Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,011
- 9,879
Frank Lentini alizaliwa May 18, 1889, Italia na alifariki Septemba 21, 1966 Marekani. Aliishi maisha yake kama mwanamaonesho akitumia umbo lake kama sehemu ya maonesho.
Frank ni moja kati ya watoto waliotakiwa kuzaliwa pacha lakini pacha wake aliunganika naye kwa kile ambacho kisayansi wanakiita ‘Parasitic twin’ ambapo kwake alijikuta ameungana uti wa mgongo na pacha wake.
Hali hiyo ilimfanya awe na miguu mitatu na sehemu mbili za siri, hali iliyoonesha kuwa pacha wake alikuwa mwanaume. Alipozaliwa wazazi wake walimuona ni laana na walimgawa kwa wengine waweze kumlea.
Mbali na hali hiyo ambayo haikuwa kawaida, aliweza kuoa na aliweza kupata watoto wanne.
Frank ni moja kati ya watoto waliotakiwa kuzaliwa pacha lakini pacha wake aliunganika naye kwa kile ambacho kisayansi wanakiita ‘Parasitic twin’ ambapo kwake alijikuta ameungana uti wa mgongo na pacha wake.
Hali hiyo ilimfanya awe na miguu mitatu na sehemu mbili za siri, hali iliyoonesha kuwa pacha wake alikuwa mwanaume. Alipozaliwa wazazi wake walimuona ni laana na walimgawa kwa wengine waweze kumlea.
Mbali na hali hiyo ambayo haikuwa kawaida, aliweza kuoa na aliweza kupata watoto wanne.