MJUE Lowasa

kiongozi makini hatakiwi hata kutuhumiwa kwa rushwa achiambali kuitoa au kupokea.

Lowasa Hana uthubutu wa kuikemea kwasababu sio msafi.
!
Mkuu umenikumbusha kisa kimoja kwenye biblia kilihusu Mfalme, katika himaya ya Mfalme kulitokea minongono ya hapa na pale kwamba mkewe alikuwa anatembea nje ya ndoa! Mfalme alikasirishwa sana na taarifa hizo, alikata shauri ya kumtariki mkewe.

Haikuchukua muda Mfalme kampa taraka mkewe na kuambiwa aondoke kwenye Kasri ya mfalme fasta! Baadae kabisa, wapambe wake wakaja kwa mfalme na kumweleza kwamba mkewe watu walimsingizia hajawahi kujihusisha na uzinzi, Mfalme kawasikiliza kwa umakini sana alfu kawapa jibu la kishindo! Kasema hivi: "Yeye kama Mke wa Mfalme hatakiwi hata kutuhumiwa/kuhisiwa na kosa lolote" i.e hata kuhisiwa tu kunatia DOA UFALME/Taifa lake.

Viongozi wetu wa ngazi za juu wakijitahidi ku-emulate uongozi wa Mfalme huyo wa Agano la kale mbona Taifa letu litashamiri na raia wapenda kula/kutoa bribes watafikilia mara mbili kabla ya ku-commit kitu kama hicho. Sasa hivi TAIFA letu limeghubikwa na kasumba ya kuwasifia mafisadi, wala rushwa na wezi utasikia raia wanasema yule jamaa "kuchangamka sijuhi ana AKILI" Personally sita kaa hata siku moja nikamsifia mwizi/mla rushwa/fisadi hata akijenga mahekalu ntamuona hafai hata kidogo.
 

Mkuu kwani Susan Mongi bado yuko TBC! Mbona hasikiki? mara ya mwisho nilimuona mwaka 2008 alipo kuwa amekwenda
Merikani ku-report kuhusu uchaguzi wa Rais wa Taifa hilo.
 

pesa za kuwapa watu Rushwa anazitoa wapi ? Ana Nyumba kubwa Masaki tena ameijenga akiwa waziri . Posho gani zitauwezesha hata kununua kiwaja tu kule masaki ?
 
lowassa alituhumiwa, na yeye hakutaka kubishana na wanaomtuhumu ila alichunguza akaona kisa ni uwaziri mkuu, lowassa aliona wazi watendaji wenzake hawapendezwi na uchapakazi wake, na wakamuundia zengwe

swala la richmond lowassa alishalieleza vizuri, ni kwamba yeye siye aliyepitisha ile kampuni, bali mwenyekiti wa baraza la mawaziri, na hata alipogundua kuna madudu juu ya kampuni alichukua hatua ya kumjulisha mwenyekiti wa baraza la mawaziri ili wabadili maamuzi, mwenyekiti akakataa!

Baadaye inaundwa tume kumchunguza lowassa, kwa kiongozi muadilifu ukituhumiwa ni wajibu kujiweka kando kupisha uchunguzi, yeye alijiweka kando na akasema naandamwa kisa ni uwaziri mkuu

aliyoyafanya lowassa kwa muda mfupi hata sumaye hakuyafanya japo alikaa 10yrs, pinda ndio usiseme, hakuna chochote na kudhihirisha ile richmond ni kampuni ya wale waliotaka lowassa aondoke, alipoondoka hawakuvunja mkataba wakaibadilisha ikaitwa dowans! Baada ya muda wakavunja mkataba wakatupeleka kwenye kesi ya kijinga the hague wakidai bil 95!

Lowassa aliwahi kuvunja mkataba na city water na walikimbilia huko ila waliambulia patupu, kama angekuwa fisadi kama hawa tungesikia tunadaiwa bills kadhaa na city water

nadhani inatosha
 
Ole wako mwalimu mkuu Paschal Mayega akusikie.
 
Ni kweli anadeliver sana akiona kuna mrija wa rushwa! kumbukeni mafuriko ya Lushoto na Korogwe miaka ya tisini mwanzoni akiwa waziri OWM Malecela alivyodeliver kwa kukwapua misaada ya maafa hayo na mpaka akaudhi kiasi alivyoweka jina lake kwenye urais 1995 aliulizwa swali moja tuna mwalimu, wewe mbona utajiri wako unazidi umri wako? Akajiondoa mapema kumpisha JK unataka ushahidi gani zaidi ya kujibu swali la baba wa taifa ambalo hadi leo hajalijibu? Kwanilazima tuongozwe na wezi wakati nchi haijaishiwa waadilifu?
 
Amevikamata vyombo vyote vya ulinzi na usalama kama JWTZ, TISS na POLICE. Pia viongozi wote wa dini wanamkubali na wanataka awe rais wa Tanzania 2015.

kwenye nyekundu, umeshuhudia ukweli wa mleta hoja anaposema "lowasa anautaka urais kuliko mtanzania yeyote aliyepata kutokea" vyombo vya dola havimtumikii mtu binafsi isipokuwa sheria na taratibu zimepindishwa. Hapo ndipo mtoa mada anapokuwa mkweli anaposema "Lowasa ananuka RUSHWA mwili mzima" naamini hata Pasco analijua hili na anaweza kukiri hadharani ikiwa atakumbuka kiapo chake cha ubarikio (kipaimara) ". . . .namkataa shetani na kazi zake zote na . . . . . ." LOWASA anajitukuza sana kiasi namfananisha na mshitaki wetu mbele za mungu. MWENYE MASIKIO NA ASIKIE. Ingekuwa heri kwake mtu huyu akitubu na kuokoka, TANZANIA ITAPUMUA.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu kwani Susan Mongi bado yuko TBC! Mbona hasikiki? mara ya mwisho nilimuona mwaka 2008 alipo kuwa amekwenda
Merikani ku-report kuhusu uchaguzi wa Rais wa Taifa hilo.

Susan bado yupo TBC ila baada ya kuingia Mshana ameminyiwa chini na sasa ni mhariri wa habari upande wa Radio tu.
 
Utajiri wake unathibitishwa nauwezowake mkubwa wa kugawa rushwa kuliko viongozi wenzie au unataka data kuwa benki fulani ana a/c hii na hi subiri wakati ukifika atashangazwa na wapambe wake
 
Ni rais wa Tanzania kuanzia 2015 hadi 2025.
Atakuwa rais tu kama watu wote watakuwa marehemu hivyo ng'ombe ndio watakaomchagua, lakini kama watanzania wako hai atauota tu na kuusikia tu. Atahonga sana apate tiketi ya CCM lakini mwisho wa yote ni wa KULIZWA
 
He will just go through CCM only not BEYOND
 
Lowasa ni mwanamume wa shoka,nijembe la kikwelikweli. Naomba mwenye kuratibu mtandao wake ani PM ili nami niwe kwenye mtandao wa kuhakikisha mwanamume huyu akitinga Magogoni 2015.
Unatafuta mwanamme wa kukuhonga au unatafuta rais wa nchi? kama unatafuta mme muone kuwadi wake mkuu Selukamba
 


Majungu sio mtaji; mwenye ushahidi 100% kuhusiana na tuhuma zote mnazosema za mzee huyo hapo juu wekeni wazi hapa jukwaani.
ushahidi umetolewa mpaka na mwasisi wa taifa hili kama wewe huutaki kwa sababu zako utafundishwa kuelewa 2015
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…