MJADALA: Kwanini Padri Luther aliondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia, na kwanini alijiondoa kanisa Katoliki?

Biblia inasema Bikra Maria ataitwa mbarikiwa, na dunia itamsifu kuwa yeye ni mbarikiwa. Bikra Maria kwa mujibu wa kumbukumbu za kanisha hakufa, alipaazwa. Ujui historia, huyu mama ni the special, hata waprotestant wakimtupa sisi Wakatoliki tutaendelea kutimiza unabii kwa kumuita mbarikiwa
Nipe mstari unaosema Maria alipaa kwenda mbinguni.
 
View attachment 1371369
PICHA: Padri Martin Luther
Padre Luther alikuwa miongoni mwa Mapdre wenye karama nyingi ndani ya Kanisa Katoliki wakati wake, yeye alikuwa na Madai mengi sana juu ya mapungufu kwa kanisa. Hata hivyo madai yake mengi hayakuwa na msingi wowote.

Moja ya madai yake ilikuwa ni kuondoa kibali cha kwamba baada ya kuungama muumini asipewe stakabadhi ya kuonesha ameungama kwa kuwa kitubio ni siri ya mtu. Hili lilifanyiwa kazi. Mengine ikiwemo kurekebisha mfumo wa sala ya Kanuni ya Imani. Na mambo mengine mengi ambayo alipojibiwa, yeye hakuridhika pamoja na kueleweshwa vya kutosha. Alikuwa ni Great Thinker sana.

Mbaya zaidi alipokuja kusababisha mpaka akajitenga na kanisa ni kitendo cha kuondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia ikiwemo pia kupunguza baadhi ya mistari kwenye vitabu kama cha Esta na cha Danieli.

Aliondoa vitabu vya Deutrokanoni na vingine baadhi na kuwa jumla ya vitabu 7 vilivyotolewa kwenye Biblia. Na kila kitabu alikuwa na sababu yake aliyoibainisha. Kimsingi alipata wafuasi wengi wa kumuunga mkono hoja yake hasa wale ambao walikuwa wanatafuta njia ya kuchuma pesa kiulaini. Na hapo Biblia mpya ilianza yenye Vitabu pungufu.

Na ndio maana leo watu hawaujui Ukristo vizuri na wanakinzana bila kujua historia ya kanisa. Watumishi wengi wa Mungu hasa hawa wa kileo wasiojua historia vizuri wao kila kitu wanapinga. Sio kosa lao Bali ni kosa la kutokujua historia ya kanisa.

Matumizi ya Ubani yalipingwa sana, na hapa ilikuwa ni kuondoa idadi ya waelewa. Kutokana na watu wengi walikuwa wamegeuka kama waganga kila mapepo ya kiwakabili walitumia ubani kuyafukuza na yalikimbia, lakini watu walijisahau kusali na kuomba na hata kufika ibadani ikawa nadra maana wanajua kujiponya kuondokana na majini na wachawi. Hapa Padre Luther na wenzake wakapiga marufuku matumizi ya ubani na kuwa sihi wakazanie Neno zaidi.

Hapa walichotakiwa kufanya ni kuliishi Neno la Mungu na wakati wa ibada basi ubani uchomwe kama Mungu alivyo agiza.

Luther na wenzake lengo lao lilikuwa ni biashara hapo baadae na kimsingi mpango huo ulifanikiwa. Na ndio maana mpaka Leo watu wametawaliwa na mfumo wa majini katika maisha yao kwa kuwa wamefungwa akili ya kujitambua na wanaamini maneno ya mdomoni na sio Maandiko ya Biblia kama yanavyosema.

Nimengi sana ya kujifunza lakini kwa Leo naishia hapa.

ZAIDI TAZAMA HAPA


deogratius Nalimi Kisandu.
1. 1. 2017.


MAONI YA WADAU

-------------

-------------

-------------

-------------

-------------


-------------

--------------

--------------

--------------

-------------

mtu yeyote akiamini kanisa linatumia biblia lazima atalipinga, maana yaliyopo kwenye biblia na yanayoendelea kwenye kanisa haviendani
ukielewa misimamo ya kanisa na chanzo cha imani yao huwezi ongelea biblia
hawafuati biblia, na ndio maana hawapendi watu wasome biblia. wanaona haina umuhimu
Luther alivoanza kufundisha chuo kikuuu akapata access ya kusoma biblia akashangaa sana, akaona mbona hatufuati biblia. katika kuhoji akaonekana muasi
 
mtu yeyote akiamini kanisa linatumia biblia lazima atalipinga, maana yaliyopo kwenye biblia na yanayoendelea kwenye kanisa haviendani
ukielewa misimamo ya kanisa na chanzo cha imani yao huwezi ongelea biblia
hawafuati biblia, na ndio maana hawapendi watu wasome biblia. wanaona haina umuhimu
Luther alivoanza kufundisha chuo kikuuu akapata access ya kusoma biblia akashangaa sana, akaona mbona hatufuati biblia. katika kuhoji akaonekana muasi
Unazungumzia hiyo karne ya 14, Martin Luther aliikuta Biblia ikiwa na vumbi katika maktaba. pamoja na usomi wake hakuwa kukutana na biblia hata ikitajwa kanisani au popote. Hiyo ndivyo ilivyokuwa Kanisa la Roma, ilikuwa inaelekea kuwa dola zaidi ya Kanisa. Uasi wa Martin LUther ndio iliyofanya Kanisa la katoliki kurudi nyuma na kuanza tena kutumia Biblia
 
Luther alivoanza kufundisha chuo kikuuu akapata access ya kusoma biblia akashangaa sana, akaona mbona hatufuati biblia. katika kuhoji akaonekana muasi
Yameulizwa maswali mawili, kwanini aliachana na kanisa katoliki na kwanini alinyofoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia?

Umejibu swali la kwanza, kujiondoa kwake kwenye ukatoliki. Swali la kwanini alinyofoa baadhi ya vitabu halijajibiwa.
 
uongo wa mchana hebu lete andiko.
maana maria ndiye aliyesema hivyo.
LUKA 1:46-48.
anasema watamwita mmbarikiwa lakini sio Mungu kusema tutamwita hivyo
Neno la MUNGU halijipingi unataka kudhihirisha kua unasema uongo
Haraka zako za kuambiwa zinakuelekeza siko
Ludi nyuma katika enjili hiyo ya Luka 1:41 roho mtakatifu anamjaza Elizabeth na kunena kua Mariam amebarikiwa kuliko wanawake wote hayo maneno yalinenwa na Elizabeth Kwa njia ya roho mtakatifu siyo Mariam
Luka 1:43 Elizabeth anakiri kua Mariam ni mama wa BWANA wake (MUNGU) kwako hiyo anafanywa kua baraka rejea mwanzo 12 :2-3
Kama alivyo muandaa Ibrahim na uzao wake kua baraka unakamilishwa Kwa mwana mwali Mariam
Usichoke kusoma biblia katika kitabu cha mwanzo 3:6 mwanamke anachuma dhambi na kumpa adamu tunda la dhambi wote wanaanguka dhambini na hayo Mwanamke anasababisha
Mwanzo 3:15 Lakini MUNGU ana ahidi ukombozi Kwa mwanamke kua uzao wake utamshinda shetani na ushawishi wa kutenda dhambi
Katika yeye ukombozi unakuja dhambi ililetwa na mwanamke mwa 3 :6 na mwana wa mwanamke Mariam Luka 1:43 anaukomboa ulimwengu
Huyo Mwanamke ndiye analeta baraka za Ibrahim Baba yake dunia yote inabarikiwa mwanzo 13:2-3
Yesu Kristo akizaliwa na mariamu si kibailojia wala hakua na Baba wa kibailojia MUNGU alichagua MTU Bora kuliko wote kwakwe yeye aweze kuufikia ulimwengu ulio potoka uwezo kumludia yeye muumba wake
 
Yameulizwa maswali mawili, kwanini aliachana na kanisa katoliki na kwanini alinyofoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia?

Umejibu swali la kwanza, kujiondoa kwake kwenye ukatoliki. Swali la kwanini alinyofoa baadhi ya vitabu halijajibiwa.
sijawahi kusoma popote juu ya kwamba huyo jamaa aliondoa vitabu kwenye biblia
na sidhani kama vitabu vilivyotolewa na havikujumuishwa kwenye biblia ni kitu kilifanywa na mtu mmoja
ni wataalam walivisoma wakaona maudhui yake yana walakini. wakavitoa
 
Back
Top Bottom