Mji gani mzuri kati ya Lindi na Singida?

Mji gani mzuri kati ya Lindi na Singida?

Lindi ukikomaa kibiashara unatoka hasa wageni ila wenyeji wengi ni wavivu,....kuna watu wapo Lindi hawataki hata kupasikia kwao,mambo yalivyo mazuri..Iringa dah!! Labda kwasababu sikukaa sana..
 
Singida ipi unaizungumzia!!!!Apo kwa nyokaa na viunga vyake ndo yakufananisha na Moshi futa iyo kauli upesi
 
Lindi labda ukavune chumvi tu
Singida ni ka mji ambako kanakuwa tofauti na kipindi cha nyuma. Ni mji ambao hata kibiashara uko vizuri halafu ni mji ambao ni rahisi kwenda popote pale ukitaka kwenda nairobi unagusa tu, kwenda kampala unagusa tu na kote huko kuna muingiliano wa kibiashara hususani kipindi kama hichi cha mavuno. Kifupi singida ni mji unaweza ukaekeza na ukatoboa tofauti na huo mji wa lindi kuna urasimu sana huko.
 
Wana viunga vya Nazi kazi kucheza zumna
Aaaah ninja afadhali Musoma kuna kamtaa kanaitwa Nyakato kanavutia wakurya wamejitambua Ugali unauzwa kila sehemu watu hawakai kindezi tena ila Lindi sijui wana nini wale watu kazi hawafanyi ni majungu na uchawi tu
 
Halafu matajiri wabaguzi sana wakitaka kujenga migorofa mirefu wanaenda Ilala na Kino ingawa unasema kote ni mjini yani huko Temeke Uswahili mwingi kama Lindi bahati yenu aliyeamua kwa Mchina pajengwe pale sijui mngejivunia nini
..tatizo mnashukia kibaha umetembea sana posta au kariakoo....ile bandari ipo laela? Igawe Nyerere road ndo utaanza ijua tmk
 
Lindi ukikomaa kibiashara unatoka hasa wageni ila wenyeji wengi ni wavivu,....kuna watu wapo Lindi hawataki hata kupasikia kwao,mambo yalivyo mazuri..Iringa dah!! Labda kwasababu sikukaa sana..
Iringa unapasemeleaje Mkuu!!
 
Kwa uzoefu wangu wa kuishi miji yote miwili Singida ni pazuri sana kulinganisha na Lindi in term of uzuri wa mji hata fursa.
Kwangu mimi Lindi iko nyuma hata kwa miji kama Kasulu, Masasi, Kahama, Makambako, Mpanda, Njombe na hata Babati, Tunduma
 
Singida Kwa sasa imekuwa sana na barabara za lami mji mzima. Pia kipato cha Singida angalau kipo juu zaidi ya Lindi
Hii miji ilikua nyuma sn ezi za Nyerere,Mwinyi na Mkapa lkn hivi karibuni mambo sio kama zamani bara bara, fulsa na miundo mbinu mingine...mingi.Je upi mji mzuri wenye fulsa nyingi..ns ni mzuti kwa kuishi
 
Back
Top Bottom