Mjadala: Hoja za Wadau kuhusu namna ambavyo Mgawo wa Umeme umeathiri shughuli za Kijamii na Kiuchumi nchini

Huku nilipo mkoani umeme unakatika Kwa saa 1 Tu na urudi fasta..
Bado najiuliza inawezekanaje hii, au kanda inayo power Yao ya kufua umeme?
 
Niliishi mkoani tanga wilaya ya kilindi around mwaka 2018 , umeme ulikua unakatika asubuhi unarudi jion saa 12 ukirudi wananchi wote wanakimbizana kwenda kwenye mabanda ya video
 
No one is addressing this serious issue huko nyumbani sio wanasiasa wala wananchi yaani kiufupi maji nimarefu sana kwa hangaya , sukari hakuna umeme hakuna dola inapaa lakini nchi ina wasomi wataalamu wa kila aina lakini wamekaa kimyaaaaa utadhani wamerogwa, ukiona watu wanaishi kwa kujipendekeza ili wapate mlo ujue hizo ndio dalili za failed state, sitaki kuamioni kama ndio tulikofika. Tunhitaji kutawaliwa upyaaa
 
Changamoto ya kukatika kwa Umeme imekuwa ikisababisha Athari za Kiuchumi, Afya na Usumbufu kwenye Maisha ya kila siku kwa Wananchi Je, unaridhishwa na hatua zinazochukuliwa na Mamlaka katika kukabiliana na hali ya ukosefu wa Umeme katika eneo lako?

Jiunge nasi katika mjadala, muda huu unakaoangazia Athari za Mgawo wa Umeme kwa Wananchi na hatua zinazochukuliwa na Serikali kukabiliana na changamoto hiyo kupitia #XSpaces ya JamiiForumsKushiriki Mjadala bofya https://jamii.app/MgawoUmeme
 
Watu wengine tena walio wengi "bila umeme mkono hauendi kinywani ". Athari ni kubwa. Kama kuna uzembe, huyo mzembe ni "MUUWAJI ".
 
Umeathiri kila kitu.

Wajasiliamali wadogo kama vinyozi, mafundi wa kuchomelea hela sasa hivi wanazishika kwa manati, huduma za kijamii zimekuwa hovyo mfano kuna maeneo utokaji wa maji unategemea uwepo wa umeme kama umeme hakuna maji inakuwa msamiati mwingine.

TANESCO na waziri wa hii wizara ajitafakali sana kwanini enzi za jiwe umeme ulikuwa hauna shida wao wanashindwa nini, kuna biashara gani wanafanya kwenye huu mgao wa umeme?
Wauza barafu,ice cream za majubani,wauza juice,soda,maji ya baridi,fruit za baridi,hali ni ngumu,ngumu sana.Hakuna umeme,wakufanya barafu zinfande na ice cream kuganda,,nq juice na maji kupata baridi,hakuna kipato.
 
Watu wengine tena walio wengi "bila umeme mkono hauendi kinywani ". Athari ni kubwa. Kama kuna uzembe, huyo mzembe ni "MUUWAJI ".
Kama wachuuzi wa barafu,ice cream,juice na maji ya baridi,maisha yamekuwa ni shida kwao.Hawana cha kuuza,barafu hazigandi,maji na juice hazipati baridi,ice cream za kutengeneza majumbani hqzigandi.Maisha magumu sana.
 
Watu wengine tena walio wengi "bila umeme mkono hauendi kinywani ". Athari ni kubwa. Kama kuna uzembe, huyo mzembe ni "MUUWAJI ".
Hali ni ngumu.wachuuzi wa barafu,ice cream za majumbani,juice,maji ya baridi,hali ni ngumu.Wengi walinunua freezer kwa biashara hizo,zi wakimu kimaisha.
 
Kwa jiji lenye joto kali kama dar umeme haukupaswa kukatika hata kwa dakika 15 tu.

Umeme unatumika kukabiliana na hii hali mbaya ya hewa, umeme unatumika kuvuta maji visimani maana dawasco nao ni tatizo, umeme unatumika kupooza vitu/kuhifadhi visiharibike, kwa mgao huu usio na ratiba maalum umefanya mtu awashe freezer yake hata kwa masaa 24 maana hujui wanakata saa ngapi, ili walau vitu vigande.

Watu wana viwanda vidogo vya kushona, mashine za kufua, mafundi wa vifaa mbalimbali wote hawa wanategemea umeme.

Kundi kubwa limechagua kuvumilia na kusubiri muujiza tu, sioni watu wakifanya jitihada zaidi ya kusubiri kusema huuoooo.
 
Nalaza kazi za ofisi katika matumizi ya computer, nalazimika kusafiri km 15 kufuata mafuta sheli ili generator liwake.

Wakati mwingine umeme urudipo usiku kama hivi leo nalazimika kwenda ofisini nikafanye kazi kwa kuwa sina uhakika kama kesho asubuhi umeme utakuwepo, tabu tupu ni mgogoro tu na wife kunihisi nipo mchepuko wakati napiga kazi muda huu.
Tumia inverter ya pure sine na betri N 100 au 200 ya kampuni Fulani hivi inaitwa Ritar SEMA bei zao zimechangamka kidogo.
 
Nilikuwa natotoresha vifaranga kwa kutumia incubator. Nilikuwa natotoresha vifaranga 1000 vya kuku, Bata na Kanga. Niliacha toka mwezi wa 10 tokana na changamoto ya umeme nikajua baada ya muda utastablelize.

Tokana na pressure ya wateja, ikabidi nitafute generator na kuanza kupiga kazi mwezi 12. Gharama zimekuwa juu kwani inabidi nitumie ⛽️ ⛽️ kuendesha mtambo. Sasa sipati faida kwani nafanya kuridhisha wateja tu.
Mkuu waweza tafuta fundi akakusukia inverter ya pure sine ambayo inaundwa kulingana na matumizi yako. Alafu unatafuta betri za kwenye minara, au za kampuni za Rita ya N100 au N200 kulingana na matumizi yako. Then unapeta maana inverter inakuwa na sehemu ya kuchajia umeme ukirudi. Pia Kuna mfumo unafungwa ambao utafanya kazi zako zisitetereke pale ambapo umeme umekuja Kwa ghafla au kukatika.
 
Back
Top Bottom