Mkakati: Lowassa kuhamia UKAWA

mkuu pasco labda na mwanakijiji ni hivi , hatuwezi kufukua makaburi , hii ndio siasa , hata jk alimsifu sana lowasa enzi zile lakini leo anamponda , na nakuhakikishia kwamba kelele zetu ndio zimesababisha ccm wakamtosa lowasa , hii ni nafuu kubwa sana kwa UKAWA .
 

ubarikiwe sana .
 
Tumeamua kuungana na maamuzi ya viongozi wetu wa UKAWA kumsapoti Lowasa kama mgombea uraisi kwetu ambalo tuliona haliwezekeni sasa limewezekana kumbe kwenye siasa hakuna urafiki wala uadui wa kudumu lakini bado lengo ni kuitoa ccm madarakani naamini tutafanikiwa huo ndo msimamo wangu
 
mtakufa njaa lowasa amewahonga sh.ngapi mna spidi sana za kumsafisha lakini hata mngemsafisha na omo bado uchafu uko pale pale
Nakubaliana na wewe kamanda wangu.
 
ukiona mtu anamsifu mtu mchafu kama Lowassa ujue yeye ni mchafu zaidi raisi ajaye chaguo la watanzania ni DR Slaa pekee yake hana skendo za wizi kama ccm
Nakabaliana na wewe kamanda wangu.

Teh teh teh
 
hizi komenti ingekuwa insta tungesema throw back Thursday. . (TBT) maana kuna watu wengi wataumbuka..ooh naacha siasa, najiua oohh sijui haiwezekani. Enji vijana hii imeandikwa 2014 na tunayaona leo yanatendeka hebu fungueni akili. Asante uliileta bonge la Throw back Aminia.
 
Na bado kampeni hazijaanza tayari madudu yote yashaanza fichuka, lililosemwa kweli lipo na kama halipo basi linakuja, leo hawa wa ukawa wanasema lowassa ndio anafaa ila kwa hizi comment humu naona kama vile hawajielewi
 
Teh Teh Teh....sitawaangusha, HAKUNA MTANZANIA MWENYE AKILI TIMAMU ATAKAYEMPIGIA KURA MGOMBEA WA CCM,mlivyotuibia mali za umma na kufanya ufisadi wenu huku mkilindana inatosha. KURA YETU NI KWA LOWASSA WA CHADEMA,UKAWA
 

haya hebu njoo hapa uone aibu yako.
 
Kamanda naona unampa za uso fisadi.

Teh teh teh
 
Jana : mkinipa kura nitaendeleza mazuri aliyoyafanya mh rais.
LEO: nipeni kura mm huyu rais hakuna aluchofanya zaid ya kuuangusha uchumi.maneno hayo yote yanatoka kwenye mdomo wa mtu mmoja.mhh langu jicho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…