Miti ya majirani ni kero

Miti ya majirani ni kero

Bin Chuma75

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2012
Posts
1,002
Reaction score
1,092
Habarini wakuu! Naombeni msaada wa kujua nitumie njia gani ya kukausha miti ya jirani yangu, kwa kweli kwangu ni kero halafu sio mstaarabu, hata nikimuomba mimi niipunguze tunasumbuana bila sababu za msingi, nataka nipate dawa/sumu niikaushe tu kimyakimya bila kujua, sipendi magomvi nae wakuu, natesa familia yangu kusafisha uwanja kila wakati.
IMG_1513667310.348976.jpg
IMG_1513667476.974384.jpg
IMG_1513667476.974384.jpg
 

Attachments

  • IMG_1513667533.198116.jpg
    IMG_1513667533.198116.jpg
    94.6 KB · Views: 53
Kama unaona mjumbe hatatenda haki basi nenda kwenye ofisi ya kata katoe malamiko yako hapo....mambo ya sumu achana nayo hii case ni rahisi sana upande wako...
 
Hii nchi yetu ya kijamaa mtu hatarajii mgombane kisa mti wake unachungulia uwanjani kwako.

Kama ingekua inakua dawa ipo ila hapo ishaota mpaka ndevu ni ama uwe unaikata wewe mwenyewe na akija kukuongelesha unamkalia kimya au uwe unazoa majani na kutupa uwanjani kwake.

Ila pia unaweza ukapandisha ua wako kama hutaki ujinga
 
Ni trespass hiyo nenda mahakamani kama hataki kuipunguza
 
Nakupa mbinu, ukifumwa shauri zako.
Chukua msumari...upake chumvi mbele kisha nenda kaugongelee kwenye mti wenyewe.
Usigongelee kwenye matawi....gongelea kwenye mti wenyewe mkubwa.
Ndani ya mwezi utakauka wote.
Tumekausha sana miembe na misandarusi kwa style hii.
NB:
Pigilia misumari hata 4 ila uhakikishe yote imezama mpaka ndani.
Ndani ya mwezi njoo unipe feedback
 
Mpeleke mahakamani, miti atakata kwa gharama zake na fidia atakulipa vizuri tu
 
Habarini wakuu! Naombeni msaada wa kujua nitumie njia gani ya kukausha miti ya jirani yangu, kwa kweli kwangu ni kero halafu sio mstaarabu, hata nikimuomba mimi niipunguze tunasumbuana bila sababu za msingi, nataka nipate dawa/sumu niikaushe tu kimyakimya bila kujua, sipendi magomvi nae wakuu, natesa familia yangu kusafisha uwanja kila wakati.View attachment 654248View attachment 654249View attachment 654249
Kwenye pic mie sijaona shida yoyote hapo. Labda kama kuna shida nyengine hujaiweka hapa...
 
Mkuu kabla yakuikausha hiyo miti sikiliza hili ngoma kwanza

 
nimejaribu kuzoom naona matawi ya hiyo miti yanagusa hizo nyaya za umeme sasa siku mvua ikinyesha mti ukalowa atakuja kujinyea mtu hapo,halafu mti wenyewe unaonekana sio wa matunda ni kivuli angefanya tu kuupunguza
0b6c30569bb8d7965ca1cc9cee4bcf62.jpg
 
Pole sana alafu ni ile miti kunuka nuka. Kamshtaki kwa mjumbe na TANESCO maana umegusa hadi nyaya.
 
Chumvi huwa inamwagiwa endapo ingekuwa imekatwa, unamwagia pale kwenye round juu ili usichipue.
Agongelee tu misumari.
Inakauka kimya kimya
nilijaribu kumwagia sufuria la chumvi ya unga kwenye mwembe wa jirani eti alikuja kuupanda kwenye mpaka,ulikauka fasta
 
Back
Top Bottom