Wakala wa majini
Senior Member
- Jan 19, 2020
- 139
- 137
"I am your god and teacher.I am the devine way,the torch that lights up the dark.There is no god but Ali solih."
Haya ni maneno yake marehemu Ali solih aliyekuwa raisi wa Visiwa vya comoro.Kipindi hicho ndio, mwanzo bara la Africa lilikuwa katika harakati za kutaka kujinasua kutoka katika ukoloni, na Visiwa vya comoro vikiwa miongoni mwa nchi zilizowahi kupata Uhuru wao mapema ukilinganisha na taifa la Afrika kusini.
Pia wakati huu,ulikuwa wakati mgumu mno kwa nchi changa za Africa,Kwa sababu ulikuwa mwanzo kwao kujitawala.Hivyo, mahitaji muhimu kama lishe bora,Elimu na Afya vilikuwa ndoto.Pia enzi hizo, Mapinduzi ya serikali ndio ilikuwa kauli mbiu.Kila mwanasiasa alijiona kuwa ana uwezo wa kuongoza, hii ilipelekea kuwepo kwa Mapinduzi ya mara kwa mara,na hili lilikuwa jambo la kawaida tu.
Wananchi nao hawakuwa na kipingamizi, walizikubali hizo serikali mpya, ambazo zilizidi kuwakandamiza na kufanya hali zao kuwa ngumu zaidi.
Tuendelee na mada yetu.
Visiwa vya Comoro vilipata Uhuru wao mnamo mwaka 1975 July kutoka kwa dola ya france. Ali Solih alionekana mtu wa kawaida tu mara ya kwanza kupindua serikali ikiyo kuwepo na kuchukua hatamu ya uongozi wa visiwa vya Comoro miezi sita baada ya kupata uhuru.
Alikuwa na miaka 39 kipindi hicho na alikuwa na kihara.Alikuwa na wake watatu. Pia alikuwa atheist na mnywaji wa vileo licha ya kuwa alikuwa kalelewa kulingana na misingi ya kiislam.
Kwa kauli zake bila Shaka ungeliamini kuwa Ali Solih alikuwa ni mtu mwenye maono makubwa na alikuwa na nia nzuri ya kutaka kuvinasua visiwa vya comoro na watu wake kutoka katika umaskini,ila hali ilikuwa tofauti. Kumbe angelikuja kupagazwa jina la "mwendawazimu wa Moroni."
Ali Solih alibadilika ghafla mara tu alipochukua uongozi. Baadhi ya watu walidai kuwa ni madawa na tembo ndivyo vilivyo mbadilisha. Wengine walisema kuwa alikuwa mwendawazimu. Ila tatizo lilikuwa ni majukumu ya uraisi yalikuwa yakimlemea.
Ndoto na maono yake vikaanza kufifia.Akawa ni mtu wa anasa. Watu waliokuwa na akili za kufikiria na ujasiri wa kuzungumza waliishia makaburini au jela, mpaka wakabaki ma zebe wa ndio tu. Comoro ikawa kama mfano wa mwana Sesere kwa Ali Solih anaichezea anavyotaka.
Akawafuta kazi members of civil service karibia mia tano, na kuwajaza katika serikali vijana ambao walikuwa ni ma school dropout ambao angelikuwa na uwezo wa kuwapeleka anavyo taka. Akashusha umri wa kupiga kura mpaka miaka kumi na minne na kujitangaza kuwa yeye alikuwa nabii. Akafunga ma hoteli huku akisema "foreign infuence corrupt." Na kutaifisha kila kitu mpaka magari ya teksi na maduka ya kuuza mikate. Akawaleta washauri wa kichina ili waje wamuongoze na ma soldier kutoka Tanzania waje wamlinde. Akatangaza kuwa dini ni laana, na kupiga marufuku wanawake wa kiislamu kuvaa majalbib na mabaibui.
Siku moja alijivurumiza msikitini na kuanza kuwakemea waumini kwa kuwaambia "Endeleeni kumuomba Mungu. Muiteni huyo Mungu muone kama atawajibu maombi yenu."
Akawataliki wake zake na kuanza kuvamia visichana vidogo.
"Hatuwezi kuendelea tena kuipeleka hii nchi jinsi tunavyo ipeleka, nchi inapelekwa na vijana wadogo, watu wanatuona sisi wenda wazimu na taifa lote kwa ujumla limekwama." Siku moja Abbas Jusuf alimwambia Ali Solih. "Nyamaza”, Ali Solih alijibu kwa ukali. "Hivi wewe hutambui kama mimi nina maono-maono makubwa. Huu ndio mustakabali wetu." Akajibu Ali Solih.
Siku iliyofuata mamake Abbas Jusuf alikamatwa na kufungwa bila mashtaka yeyote. Siku moja Ali Solih alioteshwa "maono" makubwa. Aliota mtu na mbwa wake wamemjia na kutaka kumuua. Usiku huo alishtuka kutoka usingizini jasho likimkatika huku akitetemeka. Akamueleza mfanyakazi wake kuhusu ndoto hii. Siku iliyofuata asubuhi, baada ya chajio cha soseji na kinywaji cha brandy, Bwana solih alitoa agizo mbwa wote katika visiwa vya Comoro wauliwe mara moja.
Vijana walipata kazi, order hii ya raisi Ali Solih ilitekelezwa mara moja. Mbwa waliuliwa kwa mapanga na bunduki, wakiwaburuza wengine kwa magari yao.Mbwa waliadimika ghafla.
Nitakomea hapo wapendwa. Nitarudi na muendelezo wa jinsi utawala huu dhalimu wa Ali Solih ulivyopinduliwa.
Karibuni.
Haya ni maneno yake marehemu Ali solih aliyekuwa raisi wa Visiwa vya comoro.Kipindi hicho ndio, mwanzo bara la Africa lilikuwa katika harakati za kutaka kujinasua kutoka katika ukoloni, na Visiwa vya comoro vikiwa miongoni mwa nchi zilizowahi kupata Uhuru wao mapema ukilinganisha na taifa la Afrika kusini.
Pia wakati huu,ulikuwa wakati mgumu mno kwa nchi changa za Africa,Kwa sababu ulikuwa mwanzo kwao kujitawala.Hivyo, mahitaji muhimu kama lishe bora,Elimu na Afya vilikuwa ndoto.Pia enzi hizo, Mapinduzi ya serikali ndio ilikuwa kauli mbiu.Kila mwanasiasa alijiona kuwa ana uwezo wa kuongoza, hii ilipelekea kuwepo kwa Mapinduzi ya mara kwa mara,na hili lilikuwa jambo la kawaida tu.
Wananchi nao hawakuwa na kipingamizi, walizikubali hizo serikali mpya, ambazo zilizidi kuwakandamiza na kufanya hali zao kuwa ngumu zaidi.
Tuendelee na mada yetu.
Visiwa vya Comoro vilipata Uhuru wao mnamo mwaka 1975 July kutoka kwa dola ya france. Ali Solih alionekana mtu wa kawaida tu mara ya kwanza kupindua serikali ikiyo kuwepo na kuchukua hatamu ya uongozi wa visiwa vya Comoro miezi sita baada ya kupata uhuru.
Alikuwa na miaka 39 kipindi hicho na alikuwa na kihara.Alikuwa na wake watatu. Pia alikuwa atheist na mnywaji wa vileo licha ya kuwa alikuwa kalelewa kulingana na misingi ya kiislam.
Kwa kauli zake bila Shaka ungeliamini kuwa Ali Solih alikuwa ni mtu mwenye maono makubwa na alikuwa na nia nzuri ya kutaka kuvinasua visiwa vya comoro na watu wake kutoka katika umaskini,ila hali ilikuwa tofauti. Kumbe angelikuja kupagazwa jina la "mwendawazimu wa Moroni."
Ali Solih alibadilika ghafla mara tu alipochukua uongozi. Baadhi ya watu walidai kuwa ni madawa na tembo ndivyo vilivyo mbadilisha. Wengine walisema kuwa alikuwa mwendawazimu. Ila tatizo lilikuwa ni majukumu ya uraisi yalikuwa yakimlemea.
Ndoto na maono yake vikaanza kufifia.Akawa ni mtu wa anasa. Watu waliokuwa na akili za kufikiria na ujasiri wa kuzungumza waliishia makaburini au jela, mpaka wakabaki ma zebe wa ndio tu. Comoro ikawa kama mfano wa mwana Sesere kwa Ali Solih anaichezea anavyotaka.
Akawafuta kazi members of civil service karibia mia tano, na kuwajaza katika serikali vijana ambao walikuwa ni ma school dropout ambao angelikuwa na uwezo wa kuwapeleka anavyo taka. Akashusha umri wa kupiga kura mpaka miaka kumi na minne na kujitangaza kuwa yeye alikuwa nabii. Akafunga ma hoteli huku akisema "foreign infuence corrupt." Na kutaifisha kila kitu mpaka magari ya teksi na maduka ya kuuza mikate. Akawaleta washauri wa kichina ili waje wamuongoze na ma soldier kutoka Tanzania waje wamlinde. Akatangaza kuwa dini ni laana, na kupiga marufuku wanawake wa kiislamu kuvaa majalbib na mabaibui.
Siku moja alijivurumiza msikitini na kuanza kuwakemea waumini kwa kuwaambia "Endeleeni kumuomba Mungu. Muiteni huyo Mungu muone kama atawajibu maombi yenu."
Akawataliki wake zake na kuanza kuvamia visichana vidogo.
"Hatuwezi kuendelea tena kuipeleka hii nchi jinsi tunavyo ipeleka, nchi inapelekwa na vijana wadogo, watu wanatuona sisi wenda wazimu na taifa lote kwa ujumla limekwama." Siku moja Abbas Jusuf alimwambia Ali Solih. "Nyamaza”, Ali Solih alijibu kwa ukali. "Hivi wewe hutambui kama mimi nina maono-maono makubwa. Huu ndio mustakabali wetu." Akajibu Ali Solih.
Siku iliyofuata mamake Abbas Jusuf alikamatwa na kufungwa bila mashtaka yeyote. Siku moja Ali Solih alioteshwa "maono" makubwa. Aliota mtu na mbwa wake wamemjia na kutaka kumuua. Usiku huo alishtuka kutoka usingizini jasho likimkatika huku akitetemeka. Akamueleza mfanyakazi wake kuhusu ndoto hii. Siku iliyofuata asubuhi, baada ya chajio cha soseji na kinywaji cha brandy, Bwana solih alitoa agizo mbwa wote katika visiwa vya Comoro wauliwe mara moja.
Vijana walipata kazi, order hii ya raisi Ali Solih ilitekelezwa mara moja. Mbwa waliuliwa kwa mapanga na bunduki, wakiwaburuza wengine kwa magari yao.Mbwa waliadimika ghafla.
Nitakomea hapo wapendwa. Nitarudi na muendelezo wa jinsi utawala huu dhalimu wa Ali Solih ulivyopinduliwa.
Karibuni.