshi na usalama walihousika na unyanyasaji na mateso ya kidhalimu wakati wa tawala zilizopita.Sheria hiyo iliasisiwa na Rais aliyepita Rula Da Silva,ambayo imekuja kukamilisha na Mwanamama Rais huyu wa kike wa Brazil,kwa kuwa enzi hizo akiwa Mwanaharakati yeye nae alipitia mateso ya watawala hao wakijeshi na usalama.Kwa kuwa kanuni ya What goes around comes around usubilia muda kufanya kazi.

Kwa huyu mpotezee hana jipya kwa kuwa angekuwa anawajali watanzania angemuenzi Mwalimu Nyerere aliyempa nafasi ya upendeleo wakishirikiana na karume toka ujana wake,leo anaona wazi minyukano ya watoto wadogo waliokuja nyuma yake, wakiyumbisha TAIFA uku kakaa kimya kajifungia kwenye NGO ya Mwalimu eti ana muenzi Mwalimu kwa Instutional inayotoa huduma kwa watanzania wasio dhidi Millioni huku akiwaacha Watanzania Millioni Alobaini na Mbili wakiwa na kelele zisizo isha.

Hata kama ni Udiplomasia du basi hauna maana,matokeo yake unamuongezea bifu na Marais wastaafu kwa kuwa ni kingunge kwenye kamati ya Ibrahimu Mo [Presidential Award] hivyo tuhuma za wengine kukosa huku wao wanaona wanadeserve.Hawa ndio wale Mwalimu aliosema wametumwa na kijii kwenda kutafuta chakula cha kijiji walipofika uko kuliko na chakula wakaloea na wakaamua kuwa wasaliti wa jamii kimtindo.

Anyway imekwisha toka,sidhani kama kuna Watanzania wanacho cha kumkumbuka kwa sasa kwa kuwa hakuna alicho acha kama Legacy ndio maana hata wewe mwenyewe unauliza yuko wapi?,labda aandike kitabu tena cha kiswahili,manake Udiplomasia unaweza kumfanya akaandika kwa kiingereza hivyo ujumbe ukawa tena si kwa watanzania wenzie.
 
jaribu kuulizia kwanza kama ipp ni ya mengi?
au azam ni ya bakhresa.
au microsoft ni ya bill gates.
 
Ama kweli!!! UONGO MWINGINE UNAHITAJI UJASRI WA KIFISADI KAMA WAKO KKUTUNGA NA KUTKATA WATU WAUAMINI! NINAMASHAKA NA UJAZO WA UBONGO WAKO, TUKIUPIMA NA WAKUKU, WAKUKU UNAWEZA KUWA MKUBWA. POLE SANA, MTAHANGAIKA SANA!
"chloroquine ni chungu lakini ni dawa"

Nape tunaomba usianze kutuletea "UNAFIKI" wako hapa.Uliisha tukana wananchi Mwanza kwamba utawashikisha Ukuta.Na tunajua unavyohaha ndani ya chama kutokana na unafiki wako.Tuliisha kuonya humu jamvini uachane na siasa zako hukusikia.Na bado utatapatapa sana kama kuku wa "MDONDO"
 
WAPROTESTANT na WAISLAMU wa NCHI hii hawataki MKATOLIKI mwingine awe RAIS. Mwalimu na Mkapa wanatosha kwa sasa. Chaguo la Waprotestanti ni Lowasa. Tunagawana madaraka na vyeo kwa DINI na madhehebu yetu sasa.

Mie ni Mlutheran na sitaki kumsikia Lowassa kamwe.
Simchagui mtu kwa dini yake ila kwa uadilifu na uwezo wa kiuongozi sifa asizokuwa nazo Lowassa.
OTIS
 
Du Kampeni imeshaanza kwa Kishindo, Jana nilimsikia mheshimiwa Akitangaza Ushindi toka SINGIDA, Naona 2015 Mchuano utakuwa Mkali sana, Wapambe wameingia Kazini, Mitandao inasukwa watu wanapewa sifa hewa,
Naomba niwakumbushe watanzania wenzangu, Tunataka mtu au Sifa? (JKN -1995).
Tusijadili watu, tujadili sifa anazopaswa kuwanazo rais ajaye, MABADILIKO gani tunataka kuyaona TANZANIA Katika Awamu ijayo?
 
John, ninao ushauri mdogo kwako, siasa hizi za kutunga hadithi zimepitwa wakati sana, sasa ukindelea nazo itabidi uingie kwa jina lako ili tukujibu kwa uongo wako, ukishindwa nitakusaidia kuweka jina na picha, then tuongee kama wanaume na si kutunga hadithi za kipuuzi kama hizi halafu unadhani umejificha kama mbuni. Nimeshangaa kama na M naye umemuinbiza kwenye hili badala ya yeye kufanya kazi za ofisi ya Makamu, ambazo kwakweli ni nyingi na zinahitaji muda...... Be carefull na uongo usiokuwa na mashiko...


Wana JF,

Baada ya kikao cha NEC dodoma Mh MEMBE alimwaaita wajumbe wa NEC wafuatao na Kufanya NAO kikao Nyumbani kwake wajumbe hao ni

NAPE NNAUYE
Capt CHILIGATI
LUSINDE maarufu kwa Jina kibajaji
Makongoro Nyerere
Mzee Samweli sita ambae alifatwa nyumbani kwake akiwa amejipumzisha
Ndg Wilson Mukama

Wajumbe hawa walikutana nyumbani kwa MEMBE baada ya kikao cha nec mzee sita aliwahi kutoka kwenda kupumzika baada ya SUMAYE kuongea.

Katika kikao hicho ukaandaliwa mpango madhubuti wa kupambana na kikwete kwakua hawa jamaa wanaamini Kikwete amewatosa na kuamua kujiunga na Lowasam

Makubaliano.

(1) Kutoa siri za kikwete na hapa hasa mali alizonazo Nje ya Nchi na hapa atakae fanya hii kazi ni Bwana Membe.

(2) Kutumia urafiki uliopo kati ya Membe na baadhi ya watu ndani ya idara ya usalama kufanikisha Mpango huu.

(3) Mzee Samweli Sitta aanzishe mazungumzo na CHADEMA ama CUF ili kuandaa mpango wa kujiunga na chama kimojawapo kati ya hivo viwili kwakuwa Sitta ameona kuwa hakuna njia ya kumzuia Lowassa kushinda ndani ya CCM.

(4) Kutokana IMANI na matumaini ambayo NAPE aliyokuwa nayo baada ya mkutano wa JK na wabunge wa CCM Dodoma, NAPE alimfata Bwana Mwigulu akiwa na Chiligati, Nape amedaiwa kumwambia Mwigulu "Bwana MKUBWA (JK) ameishaingia line ameelekea KIBLA tusaidie kesho tummalize huyu Lowassa, mzee anataka sisi katika kamati kuu tuanzishe, kaka usituangushe"

Baada ya hili kutotokea NAPE amedai atahakikisha analipiza kisasi kwa kuanika SMS walizo-chat na JK, kuonyesha JK alikuwa anamtuma.

Mpango wao unalenga kwanza kuonyesha JK haaminiki, Pia wanadai kwakuwa amewasaliti watamuanika.

PIA Mbunge Ismail Aden RAGE akiwa uwanja wa Ndege wa Tabora Juzi katika VIP akiwa amefatana na Mbunge wa Bukene Selemani Zedi alinukuliwa akisema, "Nimeongea na Mzee Sitta amesema njia pekee ya kupambana na Lowassa na Kikwete ni Nje ya CCM, mimi najiandaa kuondoka" haya ni maneno ya sita ambayo Rage aliyanukuu kwa Selemeni Zedi na Rage akasema Nadhani mzee Sitta yupo Sahihi acha aende JK na Lowassa wote ni Mafisadi.

Wana JF, chanzo cha habari hizi ni mtu aliyekuwa katika vikao hivo vya Dodoma na Membe na Nape walikutana Protea wakiwa na Jack Gotham na Balozi wa heshima wa Comoro. Walikutana kuendelea kupanga mikakati, kumekuwa na Vikao vingi sana ambavyo vimeanza kufanyika, na Membe sasa na yeye anjipanga kuanza kutumia makanisa; hivi karibuni na yeye atakua na Harambee ktk kanisa Katoliki Magomeni.

Kwahiyo mnyukano CCM ndo umeanza sasa waliokuwa watu wa Kikwete sasa wanaanza mipango ya kumhujumu na kuanza kutoa siri za mali zake zilizopo Uarabuni.

Nawasilisha
 
John, ninao ushauri mdogo kwako, siasa hizi za kutunga hadithi zimepitwa wakati sana, sasa ukindelea nazo itabidi uingie kwa jina lako ili tukujibu kwa uongo wako, ukishindwa nitakusaidia kuweka jina na picha, then tuongee kama wanaume na si kutunga hadithi za kipuuzi kama hizi halafu unadhani umejificha kama mbuni. Nimeshangaa kama na M naye umemuinbiza kwenye hili badala ya yeye kufanya kazi za ofisi ya Makamu, ambazo kwakweli ni nyingi na zinahitaji muda...... Be carefull na uongo usiokuwa na mashiko...

Mlolongo wa matukio ulioainishwa na mtoa mada na majibu yako yanayoonyesha wazi kuwa unakimbia hoja,nachelea kusema kuwa hii habari ina ukweli.Mbona hoja nyingine huwa hujitokezi kujibu? Hii kitu itakuwa na ukweli.Lowasa atawatesa sanaa! Hajakutana na jk barabarani kama nyie
 
Back
Top Bottom