Habari wakuu,
Tarehe 25/06/2013 nilimtembelea Rafiki yangu mmoja ambaye ni mwanajeshi Huko mkoa (kapuni) jina la kambi (kapuni). Jamaa aliniambia mambo mengi kuhusu Arusha, hasa kwenye harakati za chadema. anasema yeye alikuwa mkoa wa Arusha kabla hajahamishiwa Kigoma, alikuwa kikosi no(kapuni). aliniambaia kwamba chadema wakifanya maandamano au mikutano walikuwa wanapewa sale za asikari polisi kuja kudeal na chadema, ili ionekane kwamba ni polisi wanaotuliza ghasia kumbe ni wanajesshi wa JWTZ. Jamaa akasema hili suala lilikuwa linawauma sana, kuna siku pale arusha zilitokea fujo kati ya ccm na chadema wakaambiwa waende kuwadhibiti chadema, jamaa wakaenda na uniform za polisi, badala ya kuwapiga chadema wakawapiga ccm, vunjavunja. baada ya fujo kumalizika ikaonekana watu walioumia sana na kuvunjika ni wa ccm. Serikali ikaamua kuwahamisha wote na kuwapeleka pembeni mwa nchi (mipakani huko). akaniambia kwa sasa serikali inachukua wanajeshi wa Morgoro kuja kutuliza fujo Arusha,wakiwa wamevaa gwanda la polisi.
Hii ni hatari sana kutumia Jeshi kuwakandamiza wananchi.