Mizengo Pinda: Mnaitaka Tanganyika ipi?.

Mizengo Pinda: Mnaitaka Tanganyika ipi?.

Waziri Mkuu na wanachama wengine wa CCM watwambie wazi iliko Tanganyika ndani ya Muungano! Nadhani Nyerere alibuni haina hii ya Muungano wa serikali mbili akionesha dhamira safi ya kuipoteza Tanganyika kwanza. Na hii ilikuwa ni katika harakati zake za kuwaambia wazanzibari kuwa serikali moja na nchi moja inawezekena!Kwa miaka 50; wazanzibari wanaona hizo ndoto za kuwa serikali moja na nchi moja ni ngumu sana kuziota! Wanalalamika! Wanataka chao! Watànganyika waliosinzia miaka mingi sasa nao wameamka! Wamechoka kelele; wanataka chao hata kama ni kichanga ili wawe huru!Someni alama za nyakati enyi Watànganyika! Li nchi likubwa lenye watu wengi mnabaki kulalamika lalamika tu!
 
Pinda tunataka Tanganyika aka Tanzania Bara ambayo waziri mkuu wetu anaheshimika, sio tuna sema serikali mbili, wakati upande mwingine wanamuona kama Shoe shiner, hata dc, mkuu wa mkoa nk hawamjui
 
Huwa napata tabu sana mtu akisema analogically muungano kuvunjika?
Mkuu ingekuwa vizuri ukaeleza njia na mantiki inayokufanya upate shida kuhusu mawazo na maoni ya baadhi ya watu wanakuja na hoja zinazobainisha kuvunjika kwa Munngano.
Kama wananchi hawataki muungano/kuendeelea kuungana kwa nini "walazimishwe" kwa kuweka protactive structure?
Ni kweli huwezi kulazimisha wananchi katika mazingira ya demokrasia kufanya jambo ambalo wengi hawataki lakini vile vile hakuna research au kura ya maoni iliyopigwa kubainisha maoni ya wananchi kuhusu muungano.

Hatuwezi kusema wananchi wanalazimishwa au hawalazimishwi kutokana na historia na pia structure ya muungano.

Viongozi wetu waanzilishi wa mataifa yetu waliamua nchi ziungane na wakaziunganisha bila kutaka kusikia neno la wananchi wote kwa njia ya kura ya maoni, na kwa maana hiyo, mpaka sasa hatujafahamu mitazamo ya wananchi wengi kuhusu muungano.
Serikali moja ama tatu ingalikuwa ni kipimo sahihi cha kuweza kujua kama muungano huu ni wa hiari ama wa kulazimishana.
Hoja mbadala nadhani ni kura ya maoni ambayo itatoa constitution legitimacy kutoka kwa wananchi kuhusu aina ya muungano wanaoutaka lakini siyo kufanya test ambayo matokeo yake hasara kubwa kitaifa.

Kwa mazingira ya kisiasa tuliyonayo kwa sasa na pia historia ya nchi zetu, nadhani serikali moja ndiyo ingetoa jibu kama kweli tunataka kuungana na siyo kuwa shirikisho kama inavyoonekana kupigiwa chapuo kwa sasa.

Muungano hauwezi kuimarika kama tutaendelea kuishi kwenye pretext ya muungano wakati tunafanya mambo katika misingi ya shirikisho.
Tusiogope muungano kuvunjika kama hivyo ndivyo wananchi walio wengi wanataka iwe.Lakini suala la serikali moja kwa sasa sio mojawapo ya options kwa sababu serikali ya Zanzibar ni lazima iwepo(kwa mujibu wa ToR).
Ninadhani watu hawaogopi muungano kuvunjika bali wanahofu na gharama za muungano kuvunjika katika mazingira fulani.

Kama watu wa nchi mbili watakaa na kuamua kuvunja muungano kwa amani, basi nadhani hili wala halina uwoga lakini hofu inakuja kama kuna kundi au nchi moja itataka muungano kuvunjika kwa kutumia nguvu nje ya amani ambapo nguvu hiyo inapelekea kuwepo kwa gharama kubwa kisiasa, kiuchumi na kijamii.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
pinda anavyoongea kwa hasira utadhani hii nchi ameiletea uhuru yeye...anajikuta anaijua tanzania kinagaubaga kuliko hata wazee waliomzidi umri,Huyu ndio mana aliubwa na sura ngumu kama (.......)sio mzalendo kabsa
 
hili suala Tanganyika inayotakiwa ya mkoloni au ya baada ya uhuru angemuuliza jaji Warioba .Pinda anaonesha dharau kwa tume ya katiba
 
Ndiyo maana nikasema kwa maoni yangu ninataka serikali moja kwa sababu sioni njia nyingine itakayoweza kuondoa hizi kero ambazo kila upande wa nchi unalalamikia.

Sioni kama serikali tatu ndiyo zitaondoa kero, ninachoona serikali tatu ni njia ya kutengeneza mazingira kuelekea kuvunjika kwa muungano lakini kwa gharama kubwa hasa kama ukizichunguza kauli za viongozi wa kisiasa wa upande wa Zanzibar.

Haya ndiyo matatizo ya kutokuwepo kura ya maoni kabla ya kuingia kwenye mchakato wa kuandika Rasimu ya Katiba. Kwa sasa kinachoongelewa kwenye mchakato wa Katiba ni Muungano wakati kuna mambo mengi sana ndani ya Rasimu ya Katiba ambayo yanahitaji critical observation and examination kama inavyofanyika kwenye swala la Muungano.
Wewe ni Mnafiki........
 
Wewe ni Mnafiki........
Hata nilipozaliwa tu haikupita hata dakika nikapewa jina na kuanzia hapo nimepewa majina mengi tu mpaka sasa. Hakuna kitakachonishangaza na wewe ukija na jina jingine kwa sababu huu ni mwendelezo wa kile kilichotokea pale nilipozaliwa

Niseme tu kuwa, ninashukuru kwa kunipa jina jingine lakini vile vile ningependa kufahamu, wewe unaitwa nani katika mantiki za hoja hii?.
 
Mkuu ingekuwa vizuri ukaeleza njia na mantiki inayokufanya upate shida kuhusu mawazo na maoni ya baadhi ya watu wanakuja na hoja zinazobainisha kuvunjika kwa Munngano.

Ni kweli huwezi kulazimisha wananchi katika mazingira ya demokrasia kufanya jambo ambalo wengi hawataki lakini vile vile hakuna research au kura ya maoni iliyopigwa kubainisha maoni ya wananchi kuhusu muungano.

Hatuwezi kusema wananchi wanalazimishwa au hawalazimishwi kutokana na historia na pia structure ya muungano.

Viongozi wetu waanzilishi wa mataifa yetu waliamua nchi ziungane na wakaziunganisha bila kutaka kusikia neno la wananchi wote kwa njia ya kura ya maoni, na kwa maana hiyo, mpaka sasa hatujafahamu mitazamo ya wananchi wengi kuhusu muungano.

Hoja mbadala nadhani ni kura ya maoni ambayo itatoa constitution legitimacy kutoka kwa wananchi kuhusu aina ya muungano wanaoutaka lakini siyo kufanya test ambayo matokeo yake hasara kubwa kitaifa.

Kwa mazingira ya kisiasa tuliyonayo kwa sasa na pia historia ya nchi zetu, nadhani serikali moja ndiyo ingetoa jibu kama kweli tunataka kuungana na siyo kuwa shirikisho kama inavyoonekana kupigiwa chapuo kwa sasa.

Muungano hauwezi kuimarika kama tutaendelea kuishi kwenye pretext ya muungano wakati tunafanya mambo katika misingi ya shirikisho.

Ninadhani watu hawaogopi muungano kuvunjika bali wanahofu na gharama za muungano kuvunjika katika mazingira fulani.

Kama watu wa nchi mbili watakaa na kuamua kuvunja muungano kwa amani, basi nadhani hili wala halina uwoga lakini hofu inakuja kama kuna kundi au nchi moja itataka muungano kuvunjika kwa kutumia nguvu nje ya amani ambapo nguvu hiyo inapelekea kuwepo kwa gharama kubwa kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Gharama zipi za kuvunja muungano
 
Mazoea yaCCM ni sawa na tabia ya Wanyama Paka ukimzoesha kumpa chakula chake kwenye chombo fulsni siku ukiamua ubadilishe anakurarua. Kupe akianza kunyonya sehemu mpk anazama pale namwisho ananenepa na kudondoka nakufa. Pinda hasomi nyakati huu ndiyo mwisho wa muungano huu unatakiwa mwingine kama mnanyonya basi mmenenepa mtadondoka na kupoteza maisha enyi kupe na vitoto vyenu jueni
 
Huu ni upuuzi kwani hao walioipata Zanzibar Huru yenye Mipaka yake na Rais wake waliipata lini wakati wa uhuru au kabla ya uhuru au wakati wa mapinduzi au Kabla ya Mapinduzi.

Na kusema kwamba Tanganyika ya Mkoloni ndiyo iliyokaa muda mrefu ni mawazo mengine ya kitumwa na ufinyu wa kufikiri kwanii hii Tanzania ya sasa mipaka yake iliwekwa na nani huwezi ukatofautisha !.Huwezi kuongoza nchi kwa mawazo ya kina Nyerere na Karume. Muungano lazima uwe ni ule ambao unaridhiwa na kukubalika na wananchi wote.

Aidha nina wasiwasi na hao aliowahoji angeniuliza mimi unaitaka Tanganyika gani ningemwambia ile ya Kikoloni ili tuanze mapambano upya,tujipange vizuri na ukipatikana uhuru mpya tuwe na chama kinachothamini Utu na Haki za mwananchi Mzalendo.Tuna taka Tanganyika ya Kikoloni maake licha ya udokozi wao wakoloni hawakuwa wezi wa kura ndo maake TANU ilishinda na waliheshimu maamuzi ya wananchi na zaidi hawakuwahi kufukia raia walio hai kwenye Migodi ya Madini.

Tunacho kitaka ni Tanganyika yetu itakayosimamia Mipango na Maendeleo ya Tanganyika na siyo huu Muungano wa watu wawili tunao lazimishana kuufanya muungano wa wananchi wote.
 
Ndiyo maana nikasema kwa maoni yangu ninataka serikali moja kwa sababu sioni njia nyingine itakayoweza kuondoa hizi kero ambazo kila upande wa nchi unalalamikia.

Sioni kama serikali tatu ndiyo zitaondoa kero, ninachoona serikali tatu ni njia ya kutengeneza mazingira kuelekea kuvunjika kwa muungano lakini kwa gharama kubwa hasa kama ukizichunguza kauli za viongozi wa kisiasa wa upande wa Zanzibar.

Haya ndiyo matatizo ya kutokuwepo kura ya maoni kabla ya kuingia kwenye mchakato wa kuandika Rasimu ya Katiba. Kwa sasa kinachoongelewa kwenye mchakato wa Katiba ni Muungano wakati kuna mambo mengi sana ndani ya Rasimu ya Katiba ambayo yanahitaji critical observation and examination kama inavyofanyika kwenye swala la Muungano.

hadi leo hii kuna watu bado eti wanaota ndoto ya Serikali moja ??
kumbuka kwamb Muungano huu ni wa nchi mbili huru, na katu kwetu sisi Wazanzibar hatupo tayari kupoteza identity yetu ya asili kwa kusarenda kumezwa na Tanganyika, iliyojivisha Utanzania!!
Ikiwa CCM mumeshindw kutafuta ufumbuzi wa kero za Muungano, Wazanzibar tayari tumeshatatua tatizo hilo kupitia Muungano wa Mkataba (60%) ili kila mshirika awe na Uhuru wa kujiamulia mambo yake!!
 
tunataka Tz bara/Tanganyika ambayo haiwi bullied na watu m1.5/m2 ya chao ni chao na chetu ni chao
 
Namuunga mkono moja kwa moja eti mtu ana miaka 25 eti kwa sababu kapata tiketi ya kuingia bungeni kama mjumbe unasikia anasema serikali Tatu wakati hata wakati Tanganyika inapata uhuru hakuwepo,Pinda nakupongeza kwa msimamo wako thabiti
kwa mawazo kama yako basi ni bora wanao tunga katiba wawe wa zee tu na hatuhitaji kubadirisha kitu chochote ambacho hatujawai kukiona
 
Nimejitahidi sana kufuatilia matamko yanayotolewa na viongozi wa chama tawala wanapotetea serikali mbili zilizoboreshwa kuwa ndio suluhu ya kero za Muungano nimeshindwa kuwaelewa kabisa.

Sijui woga wa kuiogopa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar unatokana na nini. Kwa vyovyote vile ilivyo mawazo yao ni kuwa Zanzibar ndio kwenye malalamiko na Tanzania Bara kuko shwari. Mawazo haya ni potofu kabisa na hayawezi kutoka kwa mtu ambaye ana elimu na upeo wa kuona mbali. Sauti ya Zanzibar iko juu kwa sababu wana serikali yao ambayo ina mamlaka katika masuala yasiyo ya Muungano. Kuiongozea mamlaka serikali ya Zanzibar maana yake ni kupunguza mambo ya Muungano.

Kupunguza masuala ya kushirikiana ndio kuupunguza nguvu Muungano wenyewe. Hali itabaki ni ile ile ya Serikali ya Muungano kuwa koti la kuifunika Serikali ya Tanganyika na Wazanzibar hawatalikubali hilo. Wakati huu hali itakuwa mbaya sana kwani tayari Zanzibar watakuwa wamekwishapewa yale yote wanayoyadai kwa sasa na hivyo watakachofanya ni kuamua kujiondoa ndani ya Muungano.

Kwa upande wa pili wananchi wa Tanzania Bara wanaonekana kutokuwa na sauti kubwa sana katika kudai mambo yao jambo ambalo sio kweli. Sauti yao haisikiki sana kwa kuwa hakuna chombo kinachowaunganisha na kuifikisha sauti yao kwenye majukwaa ya nchi na kimataifa. Hali hii yaweza kuwa ya mpito tu kwani ukweli ulioko huku chini ni kuwa wananchi wameanza kuelewa na kuwa wadadisi wa masuala yanayohusu nchi.

Wengi na hasa vijana wanauliza maswali inakuwaje Zanzibar wawe na "Identity" lakini watu wa Bara wasiwe na hiyo "identity" yao? Je, "identity" ni haki ya Wazanzibar tu? Naamini sasa CCM kimepoteza ukaribu na wananchi wake na hivyo hakina taarifa sahihi ya kinachoendelea. Kama wamekuwa wakitegemea taarifa za uongo za kuwafurahisha wawapo kwenye vikao kutoka kwa watendaji wao ambao huku mtaani wamechoka na hawana ubunifu basi wanapokea taarifa ambazo sio sahihi.

Wananchi wa Tanzania Bara kutokuwa na mahali pa kusemea ni jambo la hatari sana kwa mstakabali wa Muungano wenyewe. Tena kwa mtazamo wangu Zanzibar haipaswi kuogopwa hata kidogo kwa sababu wao kwa hulka ni wasemaji na walalamikaji. Watalaam wa Saikolojia wanasema mtu anayesema yale yanayomkera ni mzuri kuliko asiyependa kusema kwani huwezi kujua ni jambo lipi linalomkera. Kumbe watu wa Bara wanazo kero nyingi sana za Muungano kuliko wa upande wa pili lakini huenda CCM hawajajisumbua kuzitafuta.

Jaji Warioba amewasaidia kuziweka kero za watu wa Tanganyika hadharani kama zilivyowahi kufanya Tume nyingine zilizopita kwa lengo la kuwasaidia watawala kuuona ukweli. Hata hivyo CCM kama kawaida yao wamejifunika kitambaa cheusi usoni na kuziba masikio na kupayuka kwa sauti kubwa kuwa watu wa Bara hawajasema aliyoyaandika Warioba.

Ukweli uliodhahiri sasa ni kwamba CCM hawautakii mema Muungano wetu, wao ndo watauvunja kwa hoja dhaifu ya kuwafurahisha Wazanzibar
 
Kumbe ana miaka 66 sasa! Anatarajia kustaafu lini apishe damu changa?
 
''Tanzania Bara na Zanzibar wana historia ya udugu na ushirikiano. Ukaribu, lugha moja na kuoleana,” alisema Pinda.

..Tunalinda Muungano ili tuendelee kuoleana..
 
Back
Top Bottom